حِصْنُ المُسْلِمِ
مِنْ أَذْكَارِ الكِتَابِ وَالسُّنَّةِ
Hisnu Al-Muslim Kutoka Katika Nyiradi Za Kitabu Na Sunna
د. سَعِيدُ بْنُ عَلِيِّ بْنِ وَهْفٍ الْقَحْطَانِيُّ
Mhitaji kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu
Dkt. Sa'id bin Ali bin Wahf Al-Qahtani
بِسْمِ اللهِ الرَّحمَنِ الرَّحِيمِ
Hisnu Al-Muslim Kutoka Katika Nyiradi Za Kitabu Na Sunna
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
Utangulizi
Hakika sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Tunamsifu, tunamuomba msaada, na tunamuomba maghufira. Na tunajikinga kwa Mwenyezi Mungu, kutokana na uovu wa nafsi zetu, na mabaya ya matendo yetu. Yule ambaye Mwenyezi Mungu amemwongoa, basi hakuna wa kumpoteza. Na yule ambaye amempoteza, basi hakuna wa kumwongoa. Ninashuhudia kwamba hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, hali ya kuwa peke yake, hana mshirika³. Na ninashuhudia kwamba Muhammad ni mja wake na ni Mtume wake, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, na ziwe juu ya jamaa zake, Maswahaba wake na wote wanaowafuata hao kwa wema mpaka Siku ya Malipo. Ama baada ya hayo:
Huu ni muhtasari nilioufupisha kutoka katika kitabu changu: Adh-Dhikru wad-Du'aa wal-'ilaaju birruqaa minal-kitabi wassunnati (Nyiradi na Dua na Kujitibu kwa kutumia Qur-ani na Sunna)1, nimeifanyia ufupisho sehemu yake ya Adhkari (nyiradi); ili iwe ni wepesi kukibeba katika safari.
Na kwa hakika nimeishia kwenye matini (maneno ya Mtume) ya dhikri, na nimetosheka katika kueleza mahali inapopatikana kwa kutaja chimbuko moja au mawili miongoni mwa yale yaliyopatikana katika kitabu cha asili, na anayetaka kumjua Sahaba au ziada katika kueleza daraja za hadithi, basi anapaswa kurejea katika kitabu cha asili.
Na ninamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa majina yake mazuri na sifa zake za juu zaidi akifanye kiwe ni kwa ajili ya kupata radhi zake Mwenyezi mungu mtukufu, na aninufaishe nacho katika uhai wangu, na baada ya kufa kwangu, na amnufaishe nacho kila atakayekisoma, au kukichapisha, au atakayesaidia katika kusambaa kwake. Hakika Yeye, aliyetakasika, ndiye Msimamiaji wa hayo na ndiye Muweza wa kufanya hivyo. Na rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Nabii wetu Muhammad, na familia yake na Maswahaba wake, na wote wanaowafuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.
Mtunzi
Kiliandikwa mwezi wa Safar 1409 Hijria
***
Ubora wa kumtaja Mwenyezi Mungu (dhikiri)
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
﴿فَٱذۡكُرُونِيٓ أَذۡكُرۡكُمۡ وَٱشۡكُرُواْ لِي وَلَا تَكۡفُرُونِ 152﴾
"Basi nitajeni, nitakutajeni. Na nishukuruni, wala msinikufuru."2
﴿يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ ذِكۡرٗا كَثِيرٗا41﴾
"Enyi mlioamini! Mdhukuruni Mwenyezi Mungu kwa wingi wa kumdhukuru."3
﴿...وَالذَّاكِرِينَ اللَّهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا﴾
"..na wanaume wanaomdhukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi na wanawake wanaomdhukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi, Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na ujira mkubwa."4
﴿وَٱذۡكُر رَّبَّكَ فِي نَفۡسِكَ تَضَرُّعٗا وَخِيفَةٗ وَدُونَ ٱلۡجَهۡرِ مِنَ ٱلۡقَوۡلِ بِٱلۡغُدُوِّ وَٱلۡأٓصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡغَٰفِلِينَ 205﴾
"Na mkumbuke Mola wako Mlezi katika nafsi yako kwa unyenyekevu na hofu, na bila ya kuinua sauti juu kwa kauli, asubuhi na jioni, wala usiwe miongoni wa walioghafilika."5
Na alisema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie: "Mfano wa yule anayemtaja Mola wake Mlezi na yule asiyemtaja Mola wake Mlezi, ni mfano wa aliye hai na aliyekufa."6
Na alisema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie: "Je, nisiwaambieni matendo bora zaidi kwenu, na masafi zaidi mbele ya Mfalme wenu, na yatakayo kunyanyueni juu zaidi katika daraja zenu, na bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na pesa, na bora kwenu kuliko hata kukutana na adui yenu na mkapiga shingo zao na wakapiga shingo zenu?" Wakasema: Ndiyo. “Ni kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu.”7
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Mwenyezi Mungu anasema: "Mimi niko pamoja na dhana ya mja wangu kwangu, na mimi nipo naye anaponitaja. Atakaponitaja kwenye nafsi yake, nitamtaja kwenye nafsi yangu, na atakaponitaja kwenye mkusanyiko, nitamtaja kwenye mkusanyiko bora kuliko wao. Na akijiweka karibu yangu kwa kiasi cha shibri (umbali wa kati ya kidole kidogo na kidole gumba) moja, nitakuwa karibu yake kwa kiasi cha dhiraa moja. Na akijiweka karibu yangu kwa kiasi cha dhiraa moja, nitakuwa karibu yake kiasi cha baa (kiasi cha mikono miwili iliyokunjuliwa) moja. Na akinijia kwa kutembea, nitamuendea kwa kukimbia."8
Na imesimuliwa kutoka kwa Abdallah bin Busri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake ya kwamba mtu mmoja alisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika sheria za Uislamu zimekuwa nyingi kwangu, hebu nieleze kitu ambacho nitashikamana nacho. Akasema: "Ulimi wako usiache kuwa mbichi kwa kumtaja Mwenyezi Mungu"9,
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayesoma herufi moja katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, basi atapata jema moja kwa herufi hiyo. Na jema hilo hulipwa mara kumi mfano wake. Sisemi: 'Alif Laam Miim' ni herufi moja, lakini: Alif ni herufi, na Laam ni herufi, na Miim ni herufi."10
Na imepokelewa kutoka kwa Uqba bin Aamir -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Alitoka Mtume rehema na amani ziwe juu yake na sisi tukiwa katika Suffah, akasema: "Yupi miongoni mwenu anapenda atoke nyakati za asubuhi kila siku aende Jangwani au Aqiiq (Soko), alete kutoka huko Ngamia wawili walio nona bila ya tatizo, wala kukata udugu?" Tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu tunalipenda hilo. Akasema: "Bora aende mmoja wenu Msikitini ajifunze, au asome aya mbili kutoka katika kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu, ni bora kwake yeye kuliko ngamia wawili. Na aya tatu ni bora kwake kuliko ngamia watatu. Na aya nne ni bora kwake kuliko ngamia wanne. Na idadi nyingineyo ni bora kuliko idadi yake katika ngamia."11
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Mwenye kukaa kikao chochote akawa hakumtaja Mwenyezi Mungu ndani yake, atakuwa na majuto kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na mwenye kujilaza mahali popote akawa hakumtaja Mwenyezi Mungu ndani yake, atakuwa na majuto kutoka kwa Mwenyezi Mungu."12
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Hawajawahi kukaa watu kikao chochote wakawa hawakumtaja Mwenyezi Mungu ndani yake, na wala hawakumsalia Nabii wao, isipokuwa itakuwa ni hasara juu yao, akitaka atawaadhibu, na akitaka atawasamehe."13
Na amesema Rehema na Amani ziwe juu yake: "Hakuna watu wowote watasimama katika kikao ambacho hawamtaji Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani yake, isipokuwa watanyanyuka kutoka kwenye mithili ya mzoga wa punda, na watakuwa na majuto."14
1. NYIRADI ZA KUAMKA KUTOKA USINGIZINI
Tafsiri: "Kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyetuhuisha baada ya kutufisha na kwake tutafufuliwa."15
(الحَمْدُ للَّهِ الَّذِي أَحْيَانَا بَعْدَ مَا أَمَاتَنَا، وَإِلَيْهِ النُّشُور).
Al-hamdulillaahi lladhi ah-yaanaa baada maa amaatanaa wailaihin-nushuur
Tafsiri: "Hakuna mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu peke yake, hana mshirika. Ni wake ufalme na ni zake sifa njema, naye ni Muweza wa kila kitu. Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu peke yake, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, aliye juu, Mkuu. Mola wangu Mlezi, nisamehe."16
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَريكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، سُبْحَانَ اللَّهِ، وَالحَمْدُ للَّهِ، وَلَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكبَرُ، وَلَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّهِ العَلِيِّ العَظِيمِ، رَبِّ اغْفرْ لِي).
La ilāha illallāh wahdahu la sharīka lah, lahu al-mulku wa lahu al-hamdu, wa huwa ‘ala kulli shay’in qadīr. Subhānallāh, wal-hamdulillāh, wa la ilāha illallāh, wallāhu akbar, wa la hawla wa la quwwata illa billāh al-‘aliyy al-‘adhwīm. Rabbighfir lī.
Tafsiri: "Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyenipa salama mimi katika mwili wangu, na akanirejeshea roho yangu, na akaniidhinisha mimi kumtaja."17
(الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي عَافَانِي فِي جَسَدِي، وَرَدَّ عَلَيَّ رُوحِي، وَأَذِنَ لِي بِذِكْرِه).
Al-hamdulillaahi lladhii aafaanii fii jasadii, waradda alaiyya ruuhi, wa adhina lii bidhikrihi
﴿إِنَّ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱخۡتِلَٰفِ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ لَأٓيَٰتٖ لِّأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ 190 ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَٰمٗا وَقُعُودٗا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَٰذَا بَٰطِلٗا سُبۡحَٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ 191 رَبَّنَآ إِنَّكَ مَن تُدۡخِلِ ٱلنَّارَ فَقَدۡ أَخۡزَيۡتَهُۥۖ وَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ192 رَّبَّنَآ إِنَّنَا سَمِعۡنَا مُنَادِيٗا يُنَادِي لِلۡإِيمَٰنِ أَنۡ ءَامِنُواْ بِرَبِّكُمۡ فَـَٔامَنَّاۚ رَبَّنَا فَٱغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرۡ عَنَّا سَيِّـَٔاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ ٱلۡأَبۡرَارِ 193 رَبَّنَا وَءَاتِنَا مَا وَعَدتَّنَا عَلَىٰ رُسُلِكَ وَلَا تُخۡزِنَا يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ إِنَّكَ لَا تُخۡلِفُ ٱلۡمِيعَادَ 194 فَٱسۡتَجَابَ لَهُمۡ رَبُّهُمۡ أَنِّي لَآ أُضِيعُ عَمَلَ عَٰمِلٖ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوۡ أُنثَىٰۖ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۖ فَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ وَأُخۡرِجُواْ مِن دِيَٰرِهِمۡ وَأُوذُواْ فِي سَبِيلِي وَقَٰتَلُواْ وَقُتِلُواْ لَأُكَفِّرَنَّ عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَلَأُدۡخِلَنَّهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ ثَوَابٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ عِندَهُۥ حُسۡنُ ٱلثَّوَابِ 195 لَا يَغُرَّنَّكَ تَقَلُّبُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ 196 مَتَٰعٞ قَلِيلٞ ثُمَّ مَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ 197 لَٰكِنِ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ رَبَّهُمۡ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا نُزُلٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۗ وَمَا عِندَ ٱللَّهِ خَيۡرٞ لِّلۡأَبۡرَارِ 198 وَإِنَّ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَمَن يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِمۡ خَٰشِعِينَ لِلَّهِ لَا يَشۡتَرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ 199 يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱصۡبِرُواْ وَصَابِرُواْ وَرَابِطُواْ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ 200﴾
"Hakika, katika kuumbwa mbingu na ardhi na kuhitilafiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili ya hali ya juu.
Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu hali ya kuwa wamesimama, na wamekaa, na wamelala kwa ubavu wao. Na hutafakari katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi viumbe bure. Subhanaka (umetakasika)! Basi tukinge kutokana na adhabu ya Moto.
Mola wetu Mlezi! Hakika, yule unayemwingiza Motoni, basi umemfedhehesha. Na waliodhulumu hawana wasaidizi wowote.
Mola wetu Mlezi! Hakika, sisi tumemsikia mwitaji akiita kwenye Imani kwamba: 'Muaminini Mola wenu Mlezi'; kwa hivyo, tukaamini. Basi tufutie dhambi zetu, na utufunikie makosa yetu, na utufishe pamoja na walio wema.
Mola wetu Mlezi! Na tupe yale uliyotuahidi kwa Mitume wako, wala usitudhalilishe Siku ya Kiyama. Hakika, Wewe huvunji miadi.
Basi, Mola wao Mlezi akayakubali maombi yao akayajibu: Hakika Mimi, sipotezi matendo ya mfanya matendo yeyote miongoni mwenu, akiwa mwanamume au mwanamke, kwani ni nyinyi kwa nyinyi. Basi waliohama, na waliotolewa katika makazi yao, na wakaudhiwa katika Njia yangu, na wakapigana vita, na wakauliwa, kwa yakini Mimi nitawafunikia makosa yao; na kwa yakini nitawaingiza katika Mabustani yanayopita mito chini yake. Hizo ndizo thawabu zinazotoka kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu kwake kuna thawabu njema kabisa.
Kamwe kusiwadanganye kutangatanga kwa wale waliokufuru katika nchi.
Hiyo ni starehe ndogo. Kisha makazi yao yatakuwa Jahannamu. Na ni pahali pabaya mno pa kupumzikia.
Lakini wale waliomcha Mola wao Mlezi wana Mabustani yanayopita mito chini yake. Watadumu humo. Hayo ni makaribisho yao yatokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na vilivyo kwa Mwenyezi Mungu ni bora kwa walio wema.
Na hakika, miongoni mwa Watu wa Kitabu kuna wale wanaomwamini Mwenyezi Mungu na yaliyoteremshwa kwenu na yaliyoteremshwa kwao, wakimnyenyekea Mwenyezi Mungu. Hawanunui kwa Aya za Mwenyezi Mungu thamani ndogo. Hao wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi. Hakika, Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhesabu.
Enyi mlioamini! Subirini, na vumilieni, na kuweni macho, na mcheni Mwenyezi Mungu, ili mpate kufaulu."
[Al Imran: 190-200]18.
2. DUA YA KUVAA NGUO
"Alhamdulillaahil ladhi kasaani haadhaa (ath-thauba) warazaqaniihi min ghairi haulin minni walaa quwwatin...". yaani, kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyenivisha (nguo) hii na akaniruzuku hiyo si kwa ujanja wangu wala si kwa nguvu yangu...19.
(الحَمْدُ للَّهِ الَّذِي كَسَانِي هَذَا (الثَّوْبَ) وَرَزَقَنِيهِ مِنْ غَيْرِ حَوْلٍ مِنِّي وَلَّا قُوَّة).
Alhamdulillaahil ladhi kasaani haadhaa (ath-thauba) warazaqaniihi min ghairi haulin minni walaa quwwatin
3. DUA YA KUVAA NGUO MPYA
Tafsiri: "Ewe Mwenyezi Mungu ni zako kila sifa njema, wewe ndiye uliyenivisha nguo hii, ninakuomba mazuri yake na mazuri iliyotengenezewa, na ninajilinda kwako kutokana na shari zake na shari ilizotengenezewa."20
(اللَّهُمَّ لَكَ الحَمْدُ أَنْتَ كَسَوْتَنِيهِ، أَسْأَلُكَ مِنْ خَيْرِهِ وَخَيْرِ مَا صُنِعَ لَهُ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهِ وَشَرِّ مَا صُنِعَ لَه).
Allahumma lakal hamdu anta kasautanihi, as-aluka min khairihi wa khairi ma sunia lahu, wa audhu bika min sharrihi wa sharri ma sunia lah.
4. DUA YA KUMUOMBEA ALIYEVAA NGUO MPYA
Tafsiri: "Utaivaa hadi ichakae, na Mwenyezi Mungu Mtukufu atakupa nyingine."21
(تُبْلِي وَيُخْلِفُ اللَّهُ تَعَالَى).
Tublii wa yukhliful laahu Taalaa
Tafsiri: "Vaa kipya, na uishi ukiwa mwenye kusifiwa, na ufe shahidi."22
(اِلبَسْ جَدِيدًا، وَعِشْ حَمِيدًا، وَمُتْ شَهِيدًا).
Ilbas jadidan, waish hamidan, wamut shahidan.
5. ANACHOSEMA ANAPOVUA NGUO YAKE
Tafsiri: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu."23
(بِسْمِ اللَّه).
Bismillah
6. DUA YA KUINGIA CHOONI
Tafsiri: "[Kwa jina la Mwenyezi Mungu]. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwako kutokana na mashetani wa kiume na mashetani wa kike."24
([بِسْمِ اللَّهِ] اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ الخُبْثِ وَالخَبَائِث).
[Bismillaahi] Allahumma innii a'udhu bika minalkhubthi walkhabaaith
7. DUA YA KUTOKA CHOONI
Tafsiri: "Ninakuomba msamaha (ewe Mwenyezi Mungu)."25
(غُفْرَانَك).
Ghufraanaka
8. DUA KABLA YA UDHU
Tafsiri: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu."26
(بِسْمِ اللَّه).
Bismillah
9. DHIKIRI BAADA YA KUMALIZA UDHU
"Ninashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu peke yake hana mshirika, na ninashuhudia kuwa Muhammad ni mja wake na ni Mtume wake."27
(أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ وَأَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُه).
Ash-hadu an laa ilaha illallahu, wahdahu laa shariika lahu, wa ash-hadu anna Muhammadan abduhu wa rasuluh.
"(Ewe Mola wangu nijaalie mimi kuwa miongoni mwa wenye kutubia, na unijaalie kuwa miongoni mwa wenye kujitwaharisha)."28
(اللَّهُمَّ اجْعَلْنِي مِنَ التَّوَّابِينَ وَاجْعَلْنِي مِنَ المُتَطَهِّرِين).
Allaahummaj'alniy minat tawwaabiina waj'alniy minal mutatwahhiriina
"(Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu, na sifa njema ni zako, ninashuhudia kuwa hapana Mola ila wewe, ninakuomba msamaha na ninatubia kwako."29
(سُبْحانَكَ اللَّهُمَّ وَبِحَمْدِكَ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَيْك).
Subhanaka Allahumma wa bihamdika, ash-hadu an la ilaha illa anta, astaghfiruka wa atubu ilaik
10. DHIKIRI WAKATI WA KUTOKA NYUMBANI
"(Kwa jina la Mwenyezi Mungu, nimemtegemea Mwenyezi Mungu, na wala hakuna uwezo wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu)."30
(بِسْمِ اللَّهِ، تَوَكَّلْتُ عَلَى اللَّهِ، وَلَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّّا بِاللَّه).
Bismillaahi, tawakkaltu 'alallaahi, walaa hawla walaa quwwata illaa billaahi
"Ewe Mola wangu wa haki, hakika mimi ninajikinga kwako ili nisipotee au kupotezwa, au kuteleza na kufanya kosa au kutelezeshwa na kufanya makosa, au kudhulumu au kudhulumiwa, au kufanya ujinga au kufanyiwa ujinga."31
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ أَنْ أَضِلَّ، أَوْ أُضَلَّ، أَوْ أَزِلَّ، أَوْ أُزَلَّ، أَوْ أَظْلِمَ، أَوْ أُظْلَمَ، أَوْ أَجْهَلَ، أَوْ يُجْهَلَ عَلَي).
Allahumma inni audhu bika an adhilla, au udhalla, au azilla, au uzalla, au adhlima, au udhlama, au ajhala, au yujhala alayya.
11. DHIKIRI WAKATI WA KUINGIA NYUMBANI
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu tumeingia, na kwa jina la Mwenyezi Mungu tulitoka, na kwa Mwenyezi Mungu Mola wetu ndiko tunakotegemea, kisha anawasalimia waliopo ndani."32
(بِسْمِ اللَّهِ وَلَجْنَا، وَبِسْمِ اللَّهِ خَرَجْنَا، وَعَلَى اللَّهِ رَبِّنَا تَوَكَّلْنَا).
Bismillah walajinaa, wabismillahi kharajinaa, wa a'laallahi Rabbinaa tawakkalna
12. DUA YA KWENDA MSIKITINI
"Ewe Mwenyezi Mungu uweke katika moyo wangu nuru, na katika ulimi wangu nuru, na katika masikio yangu nuru, na katika macho yangu nuru, na juu yangu nuru, na chini yangu nuru, na kuliani kwangu nuru, na kushotoni kwangu nuru, na mbele yangu nuru, na nyuma yangu nuru, na uweke katika nafsi yangu nuru, na uifanye kubwa nuru yangu, na uikuze nuru yangu, na unijaalie nuru, na unifanye kuwa nuru. Ewe Mwenyezi Mungu nipe nuru, na uweke katika mishipa yangu nuru, na katika nyama yangu nuru, na katika damu yangu nuru, na katika nywele zangu nuru, na katika ngozi yangu nuru."33
(اللَّهُمَّ اجْعَلْ فِي قَلْبِي نُورًا، وَفِي لِسَانِي نُورًا، وَفِي سَمْعِي نُورًا، وَفِي بَصَرِي نُورًا، وَمِنْ فَوْقِي نُورًا، وَمِنْ تَحْتِي نُورًا، وَعَنْ يَمِينِي نُورًا، وَعَنْ شِمَالِي نُورًا، وَمِنْ أَمَامِي نُورًا، وَمِنْ خَلْفِي نُورًا، وَاجْعَلْ فِي نَفْسِي نُورًا، وَأَعْظِمْ لِي نُورًا، وَعَظِّمْ لِي نُورًا، وَاجْعَلْ لِي نُورًا، وَاجْعَلْنِي نُورًا، اللَّهُمَّ أَعْطِنِي نُورًا، وَاجْعَلْ فِي عَصَبِي نُورًا، وَفِي لَحْمِي نُورًا، وَفِي دَمِي نُورًا، وَفِي شَعْرِي نُورًا، وَفِي بَشَرِي نُورًا).
Allahuma ijal fi kalbi nuran, wa fi lisani nuran, wa fi sami nuran, wa fi basari nuran, wa min fauki nuran, wa min tahti nuran, wa an yamini nuran, wa an shimali nuran, wa min amami nuran, wa min khalfi nuran, wajal fi nafsi nuran, wa adhim li nuran, wa adhim li nuran, wajal li nuran, wajalni nuran, Allahuma atini nuran, wajal fi asabi nuran, wa fi lahmi nuran, wa fi dami nuran, wa fi shaari nuran, wa fi bashari nuran.
"Ewe Mwenyezi Mungu, niwekee nuru katika kaburi langu... na nuru katika mifupa yangu."34 "na unizidishie nuru, na unizidishie nuru, na unizidishie nuru."35 "na unipe nuru juu ya nuru."36
(اللَّهُمَّ اجْعَلْ لِي نُورًا فِي قَبْرِي... وَنُورًا فِي عِظَامِي، وَزِدْنِي نُورًا، وَزِدْنِي نُورًا، وَزِدْنِي نُورًا، وَهَبْ لِي نُورًا عَلَى نُور).
Allahumma jaal lii nuuran fii kabri... wa nuuran fii idhaami, wa zidni nuuran, wa zidni nuuran, wa zidni nuuran, wa hab lii nuuran alaa nuur
13. DUA YA KUINGIA MSIKITINI
(Ataanza kwa mguu wake wa kulia)37, na atasema: "Ninajilinda kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwa uso wake Mkarimu, na kwa ufalme wake wa enzi, kutokana na shetani aliyelaaniwa."38
(أَعُوذُ بِاللَّهِ العَظِيمِ، وَبِوَجْهِهِ الكَرِيمِ، وَسُلْطَانِهِ القَدِيمِ، مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahil adhiim, wa bi wajhihil kariim, wa sultanihil qadiim, minash shaitanir rajiim.
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na rehema39 na salamu zimshukie Mtume wa Mwenyezi Mungu."40
(بِسْمِ اللَّهِ، وَالصَّلَاةُ وَالسَّلَامُ عَلَى رَسُولِ اللَّه).
Bismillahi, wasswalatu wassalamu ala Rasulillah
"Ewe Mola nifungulie milango ya rehema zako."41
(اللَّهُمَّ افْتَحْ لِي أَبْوَابَ رَحْمَتِك).
Allahumma iftah li abwaba rahmatik
14. DUA YA KUTOKA MSIKITINI
(Ataanza kwa mguu wake wa kushoto)42 na atasema: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na rehema na amani ziwe juu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu."
(بِسْمِ اللَّهِ وَالصَّلَاةُ وَالسَّلَامُ عَلَى رَسُولِ اللَّه).
Bismillahi wasalatu wasalamu ala rasulillah
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba unipe katika fadhila zako."
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ مِنْ فَضْلِك).
Allahumma inni as'aluka min fadhlik
"Ewe Mwenyezi Mungu nilinde kutokana na shetani aliyelaaniwa."43
(اللَّهُمَّ اعْصِمْنِي مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيم).
Allahuma asimni minash-shaitani ar-rajiim
15. DHIKIRI ZA ADHANA
Aseme kama anavyosema muadhini, isipokuwa katika "Hayya a'las swalaa" na "Hayya a'lal falaah", hapo atasema: "Hakuna uwezo wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu."44
(لَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّه).
Laa haula walaa kuwwata illaa billah
Atasema: "Na mimi ninashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu peke yake, hana mshirika, na kuwa Muhammad ni mja wake na ni Mtume wake, nimeridhia Mwenyezi Mungu kuwa Mola Mlezi, na Muhammad kuwa Mtume, na Uislamu kuwa dini."45
(وَأَنَا أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ وَأَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ، رَضِيتُ بِاللَّهِ رَبًَّا، وَبِمُحَمَّدٍ رَسُولًا، وَبِالإِسْلَامِ دِينًَا).
Wa ana ashhadu an laa ilaha illallahu wahdahu laa sharika lahu wa anna muhammadan abduhu wa rasuluhu, radhitu billahi rabban, wa bi muhammadin rasulan, wa bil islami diinan.
(Atasema hayo baada ya tashahhudi ya muadhini)46.
(Atamsalia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- baada ya kumaliza kumuitikia muadhini).47
Atasema: "Tafsiri: Ewe Mwenyezi Mungu Mola wa wito huu uliotimia, na swala iliyosimama, mpe Muhammadi wasiila (daraja) na fadhila, na umfufue kwenye nafasi yenye kusifiwa uliyomuahidi, [hakika Wewe huvunji ahadi]."48
(اللَّهُمَّ رَبَّ هَذِهِ الدَّعْوَةِ التَّامَّةِ، وَالصَّلَاةِ القَائِمَةِ، آتِ مُحَمَّدًا الوَسِيلَةَ وَالفَضِيلَةَ، وَابْعَثْهُ مَقَامًَا مَحمُودًا الَّذِي وَعَدْتَهُ، [إِنَّكَ لَا تُخْلِفُ المِيعَاد] ).
Allahumma rabba hadhihid daawatit taammati, was-swalatil qaaimati, aati muhammadanil wasiilata wal fadhilata, wab-ath-hu maqaaman mahmuudanil ladhi waadtahu, innaka laa tukhliful miiaad.
(Ajiombee dua baina ya adhana na iqaama, kwani dua wakati huo hairejeshwi)49.
16. DUA YA UFUNGUZI WA SWALA
"Ewe Mwenyezi Mungu weka mbali kati yangu na kati ya makosa yangu kama ulivyoweka mbali kati ya mashariki na magharibi. Ewe Mwenyezi Mungu nisafishe kutokana na makosa yangu kama inavyosafishwa nguo nyeupe kutokana na uchafu. Ewe Mwenyezi Mungu nioshe mimi kutokana na makosa yangu kwa barafu na maji na baridi."50
(اللَّهُمَّ بَاعِدْ بَيْنِي وَبَيْنَ خَطَايَايَ كَمَا بَاعَدْتَ بَيْنَ المَشْرِقِ وَالمَغْرِبِ، اللَّهُمَّ نَقِّنِي مِنْ خَطَايَايَ كَمَا يُنَقَّى الثَّوْبُ الأَبْيَضُ مِنَ الدَّنَسِ، اللَّهُمَّ اغْسِلْني مِنْ خَطَايَايَ، بِالثَّلْجِ وَالماءِ وَالبَرَد).
Allahumma baaid baini wa baina khatayaya kama baadta bainal mashriqi wal maghribi. Allahumma nakkini min khatayaya kama yunakkath thaubul abyadhu minad danasi. Allahumma ighsilni min khatayaaya, bith thalji wal mai wal baradi.
"Yaani: Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu, na sifa njema ni zako. Jina lako ni lenye baraka, na utukufu wako ni wa juu sana, wala hakuna mungu mwingine isipokuwa Wewe."51
(سُبْحانَكَ اللَّهُمَّ وَبِحَمْدِكَ، وَتَبارَكَ اسْمُكَ، وَتَعَالَى جَدُّكَ، وَلَا إِلَهَ غَيْرُك).
Subhanaka Allahumma wa bihamdika, wa tabaraka ismuka, wa taala jadduka, wa la ilaha ghairuk.
"Nimeuelekeza uso wangu kwa Yule aliyeumba mbingu na ardhi, hali ya kuelekea haki, na mimi si miongoni mwa washirikina, hakika swala yangu, na ibada zangu, na uhai wangu, na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu, hana mshirika, na kwa hilo nimeamrishwa na mimi ni miongoni mwa Waislamu. Ewe Mwenyezi Mungu wewe ndiye Mfalme, hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, wewe ndiye Mola Mlezi wangu na mimi ni mja wako, nimeidhulumu nafsi yangu na ninakiri kwa madhambi yangu, basi nisamehe mimi madhambi yangu yote, kwani hakuna afutae madhambi isipokuwa wewe, na niongoze kwenye tabia zilizo bora, hakuna aongozaye kwenye uzuri wake isipokuwa wewe, na niepushe na ubaya wake, hakuna aepushaye ubaya wake isipokuwa wewe, naitikia wito wako na kutii amri yako, na kheri yote ipo mikononi mwako, na shari haielekezwi kwako, mimi nipo kwa uwezo wako na narejea kwako, nimwenye baraka na umetukuka, nakuomba msamaha na ninatubu kwako."52
(وَجَّهْتُ وَجْهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ حَنِيفًَا وَمَا أَنَا مِنَ المُشْرِكِينَ، إِنَّ صَلَاتِي، وَنُسُكِي، وَمَحْيَايَ، وَمَمَاتِي لِلَّهِ رَبِّ العَالَمِينَ، لَا شَرِيكَ لَهُ وَبِذَلِكَ أُمِرْتُ وَأَنَا مِنَ المُسْلِمِينَ، اللَّهُمَّ أَنْتَ المَلِكُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَنْتَ رَبِّي وَأَنَا عَبْدُكَ، ظَلَمْتُ نَفْسِي وَاعْتَرَفْتُ بِذَنْبِي فَاغْفِرْ لِي ذُنُوبي جَمِيعًَا إِنَّهُ لَا يَغْفِرُ الذُّنوبَ إِلَّا أَنْتَ، وَاهْدِنِي لِأَحْسَنِ الأَخْلاقِ لَا يَهْدِي لِأَحْسَنِها إِلَّا أَنْتَ، وَاصْرِفْ عَنِّي سَيِّئَهَا، لَا يَصْرِفُ عَنِّي سَيِّئَهَا إِلَّا أَنْتَ، لَبَّيْكَ وَسَعْدَيْكَ، وَالخَيْرُ كُلُّهُ بِيَـدَيْكَ، وَالشَّرُّ لَيْسَ إِلَيْكَ، أَنَا بِكَ وَإِلَيْكَ، تَبارَكْتَ وَتَعَالَيْتَ، أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَيْك).
Wajjahtu wajhiya lilladhi fatwaras-samawati wal-ardha hanifan wa ma ana minal mushrikiin, inna swalati, wa nusuki, wa mahyaaya, wa mamaati lillahi rabbil aalamiin, la sharika lahu wa bidhalika umirtu wa ana minal muslimiin. Allahumma antal maliku la ilaha illa anta, anta rabbi wa ana abduka, dhalamtu nafsi wa ataraftu bi dhanbi faghfir li dhunubi jamiian innahu la yaghfirudh-dhunuba illa anta, wahdini li ahsanil akhlaqi la yahdi li ahsaniha illa anta, waswrif anni sayyiaha, la yaswrifu anni sayyiaha illa anta, labbaika wa saadaika, wal khairu kulluhu bi yadaika, wash-sharru laisa ilaika, ana bika wa ilaika, tabarakta wa taalaita, astaghfiruka wa atubu ilaik.
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa Jibril, Mikaili na Israfil, Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa siri na dhahiri, Wewe utahukumu baina ya waja wako katika yale waliyokuwa wakihitilafiana ndani yake. Niongoe kwenye haki katika yale waliyohitilafiana ndani yake kwa idhini yako. Hakika wewe unamuongoa umtakaye kwenye njia iliyonyooka."53
(اللَّهُمَّ رَبَّ جِبْرَائِيلَ، وَمِيْكَائِيلَ، وَإِسْرَافِيلَ، فَاطِرَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ، عَالِمَ الغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ أَنْتَ تَحْكُمُ بَيْنَ عِبَادِكَ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ، اهْدِنِي لِمَا اخْتُلِفَ فِيهِ مِنَ الحَقِّ بِإِذْنِكَ إِنَّكَ تَهْدِي مَنْ تَشَاءُ إِلَى صِرَاطٍ مُسْتَقيم).
Allahumma Rabba Jibraaiila, wa Miikaaiila, wa Israafiila, Faatwiras-samawaati wal-ardhi, Aalimal-ghaibi wash-shahaadati Anta tahkumu baina ibaadika fiimaa kaanuu fiihi yakhtalifuuna, Ihdinii limakhtulifa fiihi minal-haqqi bi idhnika Innaka tahdii man tashaau ilaa swiraatwim mustaqiim.
"(Mwenyezi Mungu ni Mkubwa sana, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa sana, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa sana, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu kwa wingi, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu kwa wingi, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu kwa wingi, na utakasifu ni wa Mwenyezi Mungu asubuhi na jioni)."
(اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيرًَا، اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيرًا، اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيرًا، وَالحَمْدُ لِلَّهِ كَثيرًا، وَالحَمْدُ لِلَّهِ كَثيرًا، وَالحَمْدُ لِلَّهِ كَثيرًا، وَسُبْحَانَ اللَّهِ بُكْرَةً وَأَصِيلًا).
Allahu akbaru kabiiran, Allahu akbaru kabiiran, Allahu akbaru kabiiran, Walhamdu lillahi kathiiran, Walhamdu lillahi kathiiran, Walhamdu lillahi kathiiran, Wa subhaanallahi bukratan wa asiila.
Mara tatu "Ninajilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Shetani: Kupulizia kwake hewa, na kupuliza kwake mate na kutia kwake wasiwasi (katika nyoyo za wanadamu).”54
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ: مِنْ نَفْخِهِ، وَنَفْثِهِ، وَهَمْزِه).
Audhu billahi minash shaitwani: min nafkhihi, wa nafthihi, wa hamzih.
"Yaani: Ewe Mwenyezi Mungu, sifa njema ni zako55, Wewe ni Nuru ya mbingu na ardhi na waliomo ndani yake, na sifa njema ni zako Wewe ni Msimamiaji wa mbingu na ardhi na waliomo ndani yake, [na sifa njema ni zako Wewe ni Mola wa mbingu na ardhi na waliomo ndani yake] [na sifa njema ni zako, ufalme wa mbingu na ardhi na waliomo ndani yake ni wako] [na sifa njema ni zako Wewe ni Mfalme wa mbingu na ardhi] [na sifa njema ni zako] [Wewe ni Haki, na ahadi yako ni haki, na kauli yako ni haki, na kukutana nawe ni haki, na Pepo ni haki, na Moto ni haki, na Manabii ni haki, na Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu zimshukie na amani, ni haki, na Kiyama ni haki] [Ewe Mwenyezi Mungu kwako nimejisalimisha, na kwako nimetegemea, na Wewe nimekuamini, na kwako nimerejea, na kwa uwezo wako nimegombana, na kwako nimehukumia. Basi nisamehe niliyoyatanguliza, na niliyoyachelewesha, na niliyoyaficha, na niliyoyadhihirisha] [na unayoyajua zaidi Wewe kuliko mimi] [Wewe ndiye Mwenye kutanguliza, na Wewe ndiye Mwenye kuchelewesha, hakuna mola isipokuwa Wewe] [Wewe ni Mola wangu, hakuna mola isipokuwa Wewe] [na hakuna uwezo wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu]."56
(اللَّهُمَّ لَكَ الحَمْدُ، أَنْتَ نُورُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ، وَلَكَ الحَمْدُ أَنْتَ قَيِّمُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ، [وَلَكَ الحَمْدُ أَنْتَ رَبُّ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ] [وَلَكَ الحَمْدُ لَكَ مُلْكُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ] [وَلَكَ الحَمْدُ أَنْتَ مَلِكُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ] [وَلَكَ الحَمْدُ] [أَنْتَ الحَقُّ، وَوَعْدُكَ الحَقُّ، وَقَوْلُكَ الحَقُّ، وَلِقاؤُكَ الحَقُّ، وَالجَنَّةُ حَقٌّ، وَالنَّارُ حَقٌّ، وَالنَّبِيُّونَ حَقٌّ، وَمحَمَّدٌ ﷺ حَقٌّ، وَالسَّاعَةُ حَقٌّ] [اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمتُ، وَعَلَيْكَ تَوَكَّلْتُ، وَبِكَ آمَنْتُ، وَإِلَيْكَ أَنَبْتُ، وَبِكَ خاصَمْتُ، وَإِلَيْكَ حاكَمْتُ. فَاغْفِرْ لِي مَا قَدَّمْتُ، وَمَا أَخَّرْتُ، وَمَا أَسْرَرْتُ، وَمَا أَعْلَنْتُ] [وَمَا أَنْتَ أَعْلَمُ بِهِ مِنِّي] [أَنْتَ المُقَدِّمُ، وَأَنْتَ المُؤَخِّرُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ] [أَنْتَ إِلَهِي لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ] [وَلَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّه] ).
Allahumma lakal hamdu, anta nurus-samawati wal-ardhi wa man fihinna, wa lakal hamdu anta qayyimus-samawati wal-ardhi wa man fihinna, wa lakal hamdu anta rabbus-samawati wal-ardhi wa man fihinna, wa lakal hamdu laka mulkus-samawati wal-ardhi wa man fihinna, wa lakal hamdu anta malikus-samawati wal-ardhi, wa lakal hamdu, antal haqqu, wa wa'dukal haqqu, wa qawlukal haqqu, wa liqaukal haqqu, wal jannatu haqqun, wan naru haqqun, wan nabiyyuna haqqun, wa Muhammadun sallallahu alayhi wasallam haqqun, was sa'atu haqqun. Allahumma laka aslamtu, wa alayka tawakkaltu, wa bika amantu, wa ilayka anabtu, wa bika khasamtu, wa ilayka hakamtu. Faghfir li ma qaddamtu, wa ma akhartu, wa ma asrartu, wa ma a'lantu, wa ma anta a'lamu bihi minni. Antal muqaddimu, wa antal mu'akhiru la ilaha illa anta, anta ilahi la ilaha illa anta, wa la hawla wa la quwwata illa billah.
17. DUA YA RUKUU
"Utakasifu ni wa Mola wangu Mlezi aliye Mkuu."
(سُبْحانَ رَبِّيَ العَظِيم).
Subhaana Rabbiyal Adhiim
Mara tatu57.
Yaani: Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu, Mola wetu Mlezi, na sifa njema zote ni zako. Ewe Mwenyezi Mungu, nisamehe."58.
(سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي).
Subhanaka Allahumma Rabbana wa bihamdik, Allahummaghfir li
"Yaani: Sifa za hali ya juu, na utukufu wa hali ya juu, ni wa Mola Mlezi wa Malaika na roho (Jibrili)."59
(سُبُّوُحٌ، قُدُّوسٌ، رَبُّ المَلَائِكَةِ وَالرُّوح).
Subbuhun, Quddusun, Rabbul malaikati warruh.
"Ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili yako nimerukuu, na kwako nimeamini, na kwa ajili yako nimejisalimisha, yamenyenyekea kwako masikio yangu, na macho yangu, na ubongo wangu, na mifupa yangu, na mishipa yangu, [na kilichobebwa na miguu yangu]."60
(اللَّهُمَّ لَكَ رَكَعْتُ، وَبِكَ آمَنْتُ، وَلَكَ أَسْلَمْتُ، خَشَعَ لَكَ سَمْعِي، وَبَصَرِي، وَمُخِّي، وَعَظْمِي، وَعَصَبِي، [وَمَا استَقَلَّتْ بِهِ قَدَمِي] ).
Allahumma laka rakaatu, wa bika aamantu, wa laka aslamtu, khashaa laka samii, wa basarii, wa mukhii, wa adhmii, wa asabii, wa ma staqallat bihi qadamii.
"Ametakasika yule mwenye kufanya atakavyo, mwenye ufalme, mwenye ukubwa na ukuu."61
(سُبْحَانَ ذِي الجَبَرُوتِ، وَالمَلَكُوتِ، وَالكِبْرِيَاءِ، وَالعَظَمَة
Subhaana dhil jabaruuti, wal malakuuti, wal kibriyaai, wal adhama.
18. DUA YA KUNYANYUKA KUTOKA KATIKA RUKUU
(Amemsikia Mwenyezi Mungu mwenye kumhimidi)62.
(سَمِعَ اللَّهُ لِمَنْ حَمِدَه).
Samiallahu liman hamidah
"Yaani: Mola wetu Mlezi na sifa njema ni zako, shukrani nyingi nzuri zenye baraka ndani yake."63
(رَبَّنَا وَلَكَ الحَمْدُ، حَمْدًا كَثيرًا طَيِّبًا مُبارَكًا فِيه).
Rabbanaa wa lakal hamdu, hamdan kathiiran tayyiban mubaarakan fiih
"Yaani: Ujazo wa mbingu na ujazo wa ardhi, na vilivyo baina ya viwili hivyo, na ujazo wa chochote ukitakacho baada yake. Unastahiki zaidi sifa njema na utukufu, haya ni maneno ya haki zaidi aliyoyasema mja, nasi sote ni waja wako. Ewe Mwenyezi Mungu, hakuna wa kuzuia uliyoyatoa, wala wa kuyatoa uliyoyazuia, wala hawezi kunufaisha mwenye utukufu (yeyote) kuliko Wewe ewe Mtukufu."64
(مِلْءَ السَّمَوَاتِ وَمِلْءَ الأَرْضِ، وَمَا بَيْنَهُمَا، وَمِلْءَ مَا شِئْتَ مِنْ شَيءٍ بَعْدُ. أَهلَ الثَّناءِ وَالمَجْدِ، أَحَقُّ مَا قَالَ العَبْدُ، وَكُلُّنَا لَكَ عَبْدٌ، اللَّهُمَّ لَا مَانِعَ لِمَا أَعْطَيْتَ، وَلَا مُعْطِيَ لِمَا مَنَعْتَ، وَلَا يَنْفَعُ ذَا الجَدِّ مِنْكَ الجَد).
Mil-as samawati wa mil-al ardhi, wa ma baynahuma, wa mil-a ma shiita min shayin baadu. Ahla thanai wal majdi, ahakku ma kalal abdu, wa kulluna laka abdun, Allahumma la mania lima aatayta, wala muutiya lima manaata, wala yanfau dhal jaddi minkal jad.
19. DUA NDANI YA SIJIDA
"Yaani: Utakasifu ni wa Mola wangu Mlezi aliye wa juu zaidi."
(سُبْحَانَ رَبِّيَ الأَعْلَى).
Subhana Rabbiyal Alaa
Mara tatu65.
"Maana yake: Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu, Mola wetu Mlezi, na sifa njema zote ni zako. Ewe Mwenyezi Mungu, nisamehe."66
(سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي).
Subhanaka Allahumma Rabbana wa bihamdika, Allahummaghfir li
"Yaani: Sifa za hali ya juu, na utukufu wa hali ya juu, ni wa Mola Mlezi wa Malaika na roho (Jibrili)."67
(سُبُّوحٌ، قُدُّوسٌ، رَبُّ المَلَائِكَةِ وَالرُّوح).
Subbuhun, Quddusun, Rabbul malaikati warruh
"Ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili yako nimesujudu na kwako nimeamini, na kwa ajili yako nimejisalimisha, umesujudu uso wangu kwa yule aliyeuumba, na akaupa sura, na akapasua masikio yake na macho yake. Ametukuka Mwenyezi Mungu mbora wa waumbaji."68
(اللَّهُمَّ لَكَ سَجَدْتُ وَبِكَ آمَنْتُ، وَلَكَ أَسْلَمْتُ، سَجَدَ وَجْهِيَ لِلَّذِي خَلَقَهُ، وَصَوَّرَهُ، وَشَقَّ سَمْعَهُ وَبَصَرَهُ، تَبَارَكَ اللَّهُ أَحْسَنُ الخَالِقِين).
Allahumma laka sajadtu wa bika aamantu, wa laka aslamtu, sajada wajhiya lilladhii khalakahu, wa sawwarahu, wa shakka sam'ahu wa basarahu, tabaarakallahu ahsanul khaaliqiin.
"Ametakasika yule mwenye kufanya atakavyo, mwenye ufalme, mwenye ukubwa na ukuu."69
(سُبْحَانَ ذِي الجَبَرُوتِ، وَالمَلَكُوتِ، وَالكِبْرِيَاءِ، وَالعَظَمَة).
Subhaana dhil jabaruuti, wal malakuuti, wal kibriyaai, wal adhamah.
"Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe mimi dhambi zangu: ndogo zake na kubwa zake, za mwanzo wake na mwisho wake, za wazi zake na za siri zake."70
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي ذَنْبِي كُلَّهُ: دِقَّهُ وَجِلَّهُ، وَأَوَّلَهُ وَآخِرَهُ، وَعَلَانِيَّتَهُ وَسِرَّه).
Allahumma ighfir li dhambi kullahu: diqqahu wa jillahu, wa awwalahu wa akhirahu, wa alaniyyatahu wa sirrah.
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najikinga kwa radhi zako kutokana na hasira zako, na kwa usalama wako kutokana na adhabu zako, na ninajikinga kwako kutokana na Wewe, siwezi kuhesabu sifa zako, kama ulivyojisifu Wewe mwenyewe."71
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِرِضَاكَ مِنْ سَخَطِكَ، وَبِمُعَافَاتِكَ مِنْ عُقوبَتِكَ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْكَ، لَا أُحْصِي ثَنَاءً عَلَيْكَ، أَنْتَ كَمَا أَثْنَيْتَ عَلَى نَفْسِك).
Allahumma inni audhu biridhaka min sakhatika, wa bimuafatika min ukubatika, wa audhu bika minka, laa uhsi thana-an alaika, anta kamaa athnaita alaa nafsik.
20. DUA YA KIKAO KATI YA SIJIDA MBILI
"Ewe Mola wangu Mlezi nisamehe, ewe Mola wangu Mlezi nisamehe."72
(رَبِّ اغْفِرْ لِي، رَبِّ اغْفِرْ لِي).
Rabbi ghfir li, Rabbi ghfir li
"Yaani: Ewe Mola wangu nisamehe, na unihurumie, na uniongoze, na uniunge, na unipe afya, na uniruzuku, na uniinue.73"
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَاجْبُرْنِي، وَعَافِنِي، وَارْزُقْنِي، وَارْفَعْنِي).
Allahumma ghfir li, warhamni, wahdini, wajburni, waafini, warzukni, warfaani
21. DUA YA SIJIDA YA KISOMO
"Umesujudu uso wangu kwa Yule aliyeuumba, na akapasua usikivu wake na uoni wake kwa uwezo wake na nguvu zake. Basi ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mbora wa waumbaji."
(سَجَدَ وَجْهِيَ لِلَّذِي خَلَقَهُ، وَشَقَّ سَمْعَهُ وَبَصَرَهُ بِحَوْلِهِ وَقُوَّتِهِ، فَتَبارَكَ اللَّهُ أَحْسَنُ الخَالِقِين).
Sajada wajhiya lilladhi khalaqahu, wa shaqqa sam'ahu wa baswarahu bihawlihi wa quwwatihi, fa tabaarakallahu ahsanul khaaliqiin.
[Al-Mu'minun: 14]74.
"Ewe Mwenyezi Mungu, niandikie kwayo malipo kwako, na uniondolee kwayo madhambi, na uijaalie iwe akiba kwangu kwako, na uikubali kutoka kwangu kama ulivyoikubali kutoka kwa mja wako Daud."75
(اللَّهُمَّ اكْتُبْ لِي بِهَا عِنْدَكَ أَجْرًا، وَضَعْ عَنِّي بِهَا وِزْرًا، وَاجْعَلْهَا لِي عِنْدَكَ ذُخْرًا، وَتَقَبَّلْهَا مِنِّي كَمَا تَقَبَّلْتَهَا مِنْ عَبْدِكَ دَاوُد).
Allahumma ktub li biha indaka ajran, wa dha' anni biha wizran, waj'alha li indaka dhukhran, wa taqabbalha minni kama taqabbaltaha min abdika Dawud.
22. TASHAHHUD
"Tafsiri yake: Maamkizi yote ni ya Mwenyezi Mungu, na swala na vile vilivyo vizuri. Amani iwe juu yako, ewe Nabii, na rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka zake. Amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Mwenyezi Mungu. Nashuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu, na ninashuhudia kuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake.76"
(التَّحِيَّاتُ لِلَّهِ، وَالصَّلَواتُ، وَالطَّيِّبَاتُ، السَّلَامُ عَلَيْكَ أَيُّهَا النَّبِيُّ وَرَحْمَةُ اللَّهِ وَبَرَكَاتُهُ، السَّلَامُ عَلَيْنَا وَعَلَى عِبَادِ اللَّهِ الصَّالِحِينَ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَأَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسولُه).
Atahiyatu lillahi, waswalawatu, watwayibatu. Asalamu alayka ayuha nabiyu warahmatulahi wabarakatuhu. Asalamu alayna wa ala ibadillahi swalihina. Ashhadu an la ilaha ilallahu wa ashhadu ana Muhammadan abduhu wa rasuluh.
23. KUMTAKIA REHEMA MTUME, REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE, BAADA YA TAHIYATU
"Yaani: Ewe Mwenyezi Mungu, mshushie rehema Muhammad, na jamaa zake Muhammad, kama ulivyomshushia rehema Ibrahim na jamaa za Ibrahim. Hakika Wewe ni Msifiwa, Mtukufu. Ewe Mwenyezi Mungu, mbariki Muhammad na jamaa zake Muhammad, kama ulivyombariki Ibrahim na jamaa zake Ibrahim. Hakika Wewe ni Msifiwa, Mtukufu.77"
(اللَّهُمَّ صَلِّ عَلَى مُحَمَّدٍ، وَعَلَى آلِ مُحَمَّدٍ، كَمَا صَلَّيتَ عَلَى إِبْرَاهِيمَ، وَعَلَى آلِ إِبْرَاهِيمَ، إِنَّكَ حَمِيدٌ مَجِيدٌ، اللَّهُمَّ بَارِكْ عَلَى مُحَمَّدٍ وَعَلَى آلِ مُحَمَّدٍ، كَمَا بَارَكْتَ عَلَى إِبْرَاهِيمَ وَعَلَى آلِ إِبْرَاهِيمَ، إِنَّكَ حَمِيدٌ مَجِيد).
Allahumma salli ala Muhammadin, wa ala aali Muhammadin, kama sallayta ala Ibrahima, wa ala aali Ibrahima, innaka hamidun majidun. Allahumma barik ala Muhammadin wa ala aali Muhammadin, kama barakta ala Ibrahima wa ala aali Ibrahima, innaka hamidun majid.
"Ewe Mwenyezi Mungu, shusha rehema juu ya Muhammad na wake zake na dhuriya wake, kama ulivyoshusha rehema juu ya aali za Ibrahim. Na mbariki Muhammad na wake zake na dhuriya wake, kama ulivyowabariki aali za Ibrahimu. Hakika Wewe ni Msifiwa mno, Mtukufu.”78
(اللَّهُمَّ صَلِّ عَلَى مُحَمَّدٍ وَعَلَى أَزْوَاجِهِ وَذُرِّيَّتِهِ، كَمَا صَلَّيْتَ عَلَى آلِ إِبْرَاهِيمَ، وَبَارِكْ عَلَى مُحَمَّدٍ وَعَلَى أَزْواجِهِ وَذُرِّيَّتِهِ، كَمَا بَارَكْتَ عَلَى آلِ إِبْرَاهِيمَ، إِنَّكَ حَمِيدٌ مَجِيد).
Allahumma swalli ala Muhammadin wa ala azwajihi wa dhuriyyatihi, kama swallaita ala aali Ibrahima. Wa baarik ala Muhammadin wa ala azwajihi wa dhuriyyatihi, kama baarakta ala aali Ibrahima, innaka hamiidun majiid.
24. DUA YA BAADA YA TASHAHHUD YA MWISHO KABLA YA KUTOA SALAMU
"Yaani: Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninajilinda kwako kutokana na adhabu ya kaburi, na adhabu za Jahanamu, na fitina za uhai na za kifo, na kutokana na fitina za Masihi Dajali."79
(اللَّهُــمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابِ القَبْرِ، وَمِنْ عَذَابِ جَهَنَّمَ، وَمِنْ فِتْنَةِ المَحْيَا وَالمَمَاتِ، وَمِنْ شَرِّ فِتْنَةِ المَسِيحِ الدَّجَّال).
Allahumma inni audhu bika min adhabil qabri, wa min adhabi jahannama, wa min fitnatil mahya wal mamati, wa min sharri fitnatil masihid dajjal.
"Yaani: Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninajilinda kwako kutokana na adhabu ya kaburi, na ninajilinda kwako kutokana na fitina za Masihi Dajali, na ninajilinda kwako kutokana na fitina za uhai na za kifo. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninajilinda kwako kutokana na madhambi, na madeni."80
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابِ القَبْرِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ فِتْنَةِ المَسِيحِ الدَّجَّالِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ فِتْنَةِ المَحْيَا وَالمَمَاتِ، اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ المَأْثَمِ وَالمَغْرَم).
Allahumma inni audhu bika min adhabil qabri, wa audhu bika min fitnatil masihid-dajjali, wa audhu bika min fitnatil mahya wal mamati. Allahumma inni audhu bika minal mathami wal maghram.
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu dhuluma nyingi, na hakuna anayesamehe madhambi isipokuwa Wewe, basi nisamehe msamaha utokao kwako na unirehemu, hakika Wewe ni Msamehevu, Mwingi wa kurehemu."81
(اللَّهُمَّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي ظُلْمًا كَثِيرًا، وَلَا يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا أَنْتَ، فَاغْفِرْ لِي مَغْفِرَةً مِنْ عِنْدِكَ وَارْحَمْنِي، إِنَّكَ أَنْتَ الغَفُورُ الرَّحِيم).
Allahumma inni dhalamtu nafsi dhulman kathiran, wala yaghfiru adhunuba illa anta, faghfir li maghfiratan min indaka warhamni, innaka anta al ghafuru ar-rahim.
"Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe niliyoyatanguliza, na niliyoyachelewesha, na niliyoyaficha, na niliyoyaweka hadharani, na niliyofanya ubadhirifu, na yale unayoyajua zaidi kuliko mimi. Wewe ndiwe mwenye kutanguliza, na Wewe ndiwe mwenye kuchelewesha, hapana mungu ila Wewe."82
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي مَا قَدَّمْتُ، وَمَا أَخَّرْتُ، وَمَا أَسْرَرْتُ، وَمَا أَعْلَنْتُ، وَمَا أَسْرَفْتُ، وَمَا أَنْتَ أَعْلَمُ بِهِ مِنِّي، أَنْتَ المُقَدِّمُ، وَأَنْتَ المُؤَخِّرُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْت).
Allahumma ighfir lii maa kaddamtu, wa maa akhartu, wa maa asrartu, wa maa aalantu, wa maa asraftu, wa maa anta aalamu bihi minnii, anta al-mukaddimu, wa anta al-muakhiru laa ilaha illaa anta.
"Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie katika kukutaja, na kukushukuru, na kukufanyia ibada kwa uzuri."83
(اللَّهُمَّ أَعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ، وَشُكْرِكَ، وَحُسْنِ عِبادَتِك).
Allahumma a'inni ala dhikrika, wa shukrika, wa husni ibadatik.
“Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na ubahili, na ninajikinga kwako kutokana na woga, na ninajikinga kwako kutorudi kwenye umri wenye udhalili, na ninajikinga kwako kutokana na fitina za dunia na adhabu za kaburi.”84
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ البُخْلِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنَ الجُبْنِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ أَنْ أُرَدَّ إِلَى أَرْذَلِ العُمُرِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ فِتْنَةِ الدُّنْيَا وَعَذَابِ القَبْر).
Allahumma inni audhu bika minal bukhli, wa audhu bika minal jubni, wa audhu bika min an uradda ila ardhalil umuri, wa audhu bika min fitnatid dunya wa adhabil kabr.
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba Pepo, na ninajikinga kwako kutokana na Moto"85.
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ الجَنَّةَ وَأَعُوذُ بِكَ مِنَ النَّار).
Allahumma inni as'aluka al-jannah, wa a'udhu bika minan-nar.
"Ewe Mwenyezi Mungu, kwa elimu yako ya mambo yaliyojificha, na kwa uwezo wako juu ya viumbe, nipe uhai maadamu unajua kuwa uhai ni heri kwangu, na unifishe maadamu unajua kuwa kifo ni heri kwangu. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba unifanye kukuhofu kwa wazi na kwa siri, na ninakuomba neno la haki katika hali ya kuridhia na hasira, na ninakuomba kuwa na msimamo sahihi kwenye hali ya utajiri na umasikini, na ninakuomba neema zisizomalizika, na ninakuomba kitulizo cha jicho kisichokatika, na ninakuomba kuridhia baada ya kupita hukumu, na ninakuomba maisha ya utulivu baada ya kifo, na ninakuomba ladha ya kutazama uso wako, na shauku ya kukutana na Wewe, bila ya madhara yenye kudhuru, wala fitina yenye kupoteza. Ewe Mwenyezi Mungu, tupambe kwa pambo la imani, na utujaalie kuwa viongozi walioongoka."86
(اللَّهُمَّ بِعِلْمِكَ الغَيْبَ وَقُدْرَتِكَ عَلَى الخَلقِ أَحْيِنِي مَا عَلِمْتَ الحَيَاةَ خَيْرًا لِي، وَتَوَفَّنِي إِذَا عَلِمْتَ الْوَفَاةَ خَيْرًا لِي، اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَشْيَتَكَ فِي الغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ، وَأَسْأَلُكَ كَلِمَةَ الحَقِّ فِي الرِّضَا وَالغَضَبِ، وَأَسْأَلُكَ القَصْدَ فِي الغِنَى وَالفَقْرِ، وَأَسْأَلُكَ نَعِيمًا لَا يَنْفَدُ، وَأَسْأَلُكَ قُرَّةَ عَيْنٍ لَا تَنْقَطِعُ، وَأَسْأَلُكَ الرِّضَا بَعْدَ القَضَاءِ، وَأَسْـأَلُكَ بَرْدَ العَيْشِ بَعْدَ المَوْتِ، وَأَسْأَلُكَ لَذَّةَ النَّظَرِ إِلَى وَجْهِكَ، وَالشَّوْقَ إِلَى لِقَائِكَ فِي غَيرِ ضَرَّاءَ مُضِرَّةٍ، وَلَا فِتْنَةٍ مُضِلَّةٍ، اللَّهُمَّ زَيِّنَا بِزِينَةِ الإِيمَانِ، وَاجْعَلْنَا هُدَاةً مُهْتَدِين).
Allahumma bi ilmika al-ghayba wa kudratika ala al-khalki ahyini ma alimta al-hayata khayran li, wa tawaffani idha alimta al-wafata khayran li, Allahumma inni as-aluka khashyataka fi al-ghaybi wash-shahadati, wa as-aluka kalimata al-hakki fi ar-ridha wal-ghadhabi, wa as-aluka al-kasda fi al-ghina wal-fakri, wa as-aluka naiman la yanfadu, wa as-aluka kurrata aynin la tankatiu, wa as-aluka ar-ridha bada al-kadhai, wa as-aluka barda al-ayshi bada al-mawti, wa as-aluka ladhdhata an-nadhari ila wajhika, wash-shawka ila likaika fi ghayri dharraa mudhirratin, wa la fitnatin mudhillatin, Allahumma zayyina bi zinati al-imani, waj-alna hudatan muhtadin.
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba ewe Mwenyezi Mungu kwa kuwa Wewe ni Mmoja, wa Pekee, Mkusudiwa, ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa na wala hana yeyote wa kufananishwa naye, kwamba unisamehe madhambi yangu. Hakika Wewe ni Msamehevu, Mrehemevu."87.
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ يَا أَللَّهُ بِأَنَّكَ الوَاحِدُ الأَحَدُ الصَّمَدُ الَّذِي لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ، وَلَمْ يَكُنْ لَهُ كُفُوًا أَحَدٌ، أَنْ تَغْفِرَ لِي ذُنُوبِي إِنَّكَ أَنْتَ الغَفُورُ الرَّحِّيم).
Allahumma inni as'aluka ya Allahu bi'annaka al-Wahidu al-Ahadu as-Samadu alladhi lam yalid wa lam yuulad, wa lam yakun lahu kufuwan ahad, an taghfira lii dhunuubii innaka anta al-Ghafuuru ar-Rahiim
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba kwa kuwa sifa njema zote ni zako, hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe uliye mpweke usiye na mshirika, Mwenye kuneemesha mno. Ewe Muumbaji mwanzilishi wa mbingu na ardhi. Ewe mwenye utukufu na ukarimu. Ewe uliye Hai. Ewe Msimamia yote milele, hakika mimi ninakuomba Pepo na ninajikinga kwako kutokana na Moto."88
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ بِأَنَّ لَكَ الحَمْدَ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ وَحْدَكَ لَا شَرِيكَ لَكَ، المَنَّانُ، يَا بَدِيعَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ يَا ذَا الجَلَالِ وَالإِكْرَامِ، يَا حَيُّ يَا قَيُّومُ إِنِّي أَسْأَلُكَ الجَنَّةَ وَأَعُوذُ بِكَ مِنَ النَّار).
Allahumma inni as-aluka bi-anna lakal hamda laa ilaha illaa anta wahdaka laa shariika laka, Al-Mannaanu, yaa Badii-as samawaati wal-ardhi yaa Dhaal jalaali wal-ikraami, yaa Hayyu yaa Qayyuumu inni as-alukal jannata wa a-uudhu bika minan-naar
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba kwa kuwa ninashuhudia kuwa Wewe ni Mwenyezi Mungu, hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe, uliye wa Pekee, Mkusudiwa, ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa na wala hakuna yeyote wa kufananishwa naye."89
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ بِأَنَّي أَشْهَدُ أَنَّكَ أَنْتَ اللَّهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ الأَحَدُ الصَّمَدُ الَّذِي لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ وَلَمْ يَكُنْ لَهُ كُفُوًا أَحَد).
Allahumma inni as-aluka, bi anni ash-hadu annaka antal-lahu, laa ilaha illa anta, al-ahadus-samadu, alladhi lam yalid, wa lam yuulad, wa lam yakul-lahu kufuwan ahad.
25. DHIKIRI BAADA YA SALAMU YA KUMALIZA SWALA
"Ninamuomba msamaha Mwenyezi Mungu."
(أَسْتَغْفِرُ اللَّه).
Astaghfirullah
Mara tatu "Ewe Mwenyezi Mungu, hakika wewe ndiye amani, na amani hutoka kwako. Umetukuka ewe Mwenye utukufu na ukarimu."90.
(اللَّهُمَّ أَنْتَ السَّلَامُ، وَمِنْكَ السَّلَامُ، تَبَارَكْتَ يَا ذَا الجَلَالِ وَالإِكْرَام).
Allahumma antas salamu, wa minkas salamu, tabarakta ya dhal jalali wal ikram.
"Tafsiri yake: Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika, ufalme ni wake na sifa njema ni zake, naye juu ya kila kitu ni muweza."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaaha illallaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu wa huwa alaa kulli shayin kadiir
Mara tatu "Yaani: 'Ewe Mwenyezi Mungu, hakuna wa kuzuia uliyoyatoa, wala wa kuyatoa uliyoyazuia, wala hawezi kunufaisha mwenye utukufu (yeyote) kuliko wewe ewe Mtukufu.'"91
(اللَّهُمَّ لَا مَانِعَ لِمَا أَعْطَيْتَ، وَلَا مُعْطِيَ لِمَا مَنَعْتَ، وَلَا يَنْفَعُ ذَا الجَدِّ مِنْكَ الجَد).
Allahumma la mania lima atwaita, wala muutwiya lima manata, wala yanfau dhal jaddi minkal jad.
"Tafsiri: 'Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema zote ni zake, naye ni Muweza mno wa kila kitu. Hapana uwezo wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na wala hatumuabudu yeyote ila Yeye. Yeye ndiye Mwenye neema, na fadhila zote ni zake, na Yeye ndiye Mwenye sifa nzuri. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, hali ya kuwa tunamtakasia dini (matendo) hata kama makafiri watachukia.'"92
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ، وَلَهُ الحَمدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، لَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّهِ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَلَا نَعْبُدُ إِلَّا إِيَّاهُ لَهُ النِّعْمَةُ وَلَهُ الفَضْلُ وَلَهُ الثَّنَاءُ الحَسَن، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ وَلَوْ كَرِهَ الكَافِرُون).
La ilaha illallah wahdahu la sharika lahu, lahul mulku, walahul hamdu, wa huwa ala kulli shayin qadir, la hawla wala quwwata illa billah, la ilaha illallah, wala naabudu illa iyyahu lahun niimatu walahul fadhlu walahuth thanaul hasan, la ilaha illallah mukhlisina lahud dina walaw karihal kafirun.
"Tafsiri: Ametakasika Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu Mkubwa."
(سُبْحَانَ اللَّهِ، وَالحَمْدُ لِلَّهِ، وَاللَّهُ أَكْبَر).
Subhanallahi, Walhamdulillahi, Wallahu Akbar
(mara thelathini na tatu), "Tafsiri: 'Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema zote ni zake, naye juu ya kila kitu ni muweza.'"93
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaha illallahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku walahul hamdu wahuwa alaa kulli shayin kadiir
﴿قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ1 ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ2 لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ3 وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ4﴾
"1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa Pekee.
2. Mwenyezi Mungu ndiye Mkusudiwa.
3. Hakuzaa wala hakuzaliwa.
4. Wala hana anayelingana naye hata mmoja."
[Al-Ikhlaas: 1-4].
﴿قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ1 مِن شَرِّ مَا خَلَقَ2 وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ3 وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ4 وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ5﴾
"1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko.
2. Kutokana na shari ya alivyoviumba.
3. Na kutokana na shari ya giza la usiku liingiapo.
4. Na kutokana na shari ya wanaopuliza mafundoni.
5. Na kutokana na uovu wa mwenye husuda anapohusudu."
[Al-Falaq: 1-5].
﴿قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ1 مَلِكِ ٱلنَّاسِ2 إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ3 مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ4 ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ5 مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ6﴾
"1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu.
2. Mfalme wa watu.
3. Mungu wa watu.
4. Kutokana na shari ya Shetani mtia wasiwasi, ajifichaye mno (Al-Khannaas).
5. Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu.
6. Kutokana na majini na watu."
[An-Nas: 1-6].
Baada ya kila swala94.
﴿ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُۚ لَا تَأۡخُذُهُۥ سِنَةٞ وَلَا نَوۡمٞۚ لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ مَن ذَا ٱلَّذِي يَشۡفَعُ عِندَهُۥٓ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦۚ يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيۡءٖ مِّنۡ عِلۡمِهِۦٓ إِلَّا بِمَا شَآءَۚ وَسِعَ كُرۡسِيُّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۖ وَلَا يَـُٔودُهُۥ حِفۡظُهُمَاۚ وَهُوَ ٱلۡعَلِيُّ ٱلۡعَظِيمُ255﴾
"Mwenyezi Mungu - hakuna mungu isipokuwa Yeye, aliye hai, Msimamizi wa mambo yote milele. Hashikwi na kusinzia wala kulala. Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo duniani. Ni nani huyo awezaye kufanya uombezi mbele yake isipokuwa kwa idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao, na yaliyo nyuma yao, wala wao hawajui vyema chochote katika elimu yake isipokuwa kwa kile akitakacho. Kursi (mahali inapokanyaga miguu) yake imeenea mbingu na dunia, na wala halemewi katika kuvilinda vyote viwili. Na Yeye ndiye aliye juu zaidi, Mkuu."
[Al Baqara: 255] Mwisho wa kila swala95.
"Tafsiri yake: Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika, ufalme ni wake na sifa njema ni zake, anahuisha na kufisha, naye juu ya kila kitu ni muweza."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ يُحْيِي وَيُمِيتُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
La ilaha illallah wahdahu la sharika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu yuhyi wa yumitu wa huwa ala kulli shayin kadir
Mara kumi baada ya swala ya magharibi na Alfajiri96.
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba elimu yenye manufaa, na riziki nzuri, na matendo yenye kukubalika."
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ عِلْمًا نافِعًا، وَرِزْقًا طَيِّبًا، وَعَمَلًا مُتَقَبَّلًا).
Allahumma inni as'aluka ilman nafi'an, wa rizkan tayyiban, wa amalan mutakabbalan.
Baada ya salamu ya kumaliza swala ya Alfajiri97.
26. DUA YA SWALA YA KUOMBA UCHAGUZI (ISTIKHARA)
Imepokelewa kutoka kwa Jabiri bin Abdillah radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao (yeye na baba yake) kwamba amesema: Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akitufundisha kutaka uchaguzi (kwa Mwenyezi Mungu) katika mambo yetu yote kama anavyotufundisha sura katika Qur'ani, akisema: "Anapokusudia mmoja wenu kufanya jambo, basi aswali rakaa mbili zisizokuwa za faradhi, kisha aseme: "Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba uchaguzi kupitia elimu yako, na ninakuomba uwezo kupitia uwezo wako, na ninakuomba unipe kutoka katika fadhila zako tukufu; kwani Wewe unaweza na mimi siwezi, na unajua na mimi sijui, na Wewe ni Mjuzi wa yaliyofichikana. Ewe Mwenyezi Mungu, ikiwa unajua kuwa jambo hili - anataja haja yake - ni kheri kwangu katika dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu - au alisema: haraka ya jambo langu na kuchelewa kwake - basi liwezeshe kwangu na unifanyie wepesi kwangu, kisha unibariki mimi ndani yake. Na ikiwa unajua kuwa jambo hili ni shari kwangu katika dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu - au alisema: haraka ya jambo langu na kuchelewa kwake - basi liepushe nami na uniepushe nalo, na unikadirie kheri mahala popote itakapokuwa, kisha niridhishe nayo.""98.
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْتَخِيرُكَ بِعِلْمِكَ، وَأَسْتَقْدِرُكَ بِقُدْرَتِكَ، وَأَسْأَلُكَ مِنْ فَضْلِكَ العَظِيمِ؛ فَإِنَّكَ تَقْدِرُ وَلَا أَقْدِرُ، وَتَعْلَمُ وَلَا أَعْلَمُ، وَأَنْتَ عَلَّامُ الغُيُوبِ، اللَّهُمَّ إِنْ كُنْتَ تَعْلَمُ أَنَّ هَذَا الأمْرَ - وَيُسَمِّي حَاجَتَهُ - خَيْرٌ لِي فِي دِينِي وَمَعَاشِي وَعَاقِبَةِ أَمْرِي – أَوْ قَالَ: عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ - فَاقْدُرْهُ لِي وَيَسِّرْهُ لِي ثمَّ بَارِكْ لِي فِيهِ، وَإِنْ كُنْتَ تَعْلَمُ أَنَّ هَذَا الْأَمْرَ شَرٌّ لِي فِي دِينِي وَمَعَاشِي وَعَاقِبَةِ أَمْرِي – أَوْ قَالَ: عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ – فَاصْرِفْهُ عَنِّي وَاصْرِفْنِي عَنْهُ وَاقْدُرْ لِيَ الْخَيْرَ حَيْثُ كَانَ، ثُمَّ أَرْضِنِي بِه).
Allahumma inni astakhiiruka bi ilmika, wa astakdiruka bi kudratika, wa as-aluka min fadhlikal adhiim; fa innaka takdiru wa laa akdiru, wa taalamu wa laa aalamu, wa anta allaamul ghuyuub. Allahumma in kunta taalamu anna haadhal amra - wa yusammi haajatahu - khayrun lii fii diinii wa ma-aashii wa aakibati amrii - aw kaala: aajilihi wa aajilihi - fakdurhu lii wa yassirhu lii thumma baarik lii fiihi. Wa in kunta taalamu anna haadhal amra sharrun lii fii diinii wa ma-aashii wa aakibati amrii - aw kaala: aajilihi wa aajilihi - fasrifhu annii wasrifnii anhu wakdur liyal khayra haythu kaana, thumma ardhinii bih.
Hakuwahi kujuta aliyemtaka uchaguzi Muumba, na akawataka ushauri viumbe katika waumini katika jambo lake, kwani amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
﴿...وَشَاوِرۡهُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِۖ فَإِذَا عَزَمۡتَ فَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِ...﴾.
"...na shauriana nao katika mambo. Na ukishakata shauri, basi mtegemee Mwenyezi Mungu..."99
27. NYIRADI ZA ASUBUHI NA JIONI
"Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu peke yake, na rehema na amani ziwe juu ya yule ambaye hakuna nabii baada yake100."
Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa
﴿ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُۚ لَا تَأۡخُذُهُۥ سِنَةٞ وَلَا نَوۡمٞۚ لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ مَن ذَا ٱلَّذِي يَشۡفَعُ عِندَهُۥٓ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦۚ يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيۡءٖ مِّنۡ عِلۡمِهِۦٓ إِلَّا بِمَا شَآءَۚ وَسِعَ كُرۡسِيُّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۖ وَلَا يَـُٔودُهُۥ حِفۡظُهُمَاۚ وَهُوَ ٱلۡعَلِيُّ ٱلۡعَظِيمُ255﴾
"Mwenyezi Mungu - hakuna mungu isipokuwa Yeye, aliye hai, Msimamizi wa mambo yote milele. Hashikwi na kusinzia wala kulala. Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo duniani. Ni nani huyo awezaye kufanya uombezi mbele yake isipokuwa kwa idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao, na yaliyo nyuma yao, wala wao hawajui vyema chochote katika elimu yake isipokuwa kwa kile akitakacho. Kursi (mahali inapokanyaga miguu) yake imeenea mbingu na dunia, na wala halemewi katika kuvilinda vyote viwili. Na Yeye ndiye aliye juu zaidi, Mkuu."
[Al Baqara: 255]101.
﴿قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ1 ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ2 لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ3 وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ4﴾
"1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa Pekee.
2. Mwenyezi Mungu ndiye Mkusudiwa.
3. Hakuzaa wala hakuzaliwa.
4. Wala hana anayelingana naye hata mmoja."
"[Al-Ikhlaas: 1-4]."
﴿قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ1 مِن شَرِّ مَا خَلَقَ2 وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ3 وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ4 وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ5﴾
"1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko.
2. Kutokana na shari ya alivyoviumba.
3. Na kutokana na shari ya giza la usiku liingiapo.
4. Na kutokana na shari ya wanaopuliza mafundoni.
5. Na kutokana na shari ya mwenye husuda anapohusudu."
[Al-Falaq: 1-5].
﴿قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ1 مَلِكِ ٱلنَّاسِ2 إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ3 مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ4 ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ5 مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ6﴾
"1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu.
2. Mfalme wa watu.
3. Mungu wa watu.
4. Kutokana na shari ya Shetani mtia wasiwasi, ajifichaye mno (Al-Khannaas).
5. Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu.
6. Kutokana na majini na watu."
[An-Nas: 1-6] (Mara tatu)102.
"Tumeamka na umekuwa ufalme ni wa Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni zake Mwenyezi Mungu. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema zote ni zake, naye ni Muweza mno wa kila kitu. Mola wangu Mlezi, ninakuomba heri ya yaliyomo katika siku hii na heri za baada yake, na ninajikinga kwako kutokana na shari ya yaliyomo katika siku hii na shari za baada yake. Mola wangu Mlezi, ninajikinga kwako kutokana na uvivu na ubaya wa uzee. Mola wangu Mlezi, ninajikinga kwako kutokana na adhabu katika moto na adhabu katika kaburi."103
(أَصْبَحْنَا وَأَصْبَحَ المُلْكُ لِلَّهِ، وَالحَمْدُ لِلَّهِ، لَا إِلَهَ إلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، رَبِّ أَسْأَلُكَ خَيْرَ مَا فِي هَذَا اليَوْمِ وَخَيرَ مَا بَعْدَهُ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِي هَذَا اليَوْمِ وَشَرِّ مَا بَعْدَهُ، رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنَ الكَسَلِ وَسُوءِ الكِبَرِ، رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابٍ فِي النَّارِ وَعَذَابٍ فِي القَبْر).
Asbahna wa asbahal mulku lillahi, wal hamdu lillahi, la ilaha illallahu wahdahu la sharika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu wa huwa ala kulli shayin kadirun. Rabbi asaluka khaira ma fi hadhal yaumi wa khaira ma baadahu, wa audhu bika min sharri ma fi hadhal yaumi wa sharri ma baadahu. Rabbi audhu bika minal kasali wa suil kibari. Rabbi audhu bika min adhabin fin nari wa adhabin fil kabri.
Na anapoingia jioni, atasema: "Tumeingia jioni na ufalme umethibiti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni zake Mwenyezi Mungu, hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika, Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, naye juu ya kila kitu ni Muweza. Mola wangu Mlezi, ninakuomba heri ya yaliyomo katika usiku huu, na heri za baada yake, na ninajikinga kwako kutokana na shari ya yaliyomo katika usiku huu, na shari za baada yake. Mola wangu Mlezi, ninajikinga kwako kutokana na uvivu na ubaya wa uzee. Mola wangu Mlezi, ninajikinga kwako kutokana na adhabu katika moto, na adhabu katika kaburi104."
(أَمْسَيْنَا وَأَمْسَى الْمُلْكُ لِلَّهِ، وَالحَمْدُ لِلَّهِ، لَا إِلَهَ إلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، رَبِّ أَسْأَلُكَ خَيْرَ مَا فِي هَذِهِ اللَّيْلَةِ، وَخَيْرَ مَا بَعْدَهَا، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِي هَذِهِ اللَّيْلَةِ، وَشَرِّ مَا بَعْدَهَا، رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنَ الكَسَلِ وَسُوءِ الكِبَرِ، رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابٍ فِي النَّارِ وَعَذَابٍ فِي القَبْرِ).
Amsaynaa wa amsal mulku lillahi, wal hamdu lillahi, laa ilaha illallahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu wa huwa alaa kulli shay-in qadiir. Rabbi asaluka khayra maa fii haadhihil laylati, wa khayra maa baadahaa, wa auudhu bika min sharri maa fii haadhihil laylati, wa sharri maa baadahaa. Rabbi auudhu bika minal kasali wa suu-il kibari. Rabbi auudhu bika min adhaabin fin naari wa adhaabin fil qabri.
"Ewe Mwenyezi Mungu kwako tumeamka, na kwako tumeshinda, na kwako tunakuwa hai, na kwako tunakufa na kwako tutafufuliwa105."
(اللَّهُمَّ بِكَ أَصْبَحْنَا، وَبِكَ أَمْسَيْنَا، وَبِكَ نَحْيَا، وَبِكَ نَمُوتُ وَإِلَيْكَ النُّشُور).
Allahumma bika asbahna, wa bika amsayna, wa bika nahya, wa bika namutu wa ilaykan nushur.
Na anapoingia jioni, basi atasema: "Ewe Mwenyezi Mungu kwako tumeshinda, na kwako tumeamka, na kwako tunakuwa hai, na kwako tutakufa, na marejeo ni kwako."106
(اللَّهُمَّ بِكَ أَمْسَيْنَا، وَبِكَ أَصْبَحْنَا، وَبِكَ نَحْيَا، وَبِكَ نَمُوتُ، وَإِلَيْكَ الْمَصِير).
Allahumma bika amsayna, wabika asbahna, wabika nahya, wabika namutu, wa ilaykal masir
"Ewe Mwenyezi Mungu Wewe ndiye Mola Mlezi hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, umeniumba na mimi ni mja wako na mimi nipo juu ya ahadi yako na maonyo yako kwa kiasi niwezavyo, ninataka hifadhi kwako kutokana na shari niliyoifanya, ninakiri107 kwa neema zako zilizo juu yangu, na ninakiri kwa madhambi yangu, basi nifutie mimi dhambi, kwani hakuna afutaye madhambi isipokuwa Wewe."108
(اللَّهُمَّ أَنْتَ رَبِّي لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، خَلَقْتَنِي وَأَنَا عَبْدُكَ، وَأَنَا عَلَى عَهْدِكَ وَوَعْدِكَ مَا اسْتَطَعْتُ، أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا صَنَعْتُ، أَبُوءُ لَكَ بِنِعْمَتِكَ عَلَيَّ، وَأَبُوءُ بِذَنْبِي فَاغْفِرْ لِي فَإِنَّهُ لَا يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا أَنْت).
Allahumma anta rabbi la ilaha illa anta, khalaktani wa ana abduka, wa ana ala ahdika wa waadika mastataatu, audhu bika min sharri ma sanaatu, abuu laka biniimatika alayya, wa abuu bidhanbi faghfir li fainnahu la yaghfiru dhunuba illa anta.
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nimepambazukiwa na asubuhi, ninakufanya Wewe kuwa shahidi, na ninawashuhudisha Malaika wabebao Arshi yako, na Malaika wako, na viumbe wako wote, kuwa wewe ni Mwenyezi Mungu, hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe peke yako, huna mshirika, na kuwa Muhammad ni mja wako na Mtume wako."
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَصْبَحْتُ أُشْهِدُكَ، وَأُشْهِدُ حَمَلَةَ عَرْشِكَ، وَمَلَائِكَتِكَ، وَجَمِيعَ خَلْقِكَ، أَنَّكَ أَنْتَ اللَّهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ وَحْدَكَ لَا شَرِيكَ لَكَ، وَأَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُكَ وَرَسُولُك).
Allahumma inni asbahtu ush-hiduka, wa ush-hidu hamalata arshika, wa malaikataka, wa jamia khalkika, annaka anta Allahu la ilaha illa anta wahdaka la sharika laka, wa anna Muhammadan abduka wa rasuluk.
Mara nne109.
Na anapoingia jioni, atasema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nimeingiliwa na jioni, ninakufanya Wewe kuwa shahidi na ninawashuhudisha Malaika wabebao Arshi yako na Malaika wako na viumbe wako wote kuwa wewe ni Mwenyezi Mungu, hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe peke yako huna mshirika, na kuwa Muhammad ni mja wako na Mtume wako."
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَمْسَيْتُ أُشْهِدُكَ، وَأُشْهِدُ حَمَلَةَ عَرْشِكَ، وَمَلَائِكَتِكَ، وَجَمِيعَ خَلْقِكَ، أَنَّكَ أَنْتَ اللَّهُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ وَحْدَكَ لَا شَرِيكَ لَكَ، وَأَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُكَ وَرَسُولُك).
Allahumma inni amsaitu ush-hiduka, wa ush-hidu hamalata arshika, wa malaikataka, wa jamia khalkika, annaka anta Allahu la ilaha illa anta wahdaka la sharika laka, wa anna Muhammadan abduka wa rasuluk.
Mara nne110.
"Yaani: Ewe Mwenyezi Mungu haijapambazuka kwangu au kwa yeyote katika viumbe wako neema yoyote, isipokuwa inatoka kwako peke yako hauna mshirika, basi sifa njema na shukurani ni zako."111
(اللَّهُمَّ مَا أَصْبَحَ بِي مِنْ نِعْمَةٍ أَوْ بِأَحَدٍ مِنْ خَلْقِكَ فَمِنْكَ وَحْدَكَ لَا شَرِيكَ لَكَ، فَلَكَ الحَمْدُ وَلَكَ الشُّكْر).
Allahumma maa asbaha bii min niimatin au bi ahadin min khalkika faminka wahdaka laa shariika laka, falakal hamdu walakash shukru.
Na ifikapo jioni atasema: "Ewe Mwenyezi Mungu neema yoyote haijaingia jioni kwangu au kwa yeyote katika viumbe wako, isipokuwa inatoka kwako peke yako hauna mshirika, basi sifa njema na shukurani ni zako."112
(اللَّهُمَّ مَا أَمْسَى بِي مِنْ نِعْمَةٍ أَوْ بِأَحَدٍ مِنْ خَلْقِكَ فَمِنْكَ وَحْدَكَ لَا شَرِيكَ لَكَ، فَلَكَ الحَمْدُ وَلَكَ الشُّكْر).
Allahumma maa amsaa bii min niimatin au bi ahadin min khalkika faminka wahdaka laa shariika laka, falakal hamdu walakash shukr
"Ewe Mwenyezi Mungu nipe salama katika mwili wangu. Ewe Mwenyezi Mungu nipe salama katika masikio yangu. Ewe Mwenyezi Mungu nipe salama katika macho yangu. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na kufuru, na umasikini, na ninajikinga kwako kutokana na adhabu ya kaburi. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Wewe."
(اللَّهُمَّ عَافِنِي فِي بَدَنِي، اللَّهُمَّ عَافِنِي فِي سَمْعِي، اللَّهُمَّ عَافِنِي فِي بَصَرِي، لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ الكُفْرِ، وَالفَقْرِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابِ القَبْرِ، لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْت).
Allahuma aafini fii badani. Allahuma aafini fii sam-i. Allahuma aafini fii basari, laa ilaha illa anta. Allahuma inni audhu bika minal kufri, wal fakri, wa audhu bika min adhabil kabri, laa ilaha illa anta.
Mara tatu113.
"Mwenyezi Mungu ananitosha. Hakuna mungu isipokuwa Yeye tu. Mimi ninamtegemea Yeye, na Yeye ndiye Mola Mlezi wa Kiti Kikuu cha Enzi."
(حَسْبِيَ اللَّهُ لَا إِلَهَ إِلَّا هُوَ عَلَيهِ تَوَكَّلتُ وَهُوَ رَبُّ العَرْشِ العَظِيم).
Hasbiyallahu laa ilaha illa huwa, alaihi tawakkaltu, wa huwa Rabbul arshil adhiim.
Mara saba114.
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba msamaha na afya duniani na akhera. Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba msamaha na afya: katika dini yangu na dunia yangu na familia yangu, na mali yangu. Ewe Mwenyezi Mungu sitiri uchi wangu (madhaifu yangu), na unipe amani katika hofu yangu. Ewe Mwenyezi Mungu unihifadhi mbele yangu, na nyuma yangu, na kuliani kwangu, na kushotoni kwangu, na juu yangu, na ninajilinda katika utukufu wako nisije kuvamiwa toka chini yangu."115
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ العَفْوَ وَالعَافِيَةَ فِي الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ، اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ العَفْوَ وَالعَافِيَةَ: فِي دِينِي وَدُنْيَايَ وَأَهْلِي، وَمَالِي، اللَّهُمَّ اسْتُرْ عَوْرَاتِي، وَآمِنْ رَوْعَاتِي، اللَّهُمَّ احْفَظْنِي مِنْ بَينِ يَدَيَّ، وَمِنْ خَلْفِي، وَعَنْ يَمِينِي، وَعَنْ شِمَالِي، وَمِنْ فَوْقِي، وَأَعُوذُ بِعَظَمَتِكَ أَنْ أُغْتَالَ مِنْ تَحْتِي).
Allahumma inni as'alukal-afwa wal-afiyata fid-dunya wal-akhirati. Allahumma inni as'alukal-afwa wal-afiyata: fi dini wa dunyaya wa ahli, wa mali. Allahummas-tur aurati, wa amin rau'ati. Allahummah-fadhni min baini yadayya, wa min khalfi, wa an yamini, wa an shimali, wa min fauqi, wa a'udhu bi adhamatika an ughtala min tahti
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa ghaibu na yenye kushuhudiwa, Muumba wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa kila kitu na Mmiliki wake, nashuhudia ya kwamba hapana mungu ila Wewe. Najikinga Kwako kutokana na shari ya nafsi yangu, na kutokana na shari ya Shetani na mitego yake, na nisifanye maovu juu ya nafsi yangu au kuyaleta juu ya Muislamu."116"
(اللَّهُمَّ عَالِمَ الغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ فَاطِرَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ، رَبَّ كُلِّ شَيْءٍ وَمَلِيكَهُ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ نَفْسِي، وَمِنْ شَرِّ الشَّيْطانِ وَشَرَكِهِ، وَأَنْ أَقْتَرِفَ عَلَى نَفْسِي سُوءًا، أَوْ أَجُرَّهُ إِلَى مُسْلِم).
Allahumma aalimal ghaibi wash-shahaadati faatiras-samawaati wal-ardhi, rabba kulli shai-in wa maliikahu, ash-hadu an laa ilaaha illaa anta, audhu bika min sharri nafsii, wa min sharrish-shaitaani wa sharakihi, wa an aqtarifa alaa nafsii suu-an, au ajurrahu ilaa muslim.
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu ambaye hakuna chochote kinachoweza kudhuru pamoja na jina lake, ardhini wala mbinguni, naye ni Mwenye kusikia, ajuaye zaidi."
(بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ العَلِيم).
Bismillahi lladhii laa yadhurru ma'asmihi shai'un fil ardhi walaa fis samaai wa huwas samii'ul aliim
Mara tatu117.
"Yaani: Nimeridhia Mwenyezi Mungu kuwa Mola Mlezi, na Uislamu kuwa dini, na Muhammadi, rehema na amani ziwe juu yake, kuwa Nabii."
(رَضِيتُ بِاللَّهِ رَبًَّا، وَبِالإِسْلَامِ دِينًا، وَبِمُحَمَّدٍ ﷺ نَبِيًّا).
Radhiitu billahi rabban, wabil islami diinan, wabi muhammadin swalallahu aleyhi wa sallam nabiyyan.
Mara tatu118.
"Ewe uliye Hai. Ewe Msimamiaji wa kila kitu, kwa rehema zako ninaomba msaada, unitengenezee mambo yangu yote, wala usiniache nijisimamie mwenyewe kwa kiasi cha kupepesa jicho.”119
(يَا حَيُّ يَا قَيُّومُ بِرَحْمَتِكَ أَسْتَغيثُ أَصْلِحْ لِي شَأْنِيَ كُلَّهُ وَلَا تَكِلْنِي إِلَى نَفْسِي طَرْفَةَ عَيْن).
Yaa Hayyu yaa Kayyumu,
bi rahmatika astaghiith,
aslih lii sha'niya kullah,
walaa takilnii ilaa nafsii tarfata ain.
"Tumeingia asubuhi na umekuwa Ufalme asubuhi ni wa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba heri za siku hii: ufunguzi wake, na nusura yake, na nuru yake, na baraka zake, na uongofu wake, na ninajikinga kwako kutokana na shari zilizomo ndani yake, na shari zilizo baada yake."120
(أَصْبَحْنَا وَأَصْبَحَ المُلْكُ لِلَّهِ رَبِّ العَالَمِينَ، اللَّهُـمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَ هَذَا اليَوْمِ: فَتْحَهُ، وَنَصْرَهُ، وَنورَهُ، وَبَرَكَتَهُ، وَهُدَاهُ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِيهِ وَشَرِّ مَا بَعْدَه).
Asbahna wa asbahal-mulku lillahi rabbil-aalamin. Allahumma inni as-aluka khaira haadhal-yaumi: fat-hahu, wa nasrahu, wa nurahu, wa barakatahu, wa hudahu, wa audhu bika min sharri maa fihi wa sharri maa baadah
Na anapofika jioni, atasema: "Tumeingia jioni na umekuwa Ufalme jioni ni wa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba heri za usiku huu: ufunguzi wake, na ushindi wake, na nuru yake, na baraka zake, na uongofu wake, na ninajilinda kwako kutokana na shari zilizomo ndani yake, na shari zilizo baada yake."121
(أَمْسَيْنَا وَأَمْسَى المُلْكُ لِلَّهِ رَبِّ العَالَمِينَ، اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَ هَذِهِ اللَّيْلَةِ: فَتْحَهَا، وَنَصْرَهَا، وَنُورَهَا، وَبَرَكَتَهَا، وَهُدَاهَا، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِيهَا، وَشَرِّ مَا بَعْدَهَا).
Amsaina wa amsal mulku lillahi rabbil aalamin. Allahumma inni as-aluka khaira hadhihil lailati: fat-haha, wa nasraha, wa nuraha, wa barakataha, wa hudaha, wa audhu bika min sharri ma fiha, wa sharri ma baadaha.
"Tumepambazukiwa katika umbile la Uislamu, na katika neno la Ikhlasi, na katika Dini ya Nabii wetu Muhammad, rehema na amani ziwe juu yake, na katika mila ya baba yetu Ibrahim, aliyekuwa muongofu, Muislamu, wala hakuwa miongoni mwa washirikina."122
(أَصْبَحْنا عَلَى فِطْرَةِ الإِسْلَامِ، وَعَلَى كَلِمَةِ الإِخْلاَصِ، وَعَلَى دِينِ نَبِيِّنَا مُحَمَّدٍ ﷺ، وَعَلَى مِلَّةِ أَبِينَا إِبْرَاهِيمَ، حَنِيفًا مُسْلِمًا وَمَا كَانَ مِنَ المُشرِكِين).
Asbahna ala fitratil islam, wa ala kalimatil ikhlas, wa ala dini nabiyina Muhammadin sallallahu alayhi wa salam, wa ala milati abina Ibrahima, hanifan musliman wa ma kana minal mushrikin.
Na ifikapo jioni, atasema: "Tumeingia jioni tukiwa katika maumbile ya Uislamu, na katika neno la Ikhlasi, na katika Dini ya Nabii wetu Muhammad, rehema na amani ziwe juu yake, na katika mila ya baba yetu Ibrahim, aliyekuwa muongofu, Muislamu, wala hakuwa miongoni mwa washirikina."123
(أَمْسَيْنَا عَلَى فِطْرَةِ الإِسْلَامِ، وَعَلَى كَلِمَةِ الإِخْلاَصِ، وَعَلَى دِينِ نَبِيِّنَا مُحَمَّدٍ ﷺ، وَعَلَى مِلَّةِ أَبِينَا إِبْرَاهِيمَ، حَنِيفًا مُسْلِمًا وَمَا كَانَ مِنَ المُشرِكِين).
Amsaina ala fitratil islam, wa ala kalimatil ikhlas, wa ala dini nabiyina Muhammadin swalalahu alaihi wa salam, wa ala milati abina Ibrahim, hanifan musliman wa ma kana minal mushrikin.
"(Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa zote ni zake)"
(سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِه).
Subhanallahi wa bihamdih
mara mia moja124.
"Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Yeye pekee asiye na mshirika, ufalme ni wake na sifa njema ni zake, naye juu ya kila kitu ni Muweza."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaha illallah wahdahu laa sharika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu, wa huwa ala kulli shayin kadiir.
Mara kumi125, au mara moja wakati wa uvivu126.
"Hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake asiye na mshirika, Mwenye ufalme na Mwenye sifa na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
La ilaha illallah, wahdahu la sharika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu, wa huwa ala kulli shayin kadir.
Mara mia moja asubuhi127.
"Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa zote ni zake: kwa idadi ya viumbe vyake, na ridhaa ya nafsi yake, na uzito wa Kiti chake cha Enzi, na wino wa maneno yake."
(سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ: عَدَدَ خَلْقِهِ، وَرِضَا نَفْسِهِ، وَزِنَةَ عَرْشِهِ، وَمِدَادَ كَلِمَاتِه).
Subhanallahi wa bihamdih: adada khalkih, wa ridha nafsih, wa zinata arshih, wa midada kalimatih
Mara tatu asubuhi128.
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba elimu yenye manufaa, na riziki nzuri, na matendo yenye kukubalika."
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ عِلْمًا نَافِعًا، وَرِزْقًا طَيِّبًا، وَعَمَلًا مُتَقَبَّلًا).
Allahumma inni as'aluka ilman nafian, wa rizkan tayyiban, wa amalan mutakabbalan
Anapopambaukiwa129.
"(Ninamtaka Mwenyezi Mungu msamaha na ninatubia kwake)."
(أَسْتَغْفِرُ اللَّهَ وَأَتُوبُ إِلَيْه).
Astaghfirullaha wa atubu ilaih
Mara mia moja kwa siku130.
"Ninajikinga kwa maneno makamilifu ya Mwenyezi Mungu kutokana na shari ya vile alivyoviumba."
(أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَق).
Auudhu bikalimaati llaahit taammaati min sharri maa khalak
Mara tatu ifikapo jioni131.
"Ewe Mwenyezi Mungu mpe rehema na amani Nabii wetu Muhammad."
(اللَّهُمَّ صَلِّ وَسَلِّمْ عَلَى نَبَيِّنَا مُحَمَّد).
Allahumma sali wa salim ala nabiyina Muhammad
Mara kumi132.
28. NYIRADI ZA KULALA
"Atakusanya viganja vyake, kisha atapuliza ndani yake na atasoma ndani yake:
﴿قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ1 ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ2 لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ3 وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ4﴾
1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa Pekee.
2. Mwenyezi Mungu ndiye Mkusudiwa.
3. Hakuzaa wala hakuzaliwa.
4. Wala hana anayelingana naye hata mmoja. [Al-Ikhlaas: 1-4].
﴿قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ1 مِن شَرِّ مَا خَلَقَ2 وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ3 وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ4 وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ5﴾
1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko.
2. Kutokana na shari ya alivyoviumba.
3. Na kutokana na shari ya giza la usiku liingiapo.
4. Na kutokana na shari ya wanaopuliza mafundoni.
5. Na kutokana na shari ya mwenye husuda anapohusudu.
[Al-Falaq: 1-5].
﴿قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ1 مَلِكِ ٱلنَّاسِ2 إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ3 مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ4 ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ5 مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ6﴾
1. Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu.
2. Mfalme wa watu.
3. Mungu wa watu.
4. Kutokana na shari ya Shetani mtia wasiwasi, ajifichaye mno (Al-Khannaas).
5. Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu.
6. Kutokana na majini na watu. [An-Nas: 1-6]
Kisha atafuta kwa viganja hivyo mwili wake kiasi awezacho kuanzia kichwani kwake na usoni kwake na mbele ya mwili wake." (Atafanya hivyo mara tatu)133.
﴿ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُۚ لَا تَأۡخُذُهُۥ سِنَةٞ وَلَا نَوۡمٞۚ لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ مَن ذَا ٱلَّذِي يَشۡفَعُ عِندَهُۥٓ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦۚ يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيۡءٖ مِّنۡ عِلۡمِهِۦٓ إِلَّا بِمَا شَآءَۚ وَسِعَ كُرۡسِيُّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۖ وَلَا يَـُٔودُهُۥ حِفۡظُهُمَاۚ وَهُوَ ٱلۡعَلِيُّ ٱلۡعَظِيمُ255﴾
"Mwenyezi Mungu - hakuna mungu isipokuwa Yeye, aliye hai, Msimamizi wa mambo yote milele. Hashikwi na kusinzia wala kulala. Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo duniani. Ni nani huyo awezaye kufanya uombezi mbele yake isipokuwa kwa idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao, na yaliyo nyuma yao, wala wao hawajui vyema chochote katika elimu yake isipokuwa kwa kile akitakacho. Kursi (mahali inapokanyaga miguu) yake imeenea mbingu na dunia, na wala halemewi katika kuvilinda vyote viwili. Na Yeye ndiye aliye juu zaidi, Mkuu." [Al-Baqara: 255]134.
﴿ءَامَنَ ٱلرَّسُولُ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مِن رَّبِّهِۦ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَۚ كُلٌّ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَمَلَٰٓئِكَتِهِۦ وَكُتُبِهِۦ وَرُسُلِهِۦ لَا نُفَرِّقُ بَيۡنَ أَحَدٖ مِّن رُّسُلِهِۦۚ وَقَالُواْ سَمِعۡنَا وَأَطَعۡنَاۖ غُفۡرَانَكَ رَبَّنَا وَإِلَيۡكَ ٱلۡمَصِيرُ285 لَا يُكَلِّفُ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ لَهَا مَا كَسَبَتۡ وَعَلَيۡهَا مَا ٱكۡتَسَبَتۡۗ رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذۡنَآ إِن نَّسِينَآ أَوۡ أَخۡطَأۡنَاۚ رَبَّنَا وَلَا تَحۡمِلۡ عَلَيۡنَآ إِصۡرٗا كَمَا حَمَلۡتَهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِنَاۚ رَبَّنَا وَلَا تُحَمِّلۡنَا مَا لَا طَاقَةَ لَنَا بِهِۦۖ وَٱعۡفُ عَنَّا وَٱغۡفِرۡ لَنَا وَٱرۡحَمۡنَآۚ أَنتَ مَوۡلَىٰنَا فَٱنصُرۡنَا عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ286﴾
"Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake Mlezi, na Waumini vile vile. Wote wamemwamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutofautishi baina ya yeyote katika Mitume wake, na (Waumini) husema: Tumesikia na tumetii. Tunakutaka maghfira Mola wetu Mlezi! Na marejeo ni kwako.
Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote isipokuwa kwa kiwango cha iwezavyo. Faida ya iliyoyachuma ni yake, na hasara ya iliyoyachuma ni juu yake pia. (Semeni) Mola wetu Mlezi! Usituchukulie ubaya tukisahau au tukikosea. Mola wetu Mlezi! Usitubebeshe mzigo kama uliyowabebesha wale waliokuwa kabla yetu. Mola wetu Mlezi! Usitutwike tusiyoyaweza, na uyatupilie mbali mabaya yetu, na utusamehe na uturehemu. Wewe ndiye Mlinzi wetu. Basi tupe ushindi dhidi ya watu walio makafiri." [Al Baqara: 285-286]135.
"Kwa jina lako136 Mola wangu Mlezi, nimeuweka chini ubavu wangu, na kwa sababu yako nitauinua, basi ukishika roho yangu, basi irehemu, na ukiiachia basi ihifadhi, kwa kile unachowahifadhi kwacho waja wako wema."137
(بِاسْمِكَ رَبِّي وَضَعْتُ جَنْبِي، وَبِكَ أَرْفَعُهُ، فَإِنْ أَمْسَكْتَ نَفْسِي فَارْحَمْهَا، وَإِنْ أَرْسَلْتَهَا فَاحْفَظْهَا، بِمَا تَحْفَظُ بِهِ عِبَادَكَ الصَّالِحِين).
Bismika Rabbi wadha'tu jambi, wa bika arfa'uhu, fa in amsakta nafsi farhamha, wa in arsaltaha fahfadh-ha, bima tahfadhu bihi ibadakas-swaalihin.
“Ewe Mwenyezi Mungu, hakika Wewe umeumba nafsi yangu na Wewe unaifisha. Kwako ni kifo chake na uhai wake, ukiipa uhai, basi ihifadhi, na ukiifisha, basi isamehe. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba salama.”138
(اللَّهُمَّ إِنَّكَ خَلَقْتَ نَفْسِي وَأَنْتَ تَوَفَّاهَا، لَكَ مَمَاتُهَا وَمَحْياهَا، إِنْ أَحْيَيْتَهَا فَاحْفَظْهَا، وَإِنْ أَمَتَّهَا فَاغْفِرْ لَهَا، اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ العَافِيَة).
Allahumma innaka khalakta nafsi wa anta tawaffaha, laka mamatuha wa mahyaha, in ahyaytaha fahfadh-ha, wa in amattaha faghfir laha, Allahumma inni as-aluka al-afiya.
"Ewe Mwenyezi Mungu nikinge139 na adhabu yako siku utakapowafufua waja wako."140
(اللَّهُمَّ قِنِي عَذَابَكَ يَوْمَ تَبْعَثُ عِبَادَك).
Allahumma kini adhabaka yauma tab'athu ibadak
"Yaani: Kwa jina lako Mola wangu ninakufa, na ninakuwa hai."141
(بِاسْمِكَ اللَّهُمَّ أَمُوتُ وَأَحْيَا).
Bismika Allahumma amutu wa ahya
"(Ametakasika Mwenyezi Mungu)."
(سُبْحَانَ اللَّه).
Subhanallah
(Mara thelathini na tatu) Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu.
(وَالحَمْدُ لِلَّه).
Walhamdu lillah
(Mara thelathini na tatu) Na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa
(وَاللَّهُ أَكْبَر).
Wallahu Akbar
(Mara thelathini na nne)."142.
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa ardhi, na Mola Mlezi wa Kiti cha Enzi kitukufu, Mola wetu Mlezi na Mola Mlezi wa kila kitu, Mwenye kupasua mbegu na kokwa, na Mwenye kuteremsha Taurati na Injili na Qur'ani, ninajikinga kwako kutokana na shari ya kila kitu Wewe ni mwenye kukishika kwa nywele za utosi. Ewe Mwenyezi Mungu, Wewe ndiye wa Mwanzo, hakuna kitu kabla yako, na Wewe ndiye wa Mwisho, hakuna kitu baada yako, na Wewe ni wa Wazi, hakuna kitu juu yako, na Wewe ni wa Ndani, hakuna kitu chini yako, tulipie madeni na ututosheleze kutokana na ufakiri."143
(اللَّهُمَّ رَبَّ السَّمَوَاتِ السَّبْعِ وَرَبَّ الأَرْضِ، وَرَبَّ العَرْشِ العَظِيمِ، رَبَّنَا وَرَبَّ كُلِّ شَيْءٍ، فَالِقَ الحَبِّ وَالنَّوَى، وَمُنْزِلَ التَّوْرَاةِ وَالإِنْجِيلِ، وَالفُرْقَانِ، أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ كُلِّ شَيْءٍ أَنْتَ آخِذٌ بِنَاصِيَتِهِ، اللَّهُمَّ أَنْتَ الأَوَّلُ فَلَيْسَ قَبْلَكَ شَيْءٌ، وَأَنْتَ الآخِرُ فَلَيسَ بَعْدَكَ شَيْءٌ، وَأَنْتَ الظَّاهِرُ فَلَيْسَ فَوْقَكَ شَيْءٌ، وَأَنْتَ البَاطِنُ فَلَيْسَ دُونَكَ شَيْءٌ، اقْضِ عَنَّا الدَّيْنَ وَأَغْنِنَا مِنَ الفَقْر).
Allahumma rabba ssamawati ssab'i wa rabbal ardhi, wa rabbal arshil adhimi, rabbana wa rabba kulli shay-in, faliqal habbi wannawa, wa munzilat tawrati wal injili, wal furqani, audhu bika min sharri kulli shay-in anta akhidhun binasiyatihi, Allahumma antal awwalu falaysa qablaka shay-un, wa antal akhiru falaysa baadaka shay-un, wa antadh dhahiru falaysa fawqaka shay-un, wa antal batinu falaysa dunaka shay-un, iqdhi annad dayna wa aghnina minal faqr.
"Kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyetulisha na akatunywesha, na akatutosheleza na akatuhifadhi, kwani ni wangapi wasiokuwa na wa kuwatosheleza wala wa kuwahifadhi."144
(الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي أَطْعَمَنَا وَسَقَانَا، وَكَفَانَا، وَآوَانَا، فَكَمْ مِمَّنْ لَا كَافِيَ لَهُ وَلَا مُؤْوِي).
Alhamdu lillahi alladhi at'amana wa saqana, wa kafana, wa awana, fakam mimman la kafiya lahu wala muuwi.
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa ghaibu na yenye kushuhudiwa, Muumba wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa kila kitu na Mmiliki wake, nashuhudia ya kwamba hapana mungu ila Wewe. Najikinga kwako kutokana na shari ya nafsi yangu, na kutokana na shari ya Shetani na ushirikina wake, na nisifanye maovu juu ya nafsi yangu au kuyaleta kwa Muislamu."145
(اللَّهُمَّ عَالِمَ الغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ فَاطِرَ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ، رَبَّ كُلِّ شَيْءٍ وَمَلِيكَهُ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ نَفْسِي، وَمِنْ شَرِّ الشَّيْطانِ وَشِرْكِهِ، وَأَنْ أَقْتَرِفَ عَلَى نَفْسِي سُوءًا، أَوْ أَجُرَّهُ إِلَى مُسْلِم).
Allahumma aalimal-ghaibi wash-shahadati faatiras-samawati wal-ardi, rabba kulli shai-in wa maliikahu, ash-hadu an laa ilaha illa anta, auudhu bika min sharri nafsii, wa min sharrish-shaitani wa shirkihi, wa an aktarifa alaa nafsii suu-an, au ajurrahu ilaa muslim.
"Atasoma 'Alif Lam Miim' Tanzil As-Sajdah, na 'Ametukuka ambaye mkononi mwake umo Ufalme wote."146.
"Ewe Mwenyezi Mungu147 nimeisalimisha nafsi yangu kwako, na nimekukabidhi jambo langu kwako, na nimeelekeza uso wangu kwako, na nimeutegemeza mgongo wangu kwako, kwa matumaini na hofu kwako, hapana makimbilio wala kukombolewa kutokana na Wewe isipokuwa kwako, nimekiamini Kitabu chako ulichokiteremsha, na Nabii wako uliyemtuma."148
(اللَّهُمَّ أَسْلَمْتُ نَفْسِي إِلَيْكَ، وَفَوَّضْتُ أَمْرِي إِلَيْكَ، وَوَجَّهْتُ وَجْهِي إِلَيْكَ، وَأَلْجَأْتُ ظَهْرِي إِلَيْكَ، رَغْبَةً وَرَهْبَةً إِلَيْكَ، لَا مَلْجَأَ وَلَا مَنْجَا مِنْكَ إِلَّا إِلَيْكَ، آمَنْتُ بِكِتَابِكَ الَّذِي أَنْزَلْتَ، وَبِنَبِيِّكَ الَّذِي أَرْسَلْت).
Allahumma aslamtu nafsi ilaika, wa fawwadhtu amri ilaika, wa wajjahtu wajhi ilaika, wa aljaatu dhahri ilaika, raghbatan wa rahbatan ilaika, laa maljaa wa laa manjaa minka illaa ilaika, aamantu bi kitabikal ladhi anzalta, wa bi nabiyyikal ladhi arsalt.
29. DUA WAKATI UNAPOGEUKA USIKU
"Hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mshindi, Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwingi wa kusamehe”.149
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ الوَاحِدُ القَهّارُ، رَبُّ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا العَزيزُ الغَفَّار).
Laa ilaaha illallaah, Al waahidul qahhaar, Rabbus samawaati wal ardhi wamaa baynahumaa, Al aziizul ghaffaar.
30. DUA YA MFADHAIKO USINGIZINI, NA MWENYE KUPATA MTIHANI WA KUHISI UPWEKE
“Ninajikinga kwa maneno makamilifu ya Mwenyezi Mungu kutokana na ghadhabu yake na adhabu yake, na shari ya waja wake, na minong’ono ya mashetani, na wasinikaribie.”150
(أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ غَضَبِهِ وَعِقَابِهِ، وَشَرِّ عِبَادِهِ، وَمِنْ هَمَزَاتِ الشَّياطِينِ وَأَنْ يَحْضُرُون).
Audhu bikalimatillahit tammati min ghadhabihi wa ikabihi, wa sharri ibadihi, wa min hamazatish shayatini wa ay yahdhurun.
31. ANACHOTAKIWA KUFANYA MWENYE KUOTA NDOTO MBAYA
(Atapuliza kushoto kwake) (mara tatu)151.
(Atajilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani, na kutokana na shari za alicho kiona) (Mara tatu)152.
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitanir rajiim
(Asimsimulie yeyote)153.
(Atageukia ubavu mwingine, badala ya ule aliokuwa ameulalia)154.
"Atasimama asali akitaka kufanya hivyo."155.
32. MAOMBI YA KUNUTI YA WITIRI
"Ewe Mwenyezi Mungu, niongoze miongoni mwa uliowaongoza, na unipe salama miongoni mwa waliopewa salama, na unisimamie miongoni mwa uliowasimamia, na unibariki katika kile ulichonipa, na unikinge kutokana na shari ulizozipitisha. Kwani hakika Wewe unapitisha hukumu na wala hupitishiwi hukumu. Na hakika hatodhalilika uliyemuweka karibu, [na wala hatotukuka uliyemfanyia uadui]. Umetukuka Mola wetu Mlezi na umetakasika."156
(اللَّهُمَّ اهْدِنِي فِيمَنْ هَدَيْتَ، وَعَافِنِي فِيمَنْ عَافَيْتَ، وَتَوَلَّنِي فِيمَنْ تَوَلَّيْتَ، وَبَارِكْ لِي فِيمَا أَعْطَيْتَ، وَقِنِي شَرَّ مَا قَضَيْتَ؛ فَإِنَّكَ تَقْضِي وَلَا يُقْضَى عَلَيْكَ، إِنَّهُ لَا يَذِلُّ مَنْ وَالَيْتَ، [وَلاَ يَعِزُّ مَنْ عَادَيْتَ]، تَبارَكْتَ رَبَّنا وَتَعَالَيْت).
Allahumma ihdini fiman hadayt, wa afini fiman afayt, wa tawallani fiman tawallayt, wa barik li fima atayt, wa kini sharra ma kadhayt; fa innaka takdhi wa la yukdha alayk, innahu la yadhillu man walayt, wa la yaizzu man adayt, tabarakta rabbana wa taalayt.
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najikinga kwa radhi zako kutokana na hasira zako, na kwa usalama wako kutokana na adhabu zako, na ninajikinga kwako kutokana na Wewe, wala siwezi kuhesabu sifa zako, kama ulivyojisifu Wewe mwenyewe."157
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِرِضَاكَ مِنْ سَخَطِكَ، وَبِمُعَافَاتِكَ مِنْ عُقُوبَتِكَ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْكَ، لَا أُحْصِي ثَنَاءً عَلَيْكَ، أَنْتَ كَمَا أَثْنَيْتَ عَلَى نَفْسِك).
Allahumma inni audhu biridhaka min sakhatika, wa bimuafatika min uqubatika, wa audhu bika minka, la uhsi thana-an alayka, anta kama athnayta ala nafsik.
"Tafsiri: "Ewe Mwenyezi Mungu, ni Wewe tu tunayekuabudu, na kwako tunaswali na kusujudu, na kwako tunajitahidi na kuharakisha, tunataraji rehema yako, na tunaogopa adhabu yako, hakika adhabu yako itawafikia makafiri. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika sisi tunakuomba msaada, na tunakuomba msamaha, na tunakusifu kwa heri, wala hatukukufuru, na tunakuamini, na tunakunyenyekea, na tunamwacha anayekukufuru."158
(اللَّهُمَّ إِيَّاكَ نعْبُدُ، وَلَكَ نُصَلِّي وَنَسْجُدُ، وَإِلَيْكَ نَسْعَى وَنَحْفِدُ، نَرْجُو رَحْمَتَكَ، وَنَخْشَى عَذَابَكَ، إِنَّ عَذَابَكَ بِالكَافِرِينَ مُلْحِقٌ، اللَّهُمَّ إِنَّا نَسْتَعِينُكَ، وَنَسْتَغْفِرُكَ، وَنُثْنِي عَلَيْكَ الخَيْرَ، وَلَا نَكْفُرُكَ، وَنُؤْمِنُ بِكَ، وَنَخْضَعُ لَكَ، وَنَخْلَعُ مَنْ يَكْفرُك).
Allahumma iyyaka naabudu, wa laka nuswalli wa nasjudu, wa ilayka nasaa wa nahfidu, narju rahmataka, wa nakhsha adhabaka, inna adhabaka bilkafirina mulhik, Allahumma inna nastainuka, wa nastaghfiruka, wa nuthni alaykal khayra, wala nakfuruka, wa nuuminu bika, wa nakhdhau laka, wa nakhlau man yakfuruk.
33. DHIKIRI BAADA YA SALAMU YA KUMALIZA WITIRI
"Utakasifu ni wa Mfalme Mtakatifu"
(سُبْحَانَ المَلِكِ القُدُّوس).
Subhaanal malikil kudduus
Mara tatu Na mara ya tatu ataisema kwa sauti ya juu na kuivuta sauti yake akisema: "Mola wa Malaika na roho (Jibrili).159
(رَبِّ المَلَائِكَةِ وَالرُّوح).
Rabbil malaikati waruuh
34. DUA YA WASIWASI NA HUZUNI
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mja wako, mtoto wa mja wako, mtoto wa kijakazi wako. Nywele zangu za utosi zipo mkononi mwako. Hukumu zako kwangu ni zenye kupita, na maamuzi yako kwangu ni ya uadilifu. Ninakuomba kupitia kila jina lako, ulilojiita kwalo mwenyewe, au uliloteremsha ndani ya Kitabu chako, au ulilomfundisha yeyote katika viumbe wako, au ulilificha ndani ya elimu ya ghaibu iliyo kwako, kwamba uifanye Qur'ani ndiyo kitulizo cha moyo wangu, na mwangaza wa kifua changu, na kiondoshaji cha huzuni yangu, na kimalizaji cha msongo wa mawazo yangu."160
(اللَّهُمَّ إِنِّي عَبْدُكَ، ابْنُ عَبْدِكَ، ابْنُ أَمَتِكَ، نَاصِيَتِي بِيَدِكَ، مَاضٍ فِيَّ حُكْمُكَ، عَدْلٌ فِيَّ قَضَاؤُكَ، أَسْأَلُكَ بِكُلِّ اسْمٍ هُوَ لَكَ، سَمَّيْتَ بِهِ نَفْسَكَ، أَوْ أَنْزَلْتَهُ فِي كِتَابِكَ، أَوْ عَلَّمْتَهُ أَحَدًا مِنْ خَلْقِكَ، أَوِ اسْتَأْثَرْتَ بِهِ فِي عِلْمِ الغَيْبِ عِنْدَكَ، أَنْ تَجْعَلَ القُرْآنَ رَبِيعَ قَلْبِي، وَنُورَ صَدْرِي، وَجَلَاءَ حُزْنِي، وَذَهَابَ هَمِّي).
Allahumma inni abduka, ibnu abdika, ibnu amatika, nasiyati biyadika, madhin fiyya hukmuka, adlun fiyya kadhauka, as'aluka bikulli ismin huwa laka, sammaita bihi nafsaka, au anzaltahu fi kitabika, au allamtahu ahadan min khalkika, awis tatharta bihi fi ilmil ghaibi indaka, an taj'alal kuraana rabia kalbi, wa nura sadri, wa jalaa huzni, wa dhahaba hammi.
“Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na msongo wa mawazo na huzuni, na kushindwa na uvivu, na ubahili na woga, na kuelemewa na deni na kuzidiwa nguvu na watu.”161
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ الهَمِّ وَالحَزَنِ، وَالعَجْزِ وَالكَسَلِ، وَالبُخْلِ وَالجُبْنِ، وَضَلَعِ الدَّيْنِ وَغَلَبَةِ الرِّجَال).
Allahumma inni audhu bika minal hammi wal hazani, wal ajzi wal kasali, wal bukhli wal jubni, wa dhalai deini wa ghalabatir rijal.
35. DUA WAKATI WA MATATIZO
"Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Mkuu, Mpole. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa Kiti Kikuu cha Enzi. Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa mbingu na Mola Mlezi wa ardhi, na Mola Mlezi wa Kiti Kitukufu cha Enzi."162
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ العَظِيمُ الحَلِيمُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ رَبُّ العَرْشِ العَظِيمِ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ رَبُّ السَّمَوَاتِ وَرَبُّ الأَرْضِ وَرَبُّ العَرْشِ الكَرِيم).
La ilaha illa allah al-adhim alhalim, la ilaha illa allah rabbul-arshir adhim, la ilaha illa allah rabbus-samawat warabbul-ardh warabbul-arsh alkarim
"Ewe Mwenyezi Mungu, ninataraji rehema zako, basi usiniache kujisimamia kwa kiasi cha kupepesa jicho, na unitengenezee mambo yangu yote, hakuna mungu ila Wewe."163
(اللَّهُمَّ رَحْمَتَكَ أَرْجُو، فَلَا تَكِلْنِي إِلَى نَفْسِي طَرْفَةَ عَيْنٍ، وَأَصْلِحْ لِي شَأْنِي كُلَّهُ، لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْت).
Allahumma rahmataka arju, fala takilni ila nafsi tarfata ainin, wa aslih li shaani kullahu, la ilaha illa anta.
"Hakuna mungu ila Wewe, umetakasika. Hakika mimi nilikuwa katika madhalimu.”164
(لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي كُنْتُ مِنَ الظَّالِمِين).
Laa ilaha illa anta subhaanaka inni kuntu minadh-dhaalimiin
"Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu Mlezi. Simshirikishi na chochote."165
(اللَّهُ اللَّهُ رَبِّي لَا أُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا).
Allahu Allahu Rabbi, laa ushriku bihi shai-an.
36. DUA YA KUKUTANA NA ADUI NA MWENYE MAMLAKA
"Ewe Mwenyezi Mungu hakika sisi tunakuweka wewe shingoni mwao, na tunajilinda kwako kutokana na shari zao.”166
(اللَّهُمَّ إِنَّا نَجْعَلُكَ فِي نُحُورِهِم، وَنَعُوذُ بِكَ مِنْ شُرُورِهِم).
Allahumma inna naj'aluka fi nuhurihim, wa na'udhu bika min shururihim
"Ewe Mwenyezi Mungu Wewe ndiye nguvu yangu, na Wewe ndiye mnusuru wangu, kwa ajili yako ninasonga, na kwa ajili yako ninashambulia, na kwa ajili yako ninapigana."167
(اللَّهُمَّ أَنْتَ عَضُدِي، وَأَنْتَ نَصِيرِي، بِكَ أَحُولُ وَبِكَ أَصُولُ، وَبِكَ أُقاتِل).
Allahumma anta adhudii, wa anta nasiirii, bika ahuulu wa bika asuulu, wa bika ukaatil
"Mwenyezi Mungu anatutosha, naye ni mbora wa kutegemewa."168
(حَسْبُنا اللَّهُ وَنِعْمَ الوَكِيل).
Hasbunallahu wa ni'mal wakiil
37. MAOMBI YA MWENYE KUOGOPA DHULMA YA MTAWALA
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa mbingu saba, na Mola Mlezi wa Kiti cha Enzi kikuu, kuwa mlinzi wangu kutokana na fulani bin fulani, na makundi yake miongoni mwa viumbe vyako, asije yeyote miongoni mwao akanipitukia mipaka au kunifanyia jeuri. Ametukuka aliye katika ulinzi wako, na sifa zako ni tukufu, na hakuna mungu isipokuwa Wewe.”169
(اللَّهُمَّ ربَّ السَّمَوَاتِ السَّبْعِ، وَرَبَّ العَرْشِ العَظِيمِ، كُنْ لِي جَارًا مِنْ فُلَانِ بْنِ فُلَانٍ، وَأَحْزَابِهِ مِنْ خَلَائِقِكَ، أَنْ يَفْرُطَ عَلَيَّ أَحَدٌ مِنْهُمْ أَوْ يَطْغَى، عَزَّ جَارُكَ، وَجَلَّ ثَنَاؤُكَ، وَلَا إِلَهَ إِلَّا أَنْت).
Allahumma rabbas-samawatis-sab'i, wa rabbal-arshil-adhiimi, kun lii jaaran min fulani bni fulanin, wa ahzabihi min khala-iqika, an yafruta alayya ahadun minhum aw yat-gha, azza jaruka, wa jalla thana-uka, wa la ilaha illa anta.
"(Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu zaidi kuliko viumbe vyake vyote, Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu zaidi kuliko ninavyoviogopa na kuvitahadhari. Ninajilinda kwa Mwenyezi Mungu ambaye hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye, Mwenye kuzishikilia mbingu saba zisianguke juu ya ardhi isipokuwa kwa idhini yake, kutokana na shari ya mja wako fulani, na majeshi yake, na wafuasi wake, na wasaidizi wake, miongoni mwa majini na watu. Ewe Mwenyezi Mungu, kuwa mlinzi wangu kutokana na shari zao, zimetukuka sifa zako, na hifadhi yako ina nguvu, na limetukuka jina lako, na hakuna mungu isipokuwa Wewe)."
(اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَعَزُّ مِنْ خَلْقِهِ جَمِيعًا، اللَّهُ أَعَزُّ مِمَّا أَخَافُ وَأَحْذَرُ، أَعُوذُ بِاللَّهِ الَّذِي لَا إِلَهَ إِلَّا هُوَ، المُمْسِكِ السَّمَوَاتِ السَّبْعِ أَنْ يَقَعْنَ عَلَى الأَرْضِ إِلَّا بِإِذْنِهِ، مِنْ شَرِّ عَبْدِكَ فُلَانٍ، وَجُنُودِهِ وَأَتْبَاعِهِ وَأَشْيَاعِهِ، مِنَ الجِنِّ وَالإِنْسِ، اللَّهُمَّ كُنْ لِي جَارًا مِنْ شَرِّهِمْ، جَلَّ ثَنَاؤُكَ وَعَزَّ جَارُكَ، وَتَبَارَكَ اسْمُكَ، وَلَا إِلَهَ غَيْرُك).
Allahu akbaru, Allahu aazzu min khalkihi jamian, Allahu aazzu mimma akhafu wa ahdharu, audhu billahil ladhi la ilaha illa huwa, al mumsikis samawatis sab'i an yaka'na alal ardhi illa bi idhnihi, min sharri abdika fulanin, wa junudihi wa atba'ihi wa ashya'ihi, minal jinni wal insi, Allahumma kun li jaran min sharrihim, jalla thanauka wa azza jaruka, wa tabaraka ismuka, wa la ilaha ghairuk.
Mara tatu170.
38. DUA DHIDI YA ADUI
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mteremsha Kitabu, Mwepesi wa kuhesabu, yashinde makundi ya maadui. Ewe Mwenyezi Mungu, yashinde na uyatetemeshe."171
(اللَّهُمَّ مُنْزِلَ الكِتَابِ، سَرِيعَ الحِسَابِ، اهْزِمِ الأَحْزَابَ، اللَّهُمَّ اهزِمْهُمْ وَزَلْزِلْهُم).
Allahumma munzilal kitabi, sari'al hisabi, ihzimil ahzaba. Allahumma ihzimhum wa zalzilhum.
39. ANAYOTAKIWA KUSEMA MWENYE KUWAOGOPA WATU
"Tafsiri: Ewe Mwenyezi Mungu nilinde kutokana na wao kwa namna utakavyo."172
(اللَّهُمَّ اكْفِنِيهِمْ بِمَا شِئْتَ).
Allahumma ikfiniihim bimaa shi't
40. DUA YA MTU ALIYEPATWA NA WASIWASI KATIKA IMANI
(Aombe kinga kwa Mwenyezi Mungu)173. Atasema: "Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa."
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitanir rajim
"Aache yale aliyopata wasiwasi ndani yake."174
"Atasema: "Nimemuamini Mwenyezi Mungu na Mitume wake.""175
(آمَنْتُ بِاللَّهِ وَرُسُلِه).
Aamantu billahi wa rusulih
"Atasoma kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:
﴿هُوَ ٱلۡأَوَّلُ وَٱلۡأٓخِرُ وَٱلظَّٰهِرُ وَٱلۡبَاطِنُۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ 3﴾
'Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa Mwisho, naye ndiye wa Dhahiri na wa Siri, naye ndiye ajuaye zaidi kila kitu.'" [Al-hadid: 3]176
41. DUA YA KULIPA DENI
"Tafsiri: Ewe Mwenyezi Mungu nitosheleze kwa halali yako dhidi ya haramu yako, na unitajirishe kwa fadhila zako nisimuhitaji yeyote asiyekuwa Wewe."177
(اللَّهُمَّ اكْفِنِي بِحَلَالِكَ عَنْ حَرَامِكَ، وَأَغْنِنِي بِفَضْلِكِ عَمَّنْ سِوَاك).
Allahumma ikfini bihalalika an haramika, wa aghnini bifadhlika amman siwak.
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na msongo wa mawazo na huzuni, na kushindwa na uvivu, na ubahili na woga, na kuelemewa na deni na kuzidiwa nguvu na watu.”178
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ الهَمِّ وَالحَزَنِ، وَالعَجْزِ وَالكَسَلِ، وَالبُخْلِ وَالجُبْنِ، وَضَلَعِ الدَّيْنِ وَغَلَبَةِ الرِّجَال).
Allahumma inni a'udhu bika minal hammi wal hazani, wal ajzi wal kasali, wal bukhli wal jubni, wa dala'id daini wa ghalabatir rijal.
42. DUA YA MTU ANAPOPATWA NA WASIWASI KATIKA SWALA NA KISOMO
"Yaani: Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Shetani aliyelaaniwa."
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitanir rajim
Na tema mate upande wako wa kushoto (Mara tatu)179.
43. DUA YA LITAKAYEKUWA JAMBO GUMU KWAKE
"Ewe Mwenyezi Mungu hakuna jepesi ila lile ulilolifanya kuwa jepesi, na Wewe huifanya huzuni kuwa nyepesi.”180
(اللَّهُمَّ لَا سَهْلَ إِلَّا مَا جَعَلْتَهُ سَهْلًا، وَأَنْتَ تَجْعَلُ الحَزْنَ إِذَا شِئْتَ سَهْلًا).
Allahumma la sahla illa ma ja'altahu sahlan, wa anta taj'alu al-hazna idha shi'ta sahla
44. ANACHOSEMA NA KUFANYA ATAKAYEFANYA DHAMBI
"Hakuna mja yeyote atakayetenda dhambi, akajitwaharisha vizuri, kisha akasimama na akaswali rakaa mbili, kisha akamuomba Mwenyezi Mungu msamaha, isipokuwa Mwenyezi Mungu humsamehe."181
45. DUA YA KUMFUKUZA SHETANI NA WASIWASI WAKE
(Kujikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana naye)182.
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitanir rajiim
(Adhana)183.
(Dhikiri na kusoma Qur'ani).
"Msiyafanye majumba yenu kuwa makaburi. Hakika Shetani hukimbia kutoka katika nyumba inayosomwa suratul Baqara ndani yake."184
Na miongoni mwa mambo yanayomfukuza Shetani ni nyiradi za asubuhi na jioni, na kabla ya kulala na kuamka, na nyiradi za kuingia na kutoka nyumbani, na nyiradi za kuingia na kutoka msikitini, na nyiradi nyinginezo zinazoruhusiwa kisheria, kama vile: kusoma Ayatul-Kursi wakati wa kulala, na aya mbili za mwisho za suratul-Baqarah, na mwenye kusema: "Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake asiye na mshirika, ufalme ni wake na sifa njema ni zake, naye juu ya kila kitu ni muweza."
(لَا إِلٰهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ، وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaaha illallaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu, wa huwa alaa kulli shayin kadiir.
mara mia moja, itakuwa ni kinga kwake kutokana na Shetani siku yake yote.185 Na vilevile Adhana humfukuza Shetani.
46. KUOMBA PINDI LINAPOTOKEA JAMBO ASILOLIPENDA AU AKASHINDWA NA JAMBO LAKE
"Kudura ya Mwenyezi Mungu, na atakalo hufanya."186
(قَدَرُ اللَّهُ وَمَا شَاءَ فَعَل).
Kadarullahu wa maa shaa fa'ala
47. Pongezi kwa aliye ruzukiwa mtoto na majibu yake.
"Mwenyezi Mungu akubariki katika ulichopewa, na umshukuru Mtoaji, na afikie utu uzima, na uruzukiwe wema wake."187
(بَارَكَ اللَّهُ لَكَ فِي المَوْهُوبِ لَكَ، وَشَكَرْتَ الوَاهِبَ، وَبَلَغَ أَشُدَّهُ، وَرُزِقْتَ بِرَّه).
Barakallahu laka fil mawhuubi laka, wa shakartal waahiba, wa balagha ashuddahu, wa ruzikta birrah.
Na atamjibu yule aliyepewa hongera akisema: "(Mwenyezi Mungu akubariki na atie baraka juu yako, na Mwenyezi Mungu akulipe kheri, na akuruzuku mfano wake, na akuzidishie thawabu zako)."188
(بَارَكَ اللَّهُ لَكَ وَبَارَكَ عَلَيْكَ، وَجَزَاكَ اللَّهُ خَيْرًا، وَرَزَقَكَ اللَّهُ مِثْلَهُ، وَأَجْزَلَ ثَوَابَك).
Baarakallahu laka wa baaraka alaika, wa jazaakallahu khairan, wa razaqakallahu mithlahu, wa ajzala thawaabak
48. MANENO YA KUWAKINGA WATOTO
Mtume rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akiwatafutia ulinzi wa Mwenyezi Mungu Hassan na Hussein radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao. "Ninawakinga nyinyi wawili kwa maneno makamilifu ya Mwenyezi Mungu kutokana na kila shetani na wadudu wenye sumu, na kutokana na kila jicho baya.”189
(أُعِيذُكُمَا بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّةِ مِنْ كُلِّ شَيْطَانٍ وَهَامَّةٍ، وَمِنْ كُلِّ عَيْنٍ لَامَّة).
Uiidhukumaa bikalimaatillahi at-taammati, min kulli shaitaanin wa haammatin, wa min kulli ainin laammah.
49. DUA YA KUMUOMBEA MGONJWA WAKATI WA KUMTEMBELEA
"Hakuna kitu kibaya, utapona akipenda Mwenyezi Mungu."190
(لَا بأْسَ طَهُورٌ إِنْ شَاءَ اللَّه).
Laa ba'sa tahuurun in shaa Allah
"Namuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu, Mola wa Arshi Tukufu kwamba akuponye."
(أَسْأَلُ اللَّهَ العَظِيمَ رَبَّ العَرْشِ العَظِيمِ أَنْ يَشْفيَك).
As'alul-lahal adhima rabbal arshil adhimi an yashfiyak
Mara saba191.
50. FADHILA ZA KUMTEMBELEA MGONJWA
Amesema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Mtu anapomtembelea ndugu yake Muislamu, hutembea katika machumo ya peponi mpaka anapokaa. Na anapokaa, hufunikwa na rehema. Basi ikiwa ni asubuhi, humuombea Malaika elfu sabini mpaka jioni, na ikiwa ni jioni, humuombea Malaika elfu sabini mpaka asubuhi."192
51. MAOMBI YA MGONJWA AMBAYE AMEKATA TAMAA YA MAISHA YAKE
"Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe, na unirehemu, na unikutanishe na rafiki wa juu zaidi."193
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَأَلْحِقْنِي بِالرَّفِيقِ الأَعْلَى).
Allahumma ighfir li, warhamni, wa alhikni bir rafikil aala.
Alianza Mtume rehema na amani ziwe juu yake wakati wa mauti yake kuingiza mikono yake katika maji, akawa anafuta kwayo uso wake, na kusema: "Hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّه).
La ilaha illallah
"Hakika mauti yana uchungu."194."
Yaani: Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu."195
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَاللَّهُ أَكْبَرُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَلَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّه).
La ilaha illallahu wallahu akbar, la ilaha illallahu wahdahu, la ilaha illallahu wahdahu la sharika lahu, la ilaha illallahu lahul mulku wa lahul hamdu, la ilaha illallahu wala hawla wala kuwwata illa billah.
52. KUMTAMKISHA SHAHADA MTU ANAYEKARIBIA KUFA
"Yeyote ambaye maneno yake ya mwisho yatakuwa:
Hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّه).
Laa ilaaha illallaah
ataingia peponi."196
53. DUA YA MWENYE KUPATWA NA MSIBA
(Hakika sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu na hakika kwake tutarejea. Ewe Mwenyezi Mungu nipe malipo katika msiba wangu na unipe badala bora kuliko hilo).197
(إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ، اللَّهُمَّ أْجُرْنِي فِي مُصِيبَتِي، وَأَخْلِفْ لِي خَيْرًَا مِنْهَا).
Inna lillahi wa inna ileyhi rajiun. Allahumma jurni fi musibati, wa akhlif li kheiran minha.
54. DUA WAKATI WA KUMFUMBA MACHO MAITI
"Tafsiri: "Ewe Mwenyezi Mungu, msamehe fulani (kwa jina lake), na uinue daraja yake miongoni mwa walioongoka, na uwe mbadala wake katika kizazi chake kilichobaki nyuma, na utusamehe sisi na yeye ewe Mola Mlezi wa walimwengu, na mpanulie kaburi lake, na umwekee nuru ndani yake."198
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِفُلَانٍ (بِاسْمِهِ) وَارْفَعْ دَرَجَتَهُ فِي المَهْدِيِّينَ، وَاخْلُفْهُ فِي عَقِبِهِ فِي الغَابِرِينَ، وَاغْفِرْ لَنَا وَلَهُ يَا رَبَّ العَالَمِينَ، وَافْسَحْ لَهُ فِي قَبْرِهِ، وَنَوِّرْ لَهُ فِيه).
Allahummaghfir lifulanin bismihi warfa darajatahu fil mahdiyina, wakhlufhu fi akibihi fil ghabirina, waghfir lana walahu ya rabbal aalamina, wafsah lahu fi kabrihi, wanawir lahu fihi.
55. KUMUOMBEA DUA MAITI KATIKA KUMSWALIA
"Tafsiri: Ewe Mwenyezi Mungu, msamehe na umrehemu, na umpe salama na umwachie, na mtukuze katika kushuka kwake, na upanue mahali pake pa kuingia, na muoshe kwa maji na theluji na barafu, na mtakase kutokana na makosa kama inavyotakaswa nguo nyeupe kutokana na uchafu, na mbadilishie nyumba bora kuliko nyumba yake, na jamaa bora kuliko jamaa zake, na mke bora kuliko mke wake, na muingize Peponi, na mkinge mbali na adhabu ya kaburini [na adhabu ya Motoni].199
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ وَارْحَمْهُ، وَعَافِهِ، وَاعْفُ عَنْهُ، وَأَكْرِمْ نُزُلَهُ، وَوَسِّعْ مُدْخَلَهُ، وَاغْسِلْهُ بِالمَاءِ وَالثَّلْجِ وَالبَرَدِ، وَنَقِّهِ مِنَ الخَطَايَا كَمَا نَقَّيْتَ الثَّوْبَ الأَبْيَضَ مِنَ الدَّنَسِ، وَأَبْدِلْهُ دَارًا خَيْرًا مِنْ دَارِهِ، وَأَهْلاً خَيْرًا مِنْ أَهْلِهِ، وَزَوْجًَا خَيًْرا مِنْ زَوْجِهِ، وَأَدْخِلْهُ الجَنَّةَ، وَأَعِذْهُ مِنْ عَذَابِ القَبْرِ [وَعَذَابِ النَّار]).
Allahummaghfir lahu warhamhu, wa aafihi, wa afu anhu, wa akrim nuzulahu, wa wassi mudkhalahu, waghsilhu bil maai wath thalji wal barad, wa nakkihi minal khataya kama nakkayta ath thawbal abyadha minad danas, wa abdilhu daaran khayran min daarihi, wa ahlan khayran min ahlihi, wa zawjan khayran min zawjihi, wa adkhilhul jannah, wa aidh-hu min adhaabil qabri wa adhaabin naar.
"Tafsiri: "Ewe Mwenyezi Mungu, msamehe aliye hai katika sisi na aliyekufa, na aliyepo na asiyekuwepo, na mdogo wetu na mkubwa wetu, na mwanamume kati yetu na mwanamke. Ewe Mwenyezi Mungu, unayemueka hai kati yetu, basi mweke hai katika Uislamu, na uliyemfisha miongoni mwetu, basi mfishe katika Iman. Ewe Mwenyezi Mungu, usitunyime thawabu zake wala usitupoteze baada yake."200
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِحَيِّنَا وَمَيِّتِنَا، وَشَاهِدِنَا وَغَائِبِنَا، وَصَغِيرِنَا وَكَبِيرِنَا، وَذَكَرِنَا وَأُنْثَانَا، اللَّهُمَّ مَنْ أَحْيَيْتَهُ مِنَّا فَأَحْيِهِ عَلَى الإِسْلَامِ، وَمَنْ تَوَفَّيْتَهُ مِنَّا فَتَوَفَّهُ عَلَى الإِيمَانِ، اللَّهُمَّ لَا تَحْرِمْنَا أَجْرَهُ، وَلَا تُضِلَّنَا بَعْدَه).
Allahumma ghfir lihayyina wa mayyitina, wa shahidina wa ghaibina, wa saghirina wa kabirina, wa dhakarina wa unthana. Allahumma man ahyaytahu minna fa ahyihi alal islam, wa man tawaffaytahu minna fa tawaffahu alal iman. Allahumma la tahrimna ajrahu, wala tudhillana baadah.
"Tafsiri: "Ewe Mwenyezi Mungu, hakika fulani bin fulani yumo katika ulinzi wako, na kamba ya hifadhi yako, basi mkinge mbali na fitna ya kaburini, na adhabu ya Motoni, na Wewe ni Mwenye kutimiza ahadi na haki, basi msamehe na umrehemu, hakika Wewe ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu."201
(اللَّهُمَّ إِنَّ فُلَانَ بْنَ فُلَانٍ فِي ذِمَّتِكَ، وَحَبْلِ جِوَارِكَ، فَقِهِ مِنْ فِتْنَةِ القَبْرِ، وَعَذَابِ النَّارِ، وَأَنْتَ أَهْلُ الوَفَاءِ وَالحَقِّ، فَاغْفِرْ لَهُ وَارْحَمْهُ إِنَّكَ أَنْتَ الغَفُورُ الرَّحيم).
Allahumma inna fulana bna fulanin fi dhimmatika, wa habli jiwarika, fakihi min fitnatil kabri, wa adhabin nari, wa anta ahlul wafai wal hakki, faghfir lahu warhamhu innaka antal ghafurur rahim
"Ewe Mwenyezi Mungu, mja wako na mtoto wa mjakazi wako amehitaji rehema zako, na Wewe huna haja ya kumuadhibu. Ikiwa alikuwa mwema, basi mzidishie katika mema yake, na ikiwa alikuwa mkosaji, basi msamehe.”202
(اللَّهُمَّ عَبْدُكَ وَابْنُ أَمَتِكَ احْتَاجَ إِلَى رَحْمَتِكَ، وَأَنْتَ غَنِيٌّ عَنْ عَذَابِهِ، إِنْ كَانَ مُحْسِنًا فَزِدْ فِي حَسَنَاتِهِ، وَإِنْ كَانَ مُسِيئًا فَتَجَاوَزْ عَنْه).
Allahumma abduka wabnu amatika ihtaja ila rahmatika, wa anta ghaniyun an adhabihi. In kana muhsinan, fazid fi hasanatihi, wa in kana musian, fatajawaz anh.
56. KUMUOMBEA DUA MTOTO MDOGO WAKATI WA KUMSWALIA
"Ewe Mwenyezi Mungu, mlinde kutokana na adhabu za kaburi."203
(اللَّهُمَّ أَعِذْهُ مِنْ عَذَابِ القَبْر).
Allahumma a-idh-hu min adhabil kabr
Na akisema: "(Ewe Mwenyezi Mungu, mjaalie kuwa ni mtangulizi na akiba kwa wazazi wake, na mwombezi mwenye kukubaliwa uombezi wake. Ewe Mwenyezi Mungu, kwa ajili yake zifanye nzito mizani za wazazi wake na yafanye malipo yao kuwa mengi, na mkutanishe na wema katika Waumini, na mjaalie awe katika dhamana ya Ibrahim, na umuepushe kwa rehema yako kutokana na adhabu ya Moto, na mbadilishie nyumba bora kuliko nyumba yake, na jamaa bora kuliko jamaa zake. Ewe Mwenyezi Mungu, wasamehe watangulizi wetu, na watoto wetu waliotangulia, na wale waliotutangulia katika Iman)."
((اللَّهُمَّ اجْعَلْهُ فَرَطًا وَذُخْرًا لِوَالِدَيْهِ، وَشَفِيعًا مُجَابًا، اللَّهُمَّ ثَقِّلْ بِهِ مَوَازِينَهُمَا، وَأَعْظِمْ بِهِ أُجورَهُمَا، وَأَلْحِقْهُ بِصَالِحِ المُؤْمِنِينَ، وَاجْعَلْهُ فِي كَفَالَةِ إِبْرَاهِيمَ، وَقِهِ بِرَحْمَتِكَ عَذَابَ الجَحِيمِ، وَأَبْدِلْهُ دَارًا خَيْرًا مِنْ دَارِهِ، وَأَهْلًا خَيْرًا مِنْ أَهْلِهِ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِأَسْلَافِنَا، وَأَفْرَاطِنَا، وَمَنْ سَبَقَنَا بِالإِيمَان).
Allahummaj'alhu faratan wa dhukhran liwalidayh, wa shafi'an mujaba. Allahumma thaqqil bihi mawazinahuma, wa a'dhim bihi ujurahuma, wa alhiqhu bisalihil mu'uminin, waj'alhu fi kafalati Ibrahim, waqihi birahmatika adhabal jahim, wa abdilhu daran khayran min darih, wa ahlan khayran min ahlih. Allahummaghfir liaslafina, wa afratina, waman sabaqana bil iman.
basi ni vyema204.
"Ewe Mwenyezi Mungu umfanye awe mtangulizi kwetu, na akiba, na malipo."205
(اللَّهُمَّ اجْعَلْهُ لَنَا فَرَطًا، وَسَلَفًا، وَأَجْرًا).
Allahumma jalhu lana faratan, wa salafan, wa ajran.
57. DUA YA KUTOA POLE
"Hakika ni cha Mwenyezi Mungu alichokichukua, na ni chake alichokitoa, na kila kitu kwake kina muda maalumu... vuta subira na utaraji malipo."206
(إِنَّ للَّهِ مَا أَخَذَ، وَلَهُ مَا أَعْطَى، وَكُلُّ شَيْءٍ عِنْدَهُ بِأَجَلٍ مُسَمَّى... فَلْتَصْبِرْ وَلْتَحْتَسِب).
Inna lillahi ma akhadha, wa lahu ma a'ata, wa kullu shayin indahu bi ajalin musamma... faltasbir waltahtasib
Na akisema: "(Mwenyezi Mungu akupe malipo makubwa, na akuliwaze vyema, na amsamehe maiti wako)."
(أَعْظَمَ اللَّهُ أَجْرَكَ، وَأَحْسَنَ عَزَاءَكَ، وَغَفَرَ لِمَيِّتِك).
Adhamallahu ajrak, wa ahsana azaak, wa ghafara limayyitik.
basi ni vyema207.
58. DUA WAKATI WA KUMUINGIZA MAITI KABURINI
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu na kulingana na Sunna ya Mtume wa Mwenyezi Mungu."208
(بِسْمِ اللَّهِ وَعَلَى سُنَّةِ رَسُولِ اللَّه).
Bismillahi wa ala sunnati rasulillah
59. DUA BAADA YA KUMZIKA MAITI
"Ewe Mwenyezi Mungu msamehe, ewe Mwenyezi Mungu muimarishe."209
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ، اللَّهُمَّ ثَبِّتْه).
Allahumma ghfir lahu, Allahumma thabbit hu
60. DUA YA KUZURU MAKABURI
"Amani iwe juu yenu, enyi watu wa makazi haya, miongoni mwa Waumini na Waislamu. Nasi Mwenyezi Mungu akipenda, tutakufuateni. [Mwenyezi Mungu awarehemu waliotangulia miongoni mwetu na watakaokuja baada yetu]. Namuomba Mwenyezi Mungu atupe salama sisi na nyinyi."210
(السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ أَهْلَ الدِّيَارِ، مِنَ المُؤْمِنِينَ وَالمُسْلِمِينَ، وَإِنَّا إِنْ شَاءَ اللَّهُ بِكُمْ لَاحِقُونَ، [وَيَرْحَمُ اللَّهُ المُسْتَقدِمِينَ مِنَّا وَالمُسْتأْخِرِينَ] أَسْاَلُ اللَّهَ لَنَا وَلَكُمُ العَافِيَة).
Assalamu alaykum ahlad diyar, minal muuminina wal muslimin, wa inna in shaa Allahu bikum lahikun, wa yarhamullahul mustakdimina minna wal mustakhirin. As-alullaha lana wa lakumul afiya.
61. DUA YA UPEPO MKALI
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba heri zake, na ninajilinda kwako kutokana na shari zake."211
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَهَا، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا).
Allahumma inni as'aluka kheiraha, wa audhu bika min sharriha
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba heri zake, na heri zilizomo ndani yake, na heri za kile ulichotumwa nacho, na ninajilinda kwako kutokana na shari zake, na shari zilizomo ndani yake, na shari za kile ulichotumwa nacho."212
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَهَا، وَخَيْرَ مَا فِيهَا، وَخَيْرَ مَا أُرْسِلَتْ بِهِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا، وَشَرِّ مَا فِيهَا، وَشَرِّ مَا أُرْسِلَتْ بِه).
Allahumma inni as'aluka khairaha, wa khaira ma fiha, wa khaira ma ursilat bihi, wa audhu bika min sharriha, wa sharri ma fiha, wa sharri ma ursilat bih.
62. DUA YA RADI
"Ametakasika yule ambaye radi inamtakasa kwa kumhimidi na Malaika kwa kumuhofu."213
(سُبْحَانَ الَّذِي يُسَبِّحُ الرَّعْدُ بِحَمْدِهِ وَالمَلَائِكَةُ مِنْ خِيفَتِه).
Subhanal ladhi yusabihur raadu bihamdihi, wal malaikatu min khifatih
63. MIONGONI MWA DUA ZA KUOMBA MVUA
"Ewe Mola wetu wa haki tunyeshelezee mvua yenye msaada njema na yenye kubugujika, na iwe yenye kunufaisha na isiwe yenye kudhuru, utunyeshelezee kwa haraka na si kwa kuchelewa."214
(اللَّهُمَّ اسْقِنَا غَيْثًا مُغِيثًا مَرِيئًا مَرِيعًا، نَافِعًا غَيْرَ ضَارٍّ، عَاجِلًا غَيْرَ آجِل).
Allahumma iskina ghaithan mughiithan mariian mariian, naafian ghaira dhaarrin, aajilan ghaira aajil.
"Ewe Mwenyezi Mungu tupe mvua. Ewe Mwenyezi Mungu tupe mvua. Ewe Mwenyezi Mungu tupe mvua."215
(اللَّهُمَّ أَغِثْنَا، اللَّهُمَّ أَغِثْنَا، اللَّهُمَّ أَغِثْنَا).
Allahumma aghithna, Allahumma aghithna, Allahumma aghithna
"Ewe Mola wetu wa haki wanyeshelezee waja wako, na wanyama wako, na eneza rehema zako, na ufufue mji wako uliokufa."216
(اللَّهُمَّ اسْقِ عِبَادَكَ، وَبَهَائِمَكَ، وَانْشُرْ رَحْمَتَكَ، وَأَحْيِي بَلَدَكَ المَيِّت).
Allahumma isqi ibadaka, wa bahaimaka, wanshur rahmataka, wa ahyi baladakal mayyit
64. DUA ANAPOONA MVUA
"Ewe Mwenyezi Mungu ijaalie mvua hiyo kuwa ni yenye manufaa."217
(اللَّهُمَّ صَيِّبًا نَافِعًا).
Allahumma swayyiban naafian
65. DHIKRI BAADA YA KUNYESHA MVUA
"Tumenyeshelezewa kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na rehema zake."218
(مُطِرْنَا بِفَضْلِ اللَّهِ وَرَحْمَتِه).
Mutirna bifadhlillahi wa rahmatih
66. MIONGONI MWA DUA ZA KUOMBA MVUA IKATE
"Ewe Mola tuteremshie mvua pembezoni mwetu na wala usituteremshie juu yetu. Ewe Mola wetu ishushe mvua juu ya miinuko na milimani, na ndani ya mabonde, na maoteo ya miti."219
(اللَّهُمَّ حَوَالَيْنَا وَلَا عَلَيْنَا، اللَّهُمَّ عَلَى الآكَامِ وَالظِّرَابِ، وَبُطُونِ الأَوْدِيَةِ، وَمَنَابِتِ الشَّجَر).
Allahumma hawalayna wala alayna. Allahumma alal akami wadhirabi, wa butunil awdiyati, wa manabitish shajar.
67. DUA YA KUUONA MWEZI
"Maana yake: "Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, ewe Mwenyezi Mungu uandamishe kwetu sisi kwa amani na Imani, na tuwe katika salama na Uislamu, na kuafikishwa kwa yale unayoyapenda Mola wetu Mlezi na kuyaridhia, Mola wetu Mlezi na Mola wako Mlezi ni Mwenyezi Mungu."220
(اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُمَّ أَهِلَّهُ عَلَيْنَا بِالأَمْنِ وَالإِيمَانِ، وَالسَّلَامَةِ وَالإِسْلَامِ، وَالتَّوْفِيقِ لِمَا تُحِبُّ رَبَّنَا وَتَرْضَى، رَبُّنَا وَرَبُّكَ اللَّه).
Allahu akbaru, Allahumma ahillahu alayna bil amni wal iimani, wasalamati wal islami, watawfiqi lima tuhibbu rabbana watardha, rabbuna wa rabbukallah.
68. DUA WAKATI WA KUFUTURU ALIYEFUNGA
"Kiu kimeondoka na mishipa imeloana, na malipo yamethibiti akipenda Mwenyezi Mungu."221
(ذَهَبَ الظَّمَأُ وَابْتَلَّتِ العُرُوقُ، وَثَبَتَ الأَجْرُ إِنْ شَاءَ اللَّه).
Dhahaba adh-dhamau, wabtallatil uruku, wa thabatal ajru, in shaa Allah.
"Tafsiri: Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba kupitia rehema zako zilizoenea kila kitu kwamba unisamehe."222
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ بِرَحْمَتِكَ الَّتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ أَنْ تَغْفِرَ لِي).
Allahumma inni as'aluka, birahmatikallati wasi'at kulla shai'in, an taghfira lii.
69. DUA KABLA YA KULA CHAKULA
"Atakapokula chakula mmoja wenu, basi na aseme:"
Kwa jina la Mwenyezi Mungu,
(بِسْمِ اللَّه).
Bismillah
Basi ikiwa atasahau mwanzoni mwake, basi aseme: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzoni mwake na mwishoni mwake."223
(بِسْمِ اللَّهِ فِي أَوَّلِهِ وَآخِرِه).
Bismillahi fi awwalihi wa akhirih
"Atakayelishwa chakula na Mwenyezi Mungu, basi aseme:"
"Ewe Mwenyezi Mungu tubariki katika hicho, na utulishe kilicho bora kuliko hicho,"
(اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِيهِ وَأَطْعِمْنَا خَيْرًا مِنْه).
Allahumma baarik lana fiihi wa atimna kheiran minh
Na atakayenyweshwa maziwa na Mwenyezi Mungu, basi na aseme: "Ewe Mwenyezi Mungu tubarikie ndani yake na tuzidishie kutoka humo."224
(اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِيهِ وَزِدْنَا مِنْه).
Allahumma baarik lanaa fiihi wa zidnaa minh
70. DUA WAKATI WA KUMALIZA CHAKULA
"Kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyenilisha chakula hiki na akaniruzuku si kwa ujanja wangu wala si kwa nguvu yangu."225
(الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي أَطْعَمَنِي هَذَا، وَرَزَقَنِيهِ، مِنْ غَيْرِ حَوْلٍ مِنِّي وَلَا قُوَّة).
Alhamdu lillahi alladhi at'amani hadha, wa razakanihi, min ghairi haulin minni wala kuwwa
"Yaani: Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, sifa nyingi nzuri zenye baraka ndani yake, asiyekuwa [mwenye kutoshelezwa wala] mwenye kuachwa, wala kutohitajiwa, Mola wetu Mlezi."226
(الْحَمْدُ لِلَّهِ حَمْدًا كَثِيرًا طَيِّبًا مُبَارَكًا فِيهِ، غَيْرَ [مَكْفِيٍّ وَلَا] مُوَدَّعٍ، وَلَا مُسْتَغْنَىً عَنْهُ رَبَّنَا).
Alhamdu lillahi hamdan kathiran tayyiban mubarakan fihi, ghaira makfiyyin wala muwaddain, wala mustaghnan anhu rabbana
71. DUA YA MGENI KWA MWENYEJI ALIYE MKIRIMU CHAKULA
"Ewe Mwenyezi Mungu wabariki katika vile ulivyowaruzuku, na uwasamehe na uwarehemu."227
(اللَّهُمَّ بَارِكْ لَهُمْ فِيمَا رَزَقْتَهُم، وَاغْفِرْ لَهُمْ وَارْحَمْهُم).
Allahumma barik lahum fima razaktahum, waghfir lahum warhamhum.
72. KUDOKEZA KWA DUA ILI KUOMBA CHAKULA AU KINYWAJI
"Yaani: Ewe Mola wangu mlishe aliyenilisha, na mnyweshe aliyeninywesha."228
(اللَّهُمَّ أَطْعِمْ مَنْ أَطْعَمَنِي، وَاسْقِ مَنْ سَقَانِي).
Allahumma at-im man at-amani, waski man sakani
73. DUA YA KUOMBA ENDAPO ATAFUTURU NYUMBANI KWA WATU
"Wamefuturu kwenu wafungaji, na wamekula chakula chenu watu wema, na Malaika wamekuombeeni rehema."229
(أَفْطَرَ عِنْدَكُمُ الصَّائِمُونَ، وَأَكَلَ طَعَامَكُمُ الأَبْرَارُ، وَصَلَّتْ عَلَيْكُمُ المَلَائِكَة).
Aftara indakumus swaaimuun, wa akala taamakumul abraar, wa swallat alaikumul malaaikah.
74. DUA YA MFUNGAJI ANAPOLETEWA CHAKULA NA HAJAFUNGUA
"Atakapoalikwa mmoja wenu, basi aitikie, na ikiwa ni mfungaji, basi aombe dua, na ikiwa amefungua, basi ale."230
Na maana ya 'basi na aswali': Yaaani; basi na aombe dua.
75. ANACHOSEMA MFUNGAJI IKIWA MTU ATAMTUKANA
"Hakika mimi nimefunga, hakika mimi nimefunga."231
76. DUA YA MTU ANAPOONA MATUNDA YA KWANZA
"Ewe Mola wetu wa haki tupe baraka katika matunda yetu, na utupe baraka katika mji wetu, na utupe baraka kwenye vibaba vyetu, na utupe baraka kwenye ratili zetu."232
(اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِي ثَمَرِنَا، وَبَارِكْ لَنَا فِي مَدِينَتِنَا، وَبَارِكْ لَنَا فِي صَاعِنَا، وَبَارِكْ لَنَا فِي مُدِّنَا).
Allahumma baarik lanaa fii thamarinaa, wa baarik lanaa fii madiinatinaa, wa baarik lanaa fii swaainaa, wa baarik lanaa fii muddinaa.
77. DUA YA CHAFYA
"Atakapopiga chafya mmoja wenu, basi na aseme:
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu,
(الحَمْدُ لِلَّه).
Alhamdu lillah
Na ndugu yake aseme kumwambia ndugu yake: Mwenyezi Mungu akurehemu,
(يَرْحَمُكَ اللَّه).
Yarhamukallah
Akisema kumwambia: "Yar-hamukallaah (Akuhurumie Mwenyezi Mungu), basi naye aseme: Mwenyezi Mungu akuongozeni na akutengenezeeni mambo yenu."233
(يَهْدِيكُمُ اللَّهُ وَيُصْلِحُ بَالَكُم).
Yahdikumullahu wa yuslihu balakum
78. ANACHOAMBIWA KAFIRI AKIPIGA CHAFYA NA AKAMHIMIDI MWENYEZI MUNGU
“Mwenyezi Mungu akuongozeni na akutengenezeni mambo yenu.”234
(يَهْدِيكُمُ اللَّهُ وَيُصْلِحُ بَالَكُم).
Yahdikumullahu wa yuslihu baalakum
79. DUA YA KUMUOMBEA ALIYEOA
“Tafsiri: Mwenyezi Mungu akubariki, na atie baraka juu yako, na awakusanye katika kheri."235
(بَارَكَ اللَّهُ لَكَ، وَبَارَكَ عَلَيْكَ، وَجَمَعَ بَيْنَكُمَا فِي خَيْر).
Barakallahu laka, wa baraka alaika, wa jamaa bainakuma fi khair.
80. DUA YA ALIYEOA NA KUNUNUA KIPANDO
Atakapomuoa mmoja wenu mwanamke, au akamnunua mtumishi, basi aseme: "Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakuomba heri zake, na heri za kile ulichomuumba nacho, na ninajilinda kwako kutokana na shari zake, na shari za kile ulichomuumba nacho."
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَهَا، وَخَيْرَ مَا جَبَلْتَهَا عَلَيْهِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا، وَشَرِّ مَا جَبَلْتَهَا عَلَيْه).
Allahumma inni as-aluka kheiraha, wa kheira maa jabaltaha aleyhi, wa audhu bika min sharriha, wa sharri maa jabaltaha aleyh.
"Na akinunua mnyama (au kipando), basi ashike juu ya kilele chake, na aseme hivyo hivyo."236
81. DUA KABLA YA KUMWINGILIA MKE
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu. Ewe Mwenyezi Mungu, tuepushe na shetani, na umwepushe shetani na kile ulichoturuzuku.”237
(بِسْمِ اللَّهِ، اللَّهُمَّ جَنِّبْنَا الشَّيْطَانَ، وَجَنِّبِ الشَّيْطَانَ مَا رَزَقْتَنَا).
Bismillahi. Allahumma jannibnash shaitana, wa jannibish shaitana ma razaktana.
82. DUA YA HASIRA
"Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa."238
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitanir rajiim
83. DUA YA MWENYE KUMUONA MLEMAVU
"Kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliyenipa salama mimi kutokana na hili alilompa mtihani huyu, na akanifanya kuwa bora sana kuliko wengi miongoni mwa wale aliowaumba."239
(الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي عَافَانِي مِمَّا ابْتَلَاكَ بِهِ، وَفَضَّلَنِي عَلَى كَثِيرٍ مِمَّنْ خَلَقَ تَفْضِيلًا).
Alhamdu lillahi alladhi aafani mimmabtalaka bihi, wafadhalani ala kathiirin mimman khalaka tafdhiila.
84. KINACHOSEMWA KATIKA KIKAO
Imesimuliwa kutoka kwa Ibn Umar Mwenyezi Mungu awe radhi naye kwamba alisema: Ilikuwa ikihesabiwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake katika kikao kimoja mara mia kabla ya kusimama: "Ewe Mola wangu Mlezi, nisamehe, na nikubalie toba yangu. Hakika Wewe ni Msamehevu, Mfuta madhambi."240
(رَبِّ اغْفِرْ لِي، وَتُبْ عَلَيَّ، إِنَّكَ أَنْتَ التَّوَّابُ الغَفُور).
Rabbighfir lii, wa tub alayya, innaka anta at-tawwaabul ghafuur
85. KAFARA YA KIKAO
"Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu na sifa njema ni zako. Ninashuhudia kuwa hapana Mola ila Wewe. Ninakuomba msamaha na ninatubia kwako."241
(سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ وَبِحَمْدِكَ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتُوبُ إِلَيْك).
Subhanaka Allahumma wa bihamdika, ash-hadu an la ilaha illa anta, astaghfiruka wa atubu ilaik.
86. KUMUOMBEA DUA ALIYESEMA: GHAFARALLAAHU LAKA (AKUSAMEHE MWENYEZI MUNGU)
"Nawe pia."242
(وَلَك).
Walak
87. DUA KWA ALIYEKUFANYIA WEMA
"Mwenyezi Mungu akuzidishie kheri."243
(جَزَاكَ اللَّهُ خَيْرًا).
Jazaakallahu khairan
88. YALE AMBAYO MWENYEZI MUNGU ANAKINGA KWAYO KUTOKANA NA DAJALI
"Atakayehifadhi aya kumi kuanzia mwanzo wa suratul Kahf, atakingwa kutokana na Dajali."244
Na kujikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na fitina yake baada ya tashahudi ya mwisho ya kila swala245.
89. DUA KWA YULE ANAYESEMA: HAKIKA MIMI NINAKUPENDA KWA AJILI YA MWENYEZI MUNGU
"Akupende yule ambaye umenipenda kwa ajili yake."246
(أَحَبَّكَ الَّذِي أَحْبَبْتَنِي لَه).
Ahabakal ladhi ahbabtani lah
90. DUA YA KUMUOMBEA ALIYEKUPA MALI YAKE
"(Mwenyezi Mungu akubariki katika familia yako na mali yako)."247
(بَارَكَ اللَّهُ لَكَ فِي أَهْلِكَ وَمَالِك).
Barakallahu laka fii ahlika wa maalik
91. DUA KWA ALIYEKUKOPESHA WAKATI WA KULIPA
"Mwenyezi Mungu akubariki katika familia yako na mali yako. Hakika malipo ya mkopo ni sifa njema na kulipa."248
(بَارَكَ اللَّهُ لَكَ فِي أَهْلِكَ وَمَالِك).
Baaraka Allahu laka fii ahlika wa maalik. Innamaa jazaaus-salafi al-hamdu wal-adaa
92. DUA YA KUHOFIA USHIRIKINA
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninajikinga kwako nisije kukushirikisha kwa jambo ninalolijua, na ninakutaka msamaha kwa nisilolijua."249
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ أَنْ أُشْرِكَ بِكَ وَأَنَا أَعْلَمُ، وَأَسْتَغْفِرُكَ لِمَا لَا أَعْلَم).
Allahumma inni audhu bika an ushrika bika wa ana aalam, wa astaghfiruka lima la aalam.
93. DUA YA KUMUOMBEA ALIYESEMA: BAARAKALLAAHU FIIKA (MWENYEZI MUNGU AKUBARIKI)
"Nawe Mwenyezi Mungu akubariki."250
(وَفِيكَ بَارَكَ اللَّه).
Wa fika barakallah
94. DUA YA KUCHUKIA ISHARA MBAYA (MIKOSI)
"(Ewe Mola hakuna mkosi isipokuwa kwa mipango yako, na hakuna kheri isipokuwa kheri yako, na hakuna Mola mwingine zaidi yako)."251
(اللَّهُمَّ لَا طَيْرَ إِلَّا طَيْرُكَ، وَلَا خَيْرَ إِلَّا خَيْرُكَ، وَلَا إِلَهَ غَيْرُك).
Allahumma laa taira illaa tairuka, walaa khaira illaa khairuka, walaa ilaaha ghairuk.
95. DUA YA KUPANDA KIPANDO
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu.
(بِسْمِ اللَّهِ، وَالحَمْدُ للَّه).
Bismillahi, walhamdu lillah
"Ametakasika aliyemfanya huyu atutumikie, na tusingeliweza kufanya haya wenyewe."
(سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِين).
Subhanal ladhi sakhara lana hadha, wama kunna lahu mukrinin.
"Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.",
(وَإِنَّا إِلَى رَبِّنَا لَمُنقَلِبُون).
Wa inna ila rabbina lamunkalibuun
"(Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu basi nisamehe, kwani hakika hakuna ewezaye kusamehe madhambi isipokuwa Wewe)."252.
(الحَمْدُ لِلَّهِ، الحَمْدُ لِلَّهِ، الحَمْدُ لِلَّهِ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي؛ فَإِنَّهُ لَا يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا أَنْت).
Alhamdu lillahi, Alhamdu lillahi, Alhamdu lillahi, Allahu akbaru, Allahu akbaru, Allahu akbaru, Subhanaka Allahumma inni dhalamtu nafsi faghfir li; fa innahu la yaghfiru dhunuba illa anta.
96. DUA YA SAFARI
"Yaani: Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa,
(اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَر).
Allahu akbaru, Allahu akbaru, Allahu akbar
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu aliyetudhalilishia (kipando) hiki, na hatukuwa ni wenye uwezo juu yake.
(سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِين).
Subhaanal ladhii sakhara lanaa haadhaa wamaa kunnaa lahu mukriniin
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi,
(وَإِنَّا إِلَى رَبِّنَا لَمُنقَلِبُون).
Wa inna ila rabbina lamunkalibun
"Ewe Mwenyezi Mungu, hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na ucha Mungu, na katika matendo unayoyaridhia. Ewe Mwenyezi Mungu, turahisishie safari yetu hii na utupunguzie umbali wake. Ewe Mwenyezi Mungu, wewe ndiye mwenza katika safari, na ndiye msimamizi katika familia. Ewe Mwenyezi Mungu, hakika ninajilinda kwako kutokana na uchovu wa safari, na mandhari mabaya, na kurejea kubaya katika mali na familia."
(اللَّهُمَّ إِنّا نَسْأَلُكَ فِي سَفَرِنَا هَذَا البِرَّ وَالتَّقْوَى، وَمِنَ العَمَلِ مَا تَرْضَى، اللَّهُمَّ هَوِّنْ عَلَيْنَا سَفَرَنَا هَذَا وَاطْوِ عَنَّا بُعْدَهُ، اللَّهُمَّ أَنْتَ الصَّاحِبُ فِي السَّفَرِ، وَالخَليفَةُ فِي الأَهْلِ، اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ وَعْثَاءِ السَّفَرِ، وَكَآبَةِ المَنْظَرِ، وَسُوءِ المُنْقَلَبِ فِي المَالِ وَالأَهْل).
Allahumma inna nas-aluka fi safarina hadhal birra wattakwa, waminal amali ma tardha, Allahumma hawwin alaina safarana hadha watwi anna buudahu, Allahumma antas sahibu fis safari, wal khalifatu fil ahli, Allahumma inni audhu bika min watha-is safari, wakaabatil mandhari, wasu-il munkalabi fil mali wal ahl.
Na akirejea atasema maneno hayo, na ataongeza: "Yaani, "Tunarejea, tunatubia, tunamuabudu Mwenyezi Mungu na tunamsifu Mola wetu Mlezi."253
(آيِبُونَ، تائِبُونَ، عَابِدُونَ، لِرَبِّنَا حَامِدُون).
Aayibuna, taaibuna, aabiduna, lirabbina haamidun.
97. DUA YA KUINGIA KIJIJINI AU MJINI
"Ewe Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa mbingu saba na yale ziliyoyatia kivuli, na Mola Mlezi wa ardhi saba na yale ziliyoyabeba, na Mola Mlezi wa mashetani na wale waliowapoteza, na Mola Mlezi wa pepo na yale ziliyoyapeperusha, ninakuomba kheri ya mji huu, na kheri ya watu wake, na kheri ya vilivyomo ndani yake, na ninajikinga kwako kutokana na shari yake, na shari ya watu wake, na shari ya vilivyomo ndani yake."254
(اللَّهُمَّ رَبَّ السَّمَوَاتِ السَّبْعِ وَمَا أَظْلَلْنَ، وَرَبَّ الأَرَضِينَ السَّبْعِ وَمَا أَقْلَلْنَ، وَرَبَّ الشَّياطِينِ وَمَا أَضْلَلْنَ، وَرَبَّ الرِّيَاحِ وَمَا ذَرَيْنَ، أَسْأَلُكَ خَيْرَ هَذِهِ القَرْيَةِ، وَخَيْرَ أَهْلِهَا، وَخَيْرَ مَا فِيهَا، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا، وَشَرِّ أَهْلِهَا، وَشَرِّ مَا فِيهَا).
Allahumma rabbas-samawatis-sab'i wa ma adhlalna, wa rabbal-aradhinas-sab'i wa ma aklalna, wa rabbash-shayatini wa ma adhlalna, wa rabbar-riyahi wa ma dharayna, as'aluka khaira hadhihil-karyati, wa khaira ahliha, wa khaira ma fiha, wa a'udhu bika min sharriha, wa sharri ahliha, wa sharri ma fiha.
98. DUA YA KUINGIA SOKONI
"Tafsiri: 'Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, anahuisha na kufisha, naye ni Hai asiyekufa, mkononi mwake kuna kheri, naye juu ya kila kitu ni Muweza.'"255
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ، وَلَهُ الحَمْدُ، يُحْيِي وَيُمِيتُ، وَهُوَ حَيٌّ لَا يَمُوتُ، بِيَدِهِ الخَيْرُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaaha illallaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku, wa lahul hamdu, yuhyii wa yumiitu, wa huwa hayyun laa yamuutu, biyadihil khayru, wa huwa alaa kulli shay-in kadiir.
99. DUA YA KUOMBA KINAPOCHOKA KIPANDO
"Kwa jina la Mwenyezi Mungu."256
(بِسْمِ اللَّه).
Bismillah
100. DUA YA MSAFIRI KWA MKAZI
"(Nakukabidhini kwa Mwenyezi Mungu ambaye hakipotei alichokabidhiwa kutunza)."257
(أَسْتَوْدِعُكُمُ اللَّهَ الَّذِي لَا تَضِيعُ وَدَائِعُه).
Astaudi'ukumul lahal ladhii laa tadhii'u wadaa'i'uh
101. DUA YA MKAZI KWA MSAFIRI.
"(Ninamkabidhi Mwenyezi Mungu dini yako, na amana yako, na mwisho wa matendo yako)."258
(أَسْتَوْدِعُ اللَّهَ دِينَكَ، وَأَمَانَتَكَ، وَخَوَاتِيمَ عَمَلِك).
Astawdiullaha dinaka, wa amanataka, wa khawatima amalik.
"(Mwenyezi Mungu akupe ucha Mungu, na akusamehe dhambi zako na aifanye kheri kuwa nyepesi kwako mahala popote utakapokuwa)."259
(زَوَّدَكَ اللَّهُ التَّقْوَى، وَغَفَرَ ذَنْبَكَ، وَيَسَّرَ لَكَ الخَيْرَ حَيْثُ ما كُنْت).
Zawwadakallahu attaqwa, wa ghafara dhanbaka, wa yassara lakal khaira haithu ma kunt.
102. TAKBIRI NA TASBIHI KATIKA MWENDO WA SAFARI
Amesema Jabiri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Tulikuwa tukifika kwenye miinuko, tunafanya takbira. Anasema: (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa)
(اللَّهُ أَكْبَر).
Allahu Akbar Na kwenye miteremko tunafanya tas-biihi."260.
Anasema: "Tafsiri: Ametakasika Mwenyezi Mungu"
(سُبْحَانَ اللَّه).
Subhanallah
103. DUA MAOMBI YA MSAFIRI ANAPOINGIA WAKATI WA DAKU
"Asikie msikilizaji sifa njema za Mwenyezi Mungu, na uzuri wa neema zake kwetu. Mola wetu Mlezi, kuwa pamoja nasi, na utufanyie fadhila, ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na moto."261
(سَمَّعَ سَامِعٌ بِحَمْدِ اللَّهِ، وَحُسْنِ بَلَائِهِ عَلَيْنَا، رَبَّنَا صاحِبْنَا، وَأَفْضِلْ عَلَيْنَا، عَائِذًا بِاللَّهِ مِنَ النَّار).
Samma'a saami'un bihamdillahi, wa husni balaaihi alayna, Rabbana saahibna, wa afdhil alayna, aaidhan billahi minan-naar.
104. DUA ANAPOSHUKA MAHALI KATIKA SAFARI AU MAHALI PENGINE POPOTE
“Ninajikinga kwa maneno makamilifu ya Mwenyezi Mungu kutokana na shari ya vile alivyoviumba.”262
(أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَق).
Auudhu bikalimaatil laahit taammaati min sharri maa khalaq
105. DHIKRI YA KUREJEA SAFARINI
"Atatoa takbira tatu juu ya kila mahali palipoinuka kisha atasema:"
"Yaani, "Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake, hana mshirika. Ni wake ufalme, na sifa njema zote ni zake, na Yeye ni Muweza wa kila kitu. Tunarejea, tunatubia, tunafanya ibada, na tunamsifu Mola wetu Mlezi. Mwenyezi Mungu alitimiza ahadi yake, akamnusuru mja wake na akayashinda makundi ya maadui peke yake."263
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ، وَلَهُ الحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، آيِبُونَ، تَائِبُونَ، عَابِدُونَ، لِرَبِّنا حَامِدُونَ، صَدَقَ اللَّهُ وَعْدَهُ، وَنَصَرَ عَبْدَهُ، وَهَزَمَ الأَحْزابَ وَحْدَه).
Laa ilaaha illallaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku, wa lahul hamdu, wa huwa alaa kulli shayin kadiir. Aayibuuna, taaibuuna, aabiduuna, lirabbinaa haamiduuna. , sadakallaahu waadahu, wa nasara abdahu, wa hazamal ahzaaba wahdah.
106. ANACHOTAKIWA KUSEMA LINAYEMJIA JAMBO LINALOMFURAHISHA AU KUMCHUKIZA
Alikuwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- linapomjia jambo la kumfurahisha, anasema: "Kila Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye kwa neema zake hutimia mambo mema."
(الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي بِنِعْمَتِهِ تَتِمُّ الصَّالِحَات).
Alhamdu lillahil ladhi biniimatihi tatimmus swalihat
Na likimjia jambo analolichukia, anasema: "Kila Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu kwa kila hali."264
(الحَمْدُ لِلَّهِ عَلَى كُلِّ حَال).
Alhamdu lillahi ala kulli haal
107. FADHILA ZA KUMSWALIA MTUME REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE
Amesema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "((Mwenye kunitakia rehema mara moja, basi Mwenyezi Mungu humtakia rehema mtu huyo mara kumi kwa sababu ya hilo))."265 kama kusema: (Ewe Mwenyezi Mungu mshushie Nabii wetu Muhammad rehema na amani).
(اللَّهُمَّ صَلِّ وَسَلِّمْ عَلَى نَبِيِّنَا مُحَمَّد).
Allahumma salli wa sallim ala nabiyyina Muhammad
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, na nitakieni rehema, kwani dua zenu hunifikia kutokea popote mlipo."266
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Bahili ni yule ambaye nitatajwa mbele yake, akawa hakuniswalia."267
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Hakika Mwenyezi Mungu ana Malaika wanaozunguka katika ardhi wanaonifikishia salamu kutoka kwa umma wangu.”268
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Hakuna yeyote atakayenisalimia, isipokuwa Mwenyezi Mungu hunirudishia roho yangu ili nimjibu salamu."269
108. KUENEZA SALAMU
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: "Hamtoingia Peponi mpaka muamini, na hamtoamini mpaka mpendane. Je, nisikufahamisheni juu ya jambo ambalo mkilifanya mtapendana? Toleaneni salamu kwa wingi."270
"Mambo matatu atakayeyakusanya, kwa hakika amekusanya Imani: Uadilifu kutoka katika nafsi yako, na kutoa salamu kwa walimwengu kwa wingi, na kutoa katika hali ya ufinyu."271
Na kutoka kwa Abdillahi bin Umar radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, ya kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume rehema na amani zimfikie: Ni Uislamu upi bora? Akasema: "Ulishe chakula, na utoe salamu kwa unayemjua na usiyemjua."272
109. NAMNA YA KUMJIBU SALAMU KAFIRI AKISALIMIA
"Wakikutoleeni salamu Watu wa Kitabu, basi semeni: Na kwenu pia."273"
(وَعَلَيْكُم).
Wa alaikum
110. DUA YA MTU ANAPOSIKIA SAUTI YA JOGOO NA SAUTI YA PUNDA
"Mtakaposikia sauti ya majogoo, basi muombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake; kwani hakika wameona Malaika,"
Kama kusema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba unipe katika fadhila zako"
(اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ مِنْ فَضْلِك).
Allahumma inni as'aluka min fadhlik.
Na mkisikia sauti ya punda, basi jikingeni kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani; kwani hakika yeye amemuona shetani."274 Kama kusema: "Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa."
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitanir rajim
111. DUA WAKATI WA KUSIKIA MBWA WAKIBWEKA USIKU
"Mkisikia kubweka kwa mbwa na sauti za punda usiku, basi jilindeni kwa Mwenyezi Mungu kutokana nazo; kwani hakika wao wanaona yale msiyoyaona."275
kama kusema: Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa.
(أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيم).
Audhu billahi minash shaitwanir rajiim
112. DUA KWA YULE ULIYEMTUKANA
Amesema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Ewe Mwenyezi Mungu, muumini yeyote niliyemtukana, basi lijaalie hilo kwake kuwa ni sadaka kwako siku ya Kiyama.”276
113- ANAYOSEMA MUISLAMU ANAPOMSIFU MUISLAMU
Amesema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: “Ikiwa mmoja wenu atakuwa mwenye kumsifu mwenzake bila ya budi, basi na aseme: Namdhania fulani, na Mwenyezi Mungu ndiye Mhesabu wake, wala simtakasi yeyote mbele ya Mwenyezi Mungu, namdhania – ikiwa anayajua hayo – kuwa ni kadhaa na kadhaa.”277
114- ANACHOSEMA MUISLAMU ANAPOSIFIWA
"Ewe Mwenyezi Mungu usinihukumu kwa yale wanayoyasema, na nisamehe yale wasiyoyajua, [na unifanye mbora kuliko yale wanayoyadhani]."278
(اللَّهُمَّ لَا تُؤَاخِذْنِي بِمَا يَقُولُونَ، وَاغْفِرْ لِي مَا لَا يَعْلَمُونَ، [وَاجْعَلْنِي خَيْرًا مِمَّا يَظُّنُّون] ).
Allahumma la tuakhidhni bima yakuluun, waghfir li ma la yaalamuun, wajalni khairan mimma yadhunnuun
115. NI VIPI ATALETA TALBIYA ALIYE KATIKA IHIRAMU KATIKA HIJA AU UMRA
"(Nimekuitika ewe Mwenyezi Mungu nimekuitikia! Nimekuitikia hauna mshirika nimekuitikia. Hakika sifa njema na neema na ufalme ni vyako, nimekuitikia huna mshirika!)."279
(لَبَّيْكَ اللَّهُمَّ لَبَّيْكَ، لَبَّيْكَ لَا شَرِيكَ لَكَ لَبَّيْكَ، إِنَّ الحَمْدَ، وَالنِّعْمَةَ، لَكَ وَالمُلْكَ، لَا شَرِيكَ لَك).
Labaika Allahumma labaika, labaika laa sharika laka labaika, innal hamda, wan ni'mata, laka wal mulka, laa sharika lak
116. KUTOA TAKBIRA ANAPOLIFIKIA JIWE JEUSI
"Alitufu (akaizunguka) Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, kando ya Al-ka'ba akiwa amepanda juu ya ngamia, kila alipofika katika nguzo (yenye Jiwe Jeusi), aliashiria kwake kwa kitu alichokuwa nacho na akaleta takbira."280.
117. DUA BAINA YA KONA YA YEMEN NA JIWE JEUSI
﴿...رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِي ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٗ وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِ حَسَنَةٗ وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ﴾.
"Mola wetu Mlezi, tupe duniani mema, na Akhera mema, na utulinde kutokana na adhabu ya Moto!"281
(رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِي ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٗ وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِ حَسَنَةٗ وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّار).
Rabbanaa aatinaa fid dunyaa hasanatan, wa fil akhirati hasanatan, wa kinaa adhaaban naar.
118. DUA ANAPOSIMAMA MTU JUU YA SWAFA NA MARWA (KWA WAFANYAO IBADA YA HIJA AU UMRA)
Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alipokaribia Safa, akasoma: "Hakika vilima vya Safaa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu...", ninaanza kwa kile alichoanza nacho Mwenyezi Mungu."
(إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِنْ شَعَآئِرِ اللَّهِ...، أَبْدَأُ بِمَا بَدَأَ اللَّهُ بِه).
Innas safaa wal marwata min sha-aa-iril lahi... abda-u bimaa bada-al lahu bih
Akaanza kwa Safa, akapanda juu yake mpaka akaiona Al-Ka'aba, akaelekea kibla, akampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtukuza, na akasema: "Yaani: Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, naye ni Muweza wa kila kitu. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee. Alitimiza ahadi yake, na akamnusuru mja wake, na akayashinda makundi ya maadui peke yake,"
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ، أَنْجَزَ وَعْدَهُ، وَنَصَرَ عَبْدَهُ، وَهَزَمَ الأَحْزَابَ وَحْدَه).
La ilaha illallahu wahdahu la sharika lahu, lahul mulku wa lahul hamdu wa huwa ala kulli shay in kadir, la ilaha illallahu wahdahu, anjaza wadahu, wa nasara abdahu, wa hazamal ahzaba wahdah.
Kisha akaomba dua baina ya hayo, akasema mfano wa haya mara tatu." Hadithi. Na imekuja ndani yake: Akafanya juu ya Marwa kama alivyofanya juu ya Safa282.
119. DUA YA SIKU YA ARAFA
Amesema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Dua bora ni dua ya siku ya Arafa. Na kitu bora nilichosema mimi na Manabii waliotangulia kabla yangu ni:" "Tafsiri: 'Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema zote ni zake, naye ni Muweza mno wa kila kitu.'"283
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaha illallahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku walahul hamdu wahuwa ala kulli shai-in kadiir. "Alipanda Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, Al-Qaswaa mpaka akafika Al-Mash'ar Al-Haram, akaelekea kibla (akamuomba Mwenyezi Mungu, akapiga takbira, akaleta tahlili, na akampwekesha), akaendelea kusimama mpaka kulipopambazuka sana, akaondoka kabla ya jua kuchomoza."284 "Atatoa takbira kila anaporusha kijiwe kwenye Jamarati tatu, kisha atasogea mbele, na atasimama akiomba dua akiwa kaelekea kibla, huku akiwa kanyanyua mikono yake baada ya Jamarati ya kwanza na ya pili. Ama Jamaratul-Aqaba, ataitupia na atatoa takbira kwenye kila kijiwe na ataondoka, na wala hatosimama hapo."285
120. DHIKIRI YA MTU ANAPOKUWA MUZDALIFA (SEHEMU INAYOFUATA BAADA YA KUTOKA ARAFA)
121. KUPIGA TAKBIRI WAKATI WA KUTUPA VIJIWE KWENYE JAMARAAT PAMOJA NA KILA KIJIWE
122. DUA YA KUSTAAJABU NA JAMBO LA KUFURAHISHA
"(Ametakasika Mwenyezi Mungu)!"286
(سُبْحَانَ اللَّه).
Subhanallah
"Yaani: Mwenyezi Mungu ni Mkubwa."287
(اللَّهُ أَكْبَر).
Allahu Akbar
123. ANACHOTAKIWA KUKIFANYA LINAYEMJIA JAMBO LINALOMFURAHISHA
"Alikuwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- linapomjia jambo la kumfurahisha au anapofurahishwa nalo, huporomoka kwa kusujudu kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetukuka."288
124. ANACHOTAKIWA KUKIFANYA NA KUSEMA ANAYEHISI MAUMIVU KATIKA MWILI WAKE
“Weka mkono wako juu ya mahala panapoumia katika mwili wako, na useme:"
Kwa jina la Mwenyezi Mungu,
(بِسْمِ اللَّه).
Bismillah
Mara tatu, Na useme mara saba: “Ninajikinga kwa Mwenyezi Mungu na uwezo wake kutokana na shari ya ninachokipata na kukihofia.”289
(أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِر).
Audhu billahi wa kudratihi min sharri ma ajidu wa uhadhir
125. DUA YA MWENYE KUHOFIA KUKITIA KITU KIJICHO
"Atakapoona mmoja wenu kwa ndugu yake au kwake mwenyewe, au katika mali yake chenye kumstaajabisha, [basi na akiombee baraka] kwani kijicho ni kweli (kipo)."290
126. KINACHOSEMWA WAKATI WA HOFU KUBWA
"Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu!"291
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّه).
La ilaha illallah
127. ANACHOSEMA WAKATI WA KUCHINJA AU KUDUNGA KOONI
"(Ninaanza kwa jina la Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. [Ewe Mola inatoka kwako na ni kwa ajili yako]. Ewe Mola nipokelee)."292
(بِسْمِ اللَّهِ وَاللَّهُ أَكْبَرُ [اللَّهُمَّ مِنْكَ وَلَكَ] اللَّهُمَّ تَقَبَّلْ مِنِّي).
Bismillahi Wallahu Akbar, Allahumma minka walaka, Allahumma taqabbal minni.
128. ANACHOSEMA ILI KUZUIA VITIMBI VYA MASHETANI WAASI
“Ninajikinga kwa maneno makamilifu ya Mwenyezi Mungu, ambayo mwema wala muovu hawezi kuyavuka: kutokana na uovu wa alichokiumba, kukianzisha na kukieneza, na kutokana na uovu wa kile kinachoteremka kutoka mbinguni, na kutokana na uovu wa kile kinachopanda ndani yake, na kutokana na uovu wa alichokieneza katika ardhi, na kutokana na uovu wa yale yanayotoka humo, na kutokana na uovu wa majaribu ya usiku na mchana, na kutokana na uovu wa kijacho usiku, isipokuwa kijacho usiku kwa uzuri, ewe Mwingi wa rehema.”293
(أَعُوذُ بكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ الَّتِي لَا يُجَاوِزُهُنَّ بَرٌّ وَلَا فَاجِرٌ: مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ، وَبَرَأَ وَذَرَأَ، وَمِنْ شَرِّ مَا يَنْزِلُ مِنَ السَّمَاءِ، وَمِنْ شَرِّ مَا يَعْرُجُ فيهَا، وَمِنْ شَرِّ مَا ذَرَأَ فِي الأَرْضِ، وَمِنْ شَرِّ مَا يَخْرُجُ مِنْهَا، وَمِنْ شَرِّ فِتَنِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ، وَمِنْ شَرِّ كُلِّ طَارِقٍ إِلَّا طَارِقًا يَطْرُقُ بِخَيْرٍ يَا رَحْمَن).
Audhu bi kalimaatillahi taamaati allati laa yujawizuhunna barrun wa laa faajir: min sharri maa khalaka, wa baraa wa dharaa, wa min sharri maa yanzilu minas samaai, wa min sharri maa yaaruju fiihaa, wa min sharri maa dharaa fil ardhi, wa min sharri maa yakhruju minhaa, wa min sharri fitanil layli wan nahaari, wa min sharri kulli taarikin illaa taarikan yatruku bi khayrin yaa rahmaan.
129. KUOMBA MSAMAHA NA KUTUBIA
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: "Wallahi (Namuapa Mwenyezi Mungu) hakika mimi ninamuomba msamaha Mwenyezi Mungu na ninatubia kwake ndani ya siku moja zaidi ya mara sabini."294
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Enyi watu, tubieni kwa Mwenyezi Mungu, kwani mimi kwa hakika ninatubia kwake kwa siku mara mia moja."295
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayesema: 'Ninaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu Mkuu ambaye hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Yeye aliye Hai na Mwenye kusimamia mambo yote milele na ninatubia kwake',
(أَسْتَغْفِرُ اللَّهَ العَظيمَ الَّذِي لَا إِلَهَ إِلَّا هُوَ الحَيُّ القَيُّوُمُ وَأَتُوبُ إِلَيه).
Astaghfirullahal adhima, alladhi laa ilaha illaa huwa, al hayyul kayyumu, wa atuubu ilaihi.
Mwenyezi Mungu atamsamehe hata kama alikimbia kutoka katika safu za vita vya kidini."296.
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Mahala pa karibu zaidi anapokuwa Mola Mlezi na mja ni ndani ya masaa ya mwisho ya usiku. Ikiwa utaweza kuwa miongoni mwa wanaomtaja Mwenyezi Mungu katika wakati huo, basi fanya."297
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Mahala anapokuwa karibu zaidi mja na Mola wake Mlezi ni pale anapokuwa kasujudu, basi zidisheni dua."298
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Hakika moyo wangu hufunikwa, na hakika mimi ninamuomba msamaha Mwenyezi Mungu kwa siku mara mia moja."299
130. FADHILA ZA KUSEMA SUB-HAANALLAAH, NA ALHAMDULILLAAH, NA LAA ILAAHA ILLA LLAAH, NA ALLAAHU AKBAR
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayesema: 'Utakasifu ni wa Mwenyezi Mungu na sifa njema ni zake'
(سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِه).
Subhaanallahi wa bihamdih
kwa siku mara mia moja, atasamehewa makosa yake hata kama yatakuwa mfano wa povu la bahari."300
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayesema: "Tafsiri yake: Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake asiye na mshirika, ufalme ni wake na sifa njema ni zake, naye juu ya kila kitu ni Muweza."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ، وَلَهُ الحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِير).
Laa ilaha illallahu wahdahu laa sharika lahu, lahul mulku, wa lahul hamdu, wa huwa ala kulli shayin kadiir.
mara kumi (10), atakuwa ni kama aliyewaacha huru watu wanne katika wana wa Ismail."301
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Maneno mawili ni mepesi sana katika ulimi, ni mazito sana katika mizani, yanapendeka sana kwa Ar-Rahmani (Mwingi wa rehema): "(Utakasifu ni wa Mwenyezi Mungu na sifa ni zake. Utakasifu ni wa Mwenyezi Mungu Mkuu)."302
(سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ، سُبْحانَ اللَّهِ العَظِيم).
Subhanallahi wa bihamdihi, Subhanallahil adhiim.
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Kwa hakika kusema kwangu: Tafsiri: 'Ametakasika Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, na hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa.'
(سُبْحَانَ اللَّهِ، وَالحَمْدُ لِلَّهِ، وَلَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَر).
Subhanallah, Walhamdu lillah, Wa la ilaha illallah, Wallahu akbar.
kunapendeka zaidi kwangu kuliko vyote vilivyochomozewa na jua."303
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Je, anashindwa mmoja wenu kuchuma kila siku mema elfu moja?" Akamuuliza muulizaji miongoni mwa waliokuwa naye kwenye kikao: "Vipi anaweza kuchuma mmoja wetu mema elfu moja?" Akasema: "Atasema: Sub-haana llahi (ametakasika Mwenyezi Mungu) mara mia moja (100), kisha ataandikiwa mema elfu (1000), au atafutiwa makosa elfu moja (1000)."304
(سُبْحَانَ اللَّه).
Subhanallah
"Atakayesema:
'Utakasifu ni wa Mwenyezi Mungu Mkuu na sifa ni zake'
(سُبْحَانَ اللَّهِ العَظِيمِ وَبِحَمْدِه).
Subhanallahil adhimi wa bihamdih
ataoteshewa mti wa mtende Peponi."305
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Ewe Abdallah bin Kais, hivi nikujulishe hazina miongoni mwa hazina za Pepo?" Nikasema: Ndivyo, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: "Sema: (Hakuna uwezo wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu)."306
(لَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّه).
Laa haula walaa kuwwata illaa billaah
Na amesema rehema na amani ziwe juu yake: "Maneno yanayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni manne:" Tafsiri: Ametakasika Mwenyezi Mungu, na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, na hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa.
(سُبْحَانَ اللَّهِ، وَالحَمْدُ لِلَّهِ، وَلَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَر).
Subhanallah, Walhamdu lillah, Wala ilaha illallah, Wallahu akbar.
"Haikudhuru kwa lolote kati ya hayo utakaloanza nalo."307
Alikuja bedui mmoja kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake na akasema: Nifundishe maneno nitakayoyasema. Akasema: "Sema: "Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu Yeye pekee asiyekuwa na mshirika, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa mno, na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu kwa wingi, na ametakasika Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu, na hapana ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima."
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيرًا، وَالحَمْدُ لِلَّهِ كَثِيرًا، سُبْحَانَ اللَّهِ رَبِّ العَالَمِينَ، لَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّهِ العَزِيزِ الحَكِيم).
La ilaha illallahu wahdahu la sharika lahu, Allahu akbaru kabira, walhamdu lillahi kathira, subhanallahi rabbil alamin, la hawla wala quwwata illa billahil azizil hakim.
Akasema: Basi haya ni ya Mola wangu Mlezi, basi mimi nina nini? Akasema: "Sema: "Yaani: Ewe Mola wangu nisamehe, na unihurumie, na uniongoze, na uniruzuku."308
(اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَارْزُقْنِي).
Allahummaghfir li, warhamni, wahdini, warzukni
Alikuwa mtu akisilimu, Mtume rehema na amani ziwe juu yake anamfundisha swala, kisha anamuamrisha aombe kwa maneno haya: "Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe, na unihurumie, na uniongoze, na unipe salama, na uniruzuku."309
(اللَّهُمَّ اغْفِرِ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَعَافِنِي وَارْزُقْنِي).
Allahuma ghifir lii, warhamnii, wahdinii, wa afinii warzuknii.
"Hakika dua bora ni:
'Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu',
(الحَمْدُ لِلَّه).
Alhamdu lillah
Na dhikiri bora ni 'Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu.'"310
(لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّه).
Laa ilaha illallah
"Matendo mema yenye kudumu ni:
"(Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu)."311
(سُبْحَانَ اللَّهِ، وَالحَمْدُ لِلَّهِ، وَلَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ، وَلَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّه).
Subhanallah, walhamdu lillah, wa la ilaha illallah, wallahu akbar, wa la haula wa la kuwwata illa billah.
131. NI VIPI ALIKUWA MTUME REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE AKIMTAKASA MWENYEZI MUNGU?
Imesimuliwa kutoka kwa Abdallah bin Amri -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kwamba alisema: "Nilimuona Mtume rehema na amani ziwe juu yake akihesabu tasbihi" na katika ziada: "kwa mkono wake wa kulia."312.
132- MIONGONI MWA AINA ZA KHERI NA ADABU (HESHIMA) ZINAZOKUSANYA
Amesema Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Pindi unapoingia mwanzo wa giza la usiku – au mnapoingia jioni – basi wazuieni watoto wenu, kwa sababu mashetani huenea wakati huo, na ukipita muda katika usiku, basi waacheni, na fungeni milango na mtaje jina la Mwenyezi Mungu; kwani hakika Shetani hafungui mlango uliofungwa, na fungeni viriba vyenu, na mtaje jina la Mwenyezi Mungu, na funikeni vyombo vyenu, na mtaje jina la Mwenyezi Mungu, hata kama ni kwa kuweka kitu juu yake, na zimeni taa zenu."313
Na rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad na ahali zake na Maswahaba zake.
***
Yaliyomo
Utangulizi 2
Ubora wa kumtaja Mwenyezi Mungu (dhikiri) 5
1. NYIRADI ZA KUAMKA KUTOKA USINGIZINI 9
2. DUA YA KUVAA NGUO 14
3. DUA YA KUVAA NGUO MPYA 15
4. DUA YA KUMUOMBEA ALIYEVAA NGUO MPYA 15
5. ANACHOSEMA ANAPOVUA NGUO YAKE 16
6. DUA YA KUINGIA CHOONI 16
7. DUA YA KUTOKA CHOONI 17
8. DUA KABLA YA UDHU 17
9. DHIKIRI BAADA YA KUMALIZA UDHU 17
10. DHIKIRI WAKATI WA KUTOKA NYUMBANI 18
11. DHIKIRI WAKATI WA KUINGIA NYUMBANI 19
12. DUA YA KWENDA MSIKITINI 20
13. DUA YA KUINGIA MSIKITINI 22
14. DUA YA KUTOKA MSIKITINI 23
15. DHIKIRI ZA ADHANA 24
16. DUA YA UFUNGUZI WA SWALA 26
17. DUA YA RUKUU 34
18. DUA YA KUNYANYUKA KUTOKA KATIKA RUKUU 36
19. DUA NDANI YA SIJIDA 37
20. DUA YA KIKAO KATI YA SIJIDA MBILI 40
21. DUA YA SIJIDA YA KISOMO 41
22. TASHAHHUD 42
23. KUMTAKIA REHEMA MTUME, REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE, BAADA YA TAHIYATU 43
24. DUA YA BAADA YA TASHAHHUD YA MWISHO KABLA YA KUTOA SALAMU 45
25. DHIKIRI BAADA YA SALAMU YA KUMALIZA SWALA 52
26. DUA YA SWALA YA KUOMBA UCHAGUZI (ISTIKHARA) 59
27. NYIRADI ZA ASUBUHI NA JIONI 62
28. NYIRADI ZA KULALA 83
29. DUA WAKATI UNAPOGEUKA USIKU 93
30. DUA YA MFADHAIKO USINGIZINI, NA MWENYE KUPATA MTIHANI WA KUHISI UPWEKE 94
31. ANACHOTAKIWA KUFANYA MWENYE KUOTA NDOTO MBAYA 94
32. MAOMBI YA KUNUTI YA WITIRI 95
33. DHIKIRI BAADA YA SALAMU YA KUMALIZA WITIRI 98
34. DUA YA WASIWASI NA HUZUNI 98
35. DUA WAKATI WA MATATIZO 100
36. DUA YA KUKUTANA NA ADUI NA MWENYE MAMLAKA 102
37. MAOMBI YA MWENYE KUOGOPA DHULMA YA MTAWALA 103
38. DUA DHIDI YA ADUI 105
39. ANAYOTAKIWA KUSEMA MWENYE KUWAOGOPA WATU 106
40. DUA YA MTU ALIYEPATWA NA WASIWASI KATIKA IMANI 106
41. DUA YA KULIPA DENI 107
42. DUA YA MTU ANAPOPATWA NA WASIWASI KATIKA SWALA NA KISOMO 108
43. DUA YA LITAKAYEKUWA JAMBO GUMU KWAKE 108
44. ANACHOSEMA NA KUFANYA ATAKAYEFANYA DHAMBI 109
45. DUA YA KUMFUKUZA SHETANI NA WASIWASI WAKE 109
46. KUOMBA PINDI LINAPOTOKEA JAMBO ASILOLIPENDA AU AKASHINDWA NA JAMBO LAKE 111
47. Pongezi kwa aliye ruzukiwa mtoto na majibu yake. 111
48. MANENO YA KUWAKINGA WATOTO 112
49. DUA YA KUMUOMBEA MGONJWA WAKATI WA KUMTEMBELEA 113
50. FADHILA ZA KUMTEMBELEA MGONJWA 114
51. MAOMBI YA MGONJWA AMBAYE AMEKATA TAMAA YA MAISHA YAKE 114
52. KUMTAMKISHA SHAHADA MTU ANAYEKARIBIA KUFA 116
53. DUA YA MWENYE KUPATWA NA MSIBA 116
54. DUA WAKATI WA KUMFUMBA MACHO MAITI 117
55. KUMUOMBEA DUA MAITI KATIKA KUMSWALIA 117
56. KUMUOMBEA DUA MTOTO MDOGO WAKATI WA KUMSWALIA 121
57. DUA YA KUTOA POLE 123
58. DUA WAKATI WA KUMUINGIZA MAITI KABURINI 124
59. DUA BAADA YA KUMZIKA MAITI 124
60. DUA YA KUZURU MAKABURI 124
61. DUA YA UPEPO MKALI 125
62. DUA YA RADI 126
63. MIONGONI MWA DUA ZA KUOMBA MVUA 126
64. DUA ANAPOONA MVUA 128
65. DHIKRI BAADA YA KUNYESHA MVUA 128
66. MIONGONI MWA DUA ZA KUOMBA MVUA IKATE 128
67. DUA YA KUUONA MWEZI 129
68. DUA WAKATI WA KUFUTURU ALIYEFUNGA 129
69. DUA KABLA YA KULA CHAKULA 130
70. DUA WAKATI WA KUMALIZA CHAKULA 131
71. DUA YA MGENI KWA MWENYEJI ALIYE MKIRIMU CHAKULA 132
72. KUDOKEZA KWA DUA ILI KUOMBA CHAKULA AU KINYWAJI 133
73. DUA YA KUOMBA ENDAPO ATAFUTURU NYUMBANI KWA WATU 133
74. DUA YA MFUNGAJI ANAPOLETEWA CHAKULA NA HAJAFUNGUA 133
75. ANACHOSEMA MFUNGAJI IKIWA MTU ATAMTUKANA 134
76. DUA YA MTU ANAPOONA MATUNDA YA KWANZA 134
77. DUA YA CHAFYA 135
78. ANACHOAMBIWA KAFIRI AKIPIGA CHAFYA NA AKAMHIMIDI MWENYEZI MUNGU 135
79. DUA YA KUMUOMBEA ALIYEOA 136
80. DUA YA ALIYEOA NA KUNUNUA KIPANDO 136
81. DUA KABLA YA KUMWINGILIA MKE 137
82. DUA YA HASIRA 137
83. DUA YA MWENYE KUMUONA MLEMAVU 138
84. KINACHOSEMWA KATIKA KIKAO 138
85. KAFARA YA KIKAO 139
86. KUMUOMBEA DUA ALIYESEMA: GHAFARALLAAHU LAKA (AKUSAMEHE MWENYEZI MUNGU) 139
87. DUA KWA ALIYEKUFANYIA WEMA 140
88. YALE AMBAYO MWENYEZI MUNGU ANAKINGA KWAYO KUTOKANA NA DAJALI 140
89. DUA KWA YULE ANAYESEMA: HAKIKA MIMI NINAKUPENDA KWA AJILI YA MWENYEZI MUNGU 140
90. DUA YA KUMUOMBEA ALIYEKUPA MALI YAKE 141
91. DUA KWA ALIYEKUKOPESHA WAKATI WA KULIPA 141
92. DUA YA KUHOFIA USHIRIKINA 142
93. DUA YA KUMUOMBEA ALIYESEMA: BAARAKALLAAHU FIIKA (MWENYEZI MUNGU AKUBARIKI) 142
94. DUA YA KUCHUKIA ISHARA MBAYA (MIKOSI) 142
95. DUA YA KUPANDA KIPANDO 143
96. DUA YA SAFARI 145
97. DUA YA KUINGIA KIJIJINI AU MJINI 146
98. DUA YA KUINGIA SOKONI 148
99. DUA YA KUOMBA KINAPOCHOKA KIPANDO 148
100. DUA YA MSAFIRI KWA MKAZI 148
101. DUA YA MKAZI KWA MSAFIRI. 149
102. TAKBIRI NA TASBIHI KATIKA MWENDO WA SAFARI 150
103. DUA MAOMBI YA MSAFIRI ANAPOINGIA WAKATI WA DAKU 150
104. DUA ANAPOSHUKA MAHALI KATIKA SAFARI AU MAHALI PENGINE POPOTE 151
105. DHIKRI YA KUREJEA SAFARINI 151
106. ANACHOTAKIWA KUSEMA LINAYEMJIA JAMBO LINALOMFURAHISHA AU KUMCHUKIZA 152
107. FADHILA ZA KUMSWALIA MTUME REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE 153
108. KUENEZA SALAMU 154
109. NAMNA YA KUMJIBU SALAMU KAFIRI AKISALIMIA 155
110. DUA YA MTU ANAPOSIKIA SAUTI YA JOGOO NA SAUTI YA PUNDA 155
111. DUA WAKATI WA KUSIKIA MBWA WAKIBWEKA USIKU 156
112. DUA KWA YULE ULIYEMTUKANA 157
113- ANAYOSEMA MUISLAMU ANAPOMSIFU MUISLAMU 157
114- ANACHOSEMA MUISLAMU ANAPOSIFIWA 158
115. NI VIPI ATALETA TALBIYA ALIYE KATIKA IHIRAMU KATIKA HIJA AU UMRA 158
116. KUTOA TAKBIRA ANAPOLIFIKIA JIWE JEUSI 159
117. DUA BAINA YA KONA YA YEMEN NA JIWE JEUSI 159
118. DUA ANAPOSIMAMA MTU JUU YA SWAFA NA MARWA (KWA WAFANYAO IBADA YA HIJA AU UMRA) 160
119. DUA YA SIKU YA ARAFA 161
120. DHIKIRI YA MTU ANAPOKUWA MUZDALIFA (SEHEMU INAYOFUATA BAADA YA KUTOKA ARAFA) 163
121. KUPIGA TAKBIRI WAKATI WA KUTUPA VIJIWE KWENYE JAMARAAT PAMOJA NA KILA KIJIWE 163
122. DUA YA KUSTAAJABU NA JAMBO LA KUFURAHISHA 163
123. ANACHOTAKIWA KUKIFANYA LINAYEMJIA JAMBO LINALOMFURAHISHA 163
124. ANACHOTAKIWA KUKIFANYA NA KUSEMA ANAYEHISI MAUMIVU KATIKA MWILI WAKE 164
125. DUA YA MWENYE KUHOFIA KUKITIA KITU KIJICHO 164
126. KINACHOSEMWA WAKATI WA HOFU KUBWA 165
127. ANACHOSEMA WAKATI WA KUCHINJA AU KUDUNGA KOONI 165
128. ANACHOSEMA ILI KUZUIA VITIMBI VYA MASHETANI WAASI 166
129. KUOMBA MSAMAHA NA KUTUBIA 167
130. FADHILA ZA KUSEMA SUB-HAANALLAAH, NA ALHAMDULILLAAH, NA LAA ILAAHA ILLA LLAAH, NA ALLAAHU AKBAR 169
131. NI VIPI ALIKUWA MTUME REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE AKIMTAKASA MWENYEZI MUNGU? 176
132- MIONGONI MWA AINA ZA KHERI NA ADABU (HESHIMA) ZINAZOKUSANYA 176
***
sw24v5.0 - 07/09/2026
Surat Al-Baqarah: 152.
Suratul Ahzaab: 41.
Suratul Ahzaab: 35.
Suratul-Al-Araaf: 205.
Al-Bukhari pamoja na Al-Fat-h, 11/208, nambari 6407, na Muslim, 1/539, nambari 779, kwa matamshi haya: "Mfano wa nyumba ambayo Mwenyezi Mungu anatajwa ndani yake, na nyumba ambayo Mwenyezi Mungu hatajwi ndani yake ni mfano wa aliye hai na maiti", 1/539.
At-Tirmidhi, 5/459, kwa nambari 3377, na Ibn Majah, 2/124, kwa nambari 3790. Tazama: "Sahih Ibn Majah", 2/316, na "Sahih At-Tirmidhi", 3/139.
Bukhari 8/171 kwa nambari 7405, na Muslim 4/2061 kwa nambari 2675, na tamko hili ni la Bukhari.
At-Tirmidhiy, 5/458, nambari 3375, na Ibn Majah, 2/1246, nambari 3793. Al-Albani alisema kwamba ni hadithi sahihi katika Sahih At-Tirmidhiy, 3/139, na Sahih Ibn Majah, 2/317.
At-Tirmidhiy, 5/75, nambari 2910, na Al-Albani alisema kwamba ni hadithi sahihi katika Sahih At-Tirmidhi, 3/9, na Sahih Al-Jami’ As-Swaghiir, 5/340.
Muslim 1/553 namba 803.
Abu Daud 4/264 kwa nambari 4856, na wengineo, na tazama: "Sahih Al-Jami'" 5/342.
At-Tirmidhi 5/461 namba 3380, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi" 3/140.
Abu Daud 4/264 kwa nambari 4855, na Ahmad 2/389 kwa nambari 10680 na tazama: "Sahih Al-Jami’i" 5/176.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/113, namba 6314, na Muslim, 4/2083, namba 2711.
"Atakayesema hayo, atasamehewa, na kama ataomba, atajibiwa, na kama atasimama akatawadha kisha akasali itakubaliwa sala yake." Ameipokea Al-Bukhari pamoja na Al-Fath 3/39 kwa nambari 1154 na wengineo, na tamko hili ni la Ibn Majah, tazama: Sahih Ibn Majah 2/335.
At-Tirmidhiy 5/473 kwa namba 3401, na tazama: Sahih At-Tirmidhiy 3/144.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 8/337 namba 4569, na Muslim 1/530 namba 256.
Imepokelewa na Ahlus-Sunan isipokuwa An-Nasaai: Abuu Daud kwa nambari 4023, na At-Tirmidhiy kwa nambari 3458, na Ibn Maajah kwa nambari 3285, na Albaani alisema kwamba ni hadithi nzuri (Hasan) katika: Irwaaul-Ghaliil 47/7.
Abu Daud kwa nambari 4020, na At-Tirmidhiy kwa nambari 1767, na Al-Baghawiy 12/40, na tazama: "Mukhtasar Shamail At-Tirmidhiy" cha Al-Albaaniy uk. 47.
Imepokelewa na Abu Daawuud 4/41, nambari 4020, na tazama: Sahihi Abu Daawuud 2/760.
Ibn Majah 2/1178 kwa nambari 3558, na Al-Baghawiy 41/12, na tazama: Sahih Ibn Majah 275/2.
At-Tirmidhi 2/505 nambari 606, na wengineo, na tazama: Ir'waail Ghaliil nambari 50, na Sahih Al-Jaami' 3/203.
Imepokelewa na Bukhari 1/45, nambari 142, na Muslim 1/283, nambari 375, na ziada ya: 'Bismillaah' mwanzoni mwake imepokelewa na Said bin Mansur. Tazama Fathul Bari 1/244.
Imepokelewa na As-haabus-Sunan isipokuwa An-Nasaai, ambaye ameitoa katika kitabu "Amalul-Yaum wal-Lailah" kwa nambari 79, Abuu Daud kwa nambari 30, na At-Tirmidhiy kwa nambari 7, na Ibn Majah kwa nambari 300, na Al-Albaani amesema kwamba ni sahihi katika Sahihi Sunan Abuu Daud 1/19.
Abu Daud kwa nambari 101, na Ibn Majah kwa nambari 397, na Ahmad kwa nambari 9418, na tazama "Irwa’ Al-Ghaliil" 1/122.
Muslim 1/209 namba 234.
At-Tirmidhi 1/78 kwa nambari 55, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 1/18.
An-Nnasaai katika Amali Al-Yaumi wa Al-Lailah uk. 173, na tazama: Irwaau Al-Ghaliyl 1/135 na 3/94.
Abu Daud 4/325 namba 5095, na At-Tirmidhi 5/490 namba 3426, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 3/151.
Wenye Sunan: Abu Daud kwa nambari 5094, na Tirmidhiy kwa nambari 3427, na Nasaai kwa nambari 5501, na Ibn Majah kwa nambari 3884, na tazama: "Sahih At-Tirmidhiy" 3/152, na "Sahih Ibn Majah" 2/336.
Ameipokea Abu Dawud 4/325 kwa nambari 5096, na msururu wa wapokezi wake umepewa daraja ya Hasan na Mwanachuoni Ibn Baz katika Tuhfatul Akhyar uk. 28, na katika Sahihi: "Anapoingia mtu nyumbani kwake na akamtaja Mwenyezi Mungu wakati wa kuingia kwake na wakati wa chakula chake, Shetani husema: Hakuna malazi kwenu, wala chakula cha usiku", Muslim kwa nambari 2018.
Tazama matamko haya yote katika Bukhari 11/116 nambari 3166, na Muslim 1/526 nambari 529 na 530 na 763.
At-Tirmidhiy 5/483 nambari 3419.
Ameipokea Bukhari katika Adabu Al-Mufrad kwa nambari 695 uk. 258, na ameisahihisha isnaad yake Albaani katika Sahih Adabu Al-Mufrad kwa nambari 536.
Ameitaja Ibn Hajar katika Fath Al-Baariy, na akainasibisha kwa Ibn Abi Aaswym katika kitabu cha Dua, tazama Al-Fath 11/118 na akasema: Basi zikakusanyika kutokana na tofauti za mapokezi sifa ishirini na tano.
Kwa kauli ya Anas bin Maalik radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Ni katika Sunna utakapoingia msikitini uanze na mguu wako wa kulia, na utakapotoka uanze na mguu wako wa kushoto." Ameipokea Al-Haakim 1/218, na akaisahihisha kwa sharti ya Muslim, na Adh-Dhahabi akakubaliana naye, na ameipokea Al-Bayhaqi 2/442, na Al-Albani akaipa daraja ya Hasan katika Silsilat al-Ahadith as-Sahiha 5/624 kwa namba 2478.
Abu Daud nambari 466, na tazama: Sahih Al-Jami nambari 4591.
Ameipokea Ibn As-Sunniy kwa nambari 88, na ameihasanisha Al-Albaaniy katika Ath-Thamar Al-Mustatwaab, uk. 607.
Abu Daud 1/126 kwa nambari 465, na tazama: Sahih Al-Jami' 1/528.
Muslim 1/494 kwa nambari 713, na katika Sunan Ibn Maajah kutokana na hadithi ya Fatimah - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Ewe Mwenyezi Mungu, nisamehe madhambi yangu, na nifungulie milango ya rehema zako." Na ameifanya kuwa ni sahihi Albaani kutokana na ushahidi wake. Angalia: Sahiih Ibn Maajah 1/128 kwa nambari 129.
Al-Haakim 1/218, na Al-Bayhaqiy 2/442, na Al-Albaaniy alisema kwamba ni hadithi nzuri (Hasan) katika "Silsilat Al-Ahaadiith Asswahiiha" 5/624 kwa nambari 2478, na imeshatangulia kuelezea upokezi wake.
Tazama maelezo ya upokezi wa riwaya za Hadithi iliyotangulia katika dua ya kuingia msikitini, namba 20 na ziada: "Ewe Mwenyezi Mungu nilinde kutokana na shetani aliyelaaniwa" ya Ibn Majah. Tazama: Sahihi Ibn Majah 1/129.
Bukhari 1/152 nambari 611 na 613, na Muslim 1/288 nambari 383.
Muslim 1/290 kwa nambari 386.
Ibn Khuzaima 1/220.
Muslim 1/288 namba 384.
Bukhari 1/152 namba 614, na yaliyo baina ya mabano ni ya Al-Baihaqi 1/410, na ameipa daraja ya Hasan isnaad yake Al-'Allaamah Abdul-Aziz bin Baaz - Mwenyezi Mungu amrehemu - katika "Tuhfatul-Akhyaar" uk. 38.
Tirmidhi kwa nambari 3594 na 3595, na Abuu Daudi kwa nambari 525, na Ahmad kwa nambari 12200, na tazama: "Irwaai Al-Ghaliil" 1/262.
Bukhari 1/181 nambari 744, na Muslim 1/419 nambari 598.
Muslim kwa nambari 399, na wenye Sunan nne: Abu Daud kwa nambari 775, na Tirmidhiy kwa nambari 243, na Ibn Majah kwa nambari 806, na Nasaai kwa nambari 899, na tazama: Sahih At-Tirmidhiy 1/77, na Sahih Ibn Majah 1/135.
Imepokelewa na Muslim 1/534, nambari 771.
Imepokelewa na Muslim 1/534, nambari 770.
Imepokelewa na Abu Dawud, 1/203, nambari 764, Ibn Majah, 1/265, nambari 807, Ahmad 4/85, nambari 16739. Alisema Shu'aib Al-Arna'uut katika uthibitisho wa mlolongo wa upokezaji wa hadithi hii: "Ni hadithi hasan lighayrihii (nzuri kwa sababu ya hadithi nyinginezo mfano wake). Naye 'Abdul-Qadir Al-Arna'uut alisema katika kuelezea upokezaji wa hadithi hii katika kitabu kiitwacho Al-Kalim Atwayyib cha Ibn Taymiyyah, kwa nambari 78: Ni Hadithi Sahih inayoungwa mkono na hadithi nyinginezo mbalimbali." Naye Al-Albani aliitaja katika Sahih Al-Kalim Atwayyib, nambari 62. Vile vile, Muslim aliipokea kutoka kwa Ibn `Umar - Mwenyezi Mungu amuwiye radhi yeye na baba yake - kwa namna inayofanana na hii, na ndani yake kuna kisa, 1/420, nambari 601.
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiyasema anapoamka usiku kuswali tahajudi.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 3/3 na 11/116 na 13/371 namba 423 na 465 na 1120 na 6317 na 7385 na 7442 na 7499, na Muslim kwa muhtasari mfano wake 1/532 namba 769.
Imepokelewa na waandishi wa vitabu vya Sunan, na Ahmad: Abuu Daud kwa nambari 870, na At-Tirmidhiy kwa nambari 262, na An-Nasaai kwa nambari 1007, na Ibn Maajah kwa nambari 897, na Ahmad kwa nambari 3514, na angalia: Sahihi At-Tirmidhiy 1/83.
Bukhari 1/99 nambari 794, na Muslim 1/350 nambari 484.
Muslim 1/353 kwa nambari 487, na Abu Daud 1/230 kwa nambari 872.
Muslim 1/534 kwa nambari 771, na wale Wanne isipokuwa Ibn Majah: Abu Daud kwa nambari 760 na 761, na Tirmidhiy kwa nambari 3421, na Nasai kwa nambari 1049, na yaliyo baina ya mabano mraba ni tamko la Ibn Khuzaimah kwa nambari 607, na Ibn Hibban kwa nambari 1901.
Abu Daud 1/230 kwa nambari 873, na Nasaai kwa nambari 1131, na Ahmad kwa nambari 23980, na mlolongo wa wasimulizi wake ni mzuri.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 2/282 namba 796.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 2/284 namba 796.
Muslim 1/346 namba 477.
Imepokelewa na Ahlus-Sunan, na Ahmad: Abuu Daud kwa nambari 870, na At-Tirmidhiy kwa nambari 262, na An-Nasaai kwa nambari 1007, na Ibn Maajah kwa nambari 897, na Ahmad kwa nambari 3514, na tazama: Sahih At-Tirmidhiy 1/83.
Bukhari nambari 794, na Muslim nambari 484, na imetangulia kwa nambari 34.
Muslim 1/533 nambari 487, na Abu Dawud nambari 872 na imetangulia kwa nambari 35.
Muslim 1/534 namba 771, na wengineo.
Abu Daud 1/230 kwa nambari 873, na Nasaai kwa nambari 1131, na Ahmad kwa nambari 23980, na Al-Albaaniy alisema kwamba ni hadithi sahihi katika "Sahih Abu Daud" 1/166, na imetangulia mapokezi yake kwa nambari 37.
Muslim 1/230 namba 483.
Muslim 1/352 namba 486.
Abu Daud 1/231 kwa nambari 874, na Ibn Majah kwa nambari 897, na angalia: "Sahih Ibn Majah" 1/148.
Imepokelewa na watunzi wa Sunan isipokuwa An-Nasaai: Abu Daawuud 1/231 kwa nambari 850, na At-Tirmidhiy kwa nambari 284 na 285, na Ibn Maajah kwa nambari 898, na angalia: Sahih At-Tirmidhiy 1/90, na Sahih Ibn Maajah 1/148.
At-Tirmidhiy 2/474 kwa nambari 3425, na Ahmad 6/30 kwa nambari 24022, na Al-Haakim, na akasema kwamba ni sahihi, na Adh-Dhahabiy akakubaliana naye 1/220, na ziada ni mapokezi yake.
At-Tirmidhiy 2/473 kwa nambari 579, na Al-Haakim na akasema kwamba ni hadithi sahihi, na Adh-Dhahabiy akakubaliana naye 1/219.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 2/311, namba 831, na Muslim 1/301, namba 402.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/408, namba 3370, na Muslim, namba 406.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/407 namba 3369, na Muslim 1/306 namba 407, na tamko hili ni lake.
Bukhari 2/102 nambari 1377, na Muslim 1/412 nambari 588, na tamko hili ni la Muslim.
Bukhari 1/202 nambari 832, na Muslim 1/412 nambari 587.
Bukhari 8/168 nambari 834, na Muslim 4/2078 nambari 2705.
Muslim 1/534 namba 771.
Abu Daud 2/86 kwa nambari 1522, na Nasaai 3/53 kwa nambari 2302, na Albaniy amesema kwamba ni hadithi sahihi katika sahihi Abi Daud 1/284.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/35, namba 2822 na 6390.
Abu Daud kwa nambari 792, na Ibn Majah kwa nambari 910, na tazama: "Sahih Ibn Majah" 2/328.
Ameipokea An-Nasai 3/54 na 55 kwa nambari 1304, na Ahmad 4/364 kwa nambari 21666, na Albaani akasema kwamba ni Hadithi sahihi katika "Sahih An-Nasai" 1/281.
Ameipokea An-Nasai 3/52 kwa nambari 1300 kwa matamshi yake, na Ahmad 4/338 kwa nambari 18974, na Albaani akasema kwamba ni Hadithi sahihi katika "Sahih An-Nasai" 1/280.
Wameipokea Ahlus-Sunan: Abu Daud kwa nambari 1495, na Tirmidhiy kwa nambari 3544, na Ibn Majah kwa nambari 3858, na Nasaai kwa nambari 1299, na angalia: sahihi Ibn Majah 2/329.
Abu Daud 2/62 kwa nambari 1493, na Tirmidhiy 5/515 kwa nambari 3475, na Ibn Majah 2/1267 kwa nambari 3857, na Nasaai kwa nambari 1300 kwa tamshi lake, na Ahmad kwa nambari 18974, na ameisahihisha Albaniy katika sahihi An-Nasaai 1/280, na tazama: sahihi Ibn Majah 2/329, na sahihi Tirmidhiy 3/163.
Muslim 1/414 namba 591.
Bukhari 1/255 nambari 844, na Muslim 1/414 nambari 593, na yaliyo baina ya mabano ni ziada kutoka kwa Bukhari nambari 6473.
Muslim 1/415 namba 594.
Muslim 1/418 namba 597, na ndani yake: "Atakayesema hayo mwisho wa kila swala, yatasamehewa madhambi yake, hata kama yatakuwa na wingi mfano wa povu la bahari."
Abu Daud 2/86 kwa nambari 1523, na At-Tirmidhiy kwa nambari 2903, na An-Nasaai 3/68 kwa nambari 1335, na tazama: "Sahih At-Tirmidhiy" 2/8. Na sura hizi tatu zinaitwa: Al-Mu'awwidhaat. Tazama: Fathul Baari 9/62.
"Yeyote atakayeisoma mwisho wa kila swala, hakuna kitakachomzuia kuingia peponi isipokuwa kufa". Al-Nnasaai katika Amali Al-Yaumi wa Al-Lailah kwa nambari 100, na Ibn Al-Sunniy kwa nambari 121, na amesema Albaniy kwamba ni hadithi sahihi katika kitabu Sahihi Al-Jaami' 5/339, na Silsilatu Al-Ahaadiithi Al-Sahiihah 2/697, kwa nambari 972.
Ameipokea Tirmidhi 5/515 kwa namba 3474, na Ahmad 4/227 kwa namba 17990, na tazama takhriji yake katika Zaadul Ma'ad 1/300.
Ameipokea Ibn Majah kwa nambari 925, na An-Nasaai katika "Amali al-yaumi wal-lailah" kwa nambari 102, na tazama: "Sahih Ibn Majah" 1/152, na "Majmau Az-Zawaid" 10/111, na itakuja kwa nambari 95.
Bukhari 7/162 nambari 1162.
Surat Al Imran: 159.
Imesimuliwa kutoka kwa Anas akiipandisha kwa Mtume: "Hakika kukaa kwangu na watu wanaomdhukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kuanzia swala ya asubuhi mpaka jua lichomoze kunapendeza zaidi kwangu kuliko kuwaacha huru wanne katika watoto wa Ismaili. Na hakika kukaa kwangu na watu wanaomdhukuru Mwenyezi Mungu kuanzia swala ya alasiri mpaka jua lizame kunapendeza zaidi kwangu kuliko kuwaacha huru wanne." Ameipokea Abu Daud kwa nambari 3667, na ameipa daraja ya Hasan Al-Albani katika Sahihi Abu Daud 2/698.
"Atakayesema wakati wa asubuhi, atalindwa dhidi ya majini mpaka afike jioni. Na atakayesema wakati wa jioni, atalindwa dhidi yao mpaka afike asubuhi." Kaipokea Al-Haakim 1/562, na akaisahihisha Al-Albaaniy katika Sahihi At-Targhiib wat-Tarhiib 1/273, na akainasibisha kwa An-Nasaaiy, na At-Tabaraaniy, na akasema: "Isnaad ya At-Tabaraaniy ni nzuri".
"Atakayeisema mara tatu wakati wa asubuhi na wakati wa jioni, itamtosheleza kutokana na kila kitu." Ameipokea Hadithi hii Abu Daud 4/322 kwa nambari 5082, na At-Tirmidhi, 5/567 kwa nambari 3575, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi" 3/182.
Muslim 4/2088 namba 2723.
Rejea iliyotangulia.
At-Tirmidhi 5/466 namba 3391, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi" 3/142.
Marejeo yaliyotangulia.
Ninakiri na kukubali.
"Atakayeisema hali ya kuwa na yakini nayo wakati wa jioni, kisha akafa usiku wake huo, ataingia peponi, na kadhalika ifikapo asubuhi". Ameipokea Bukhari 7/150 kwa nambari 6306.
"Atakayeisema asubuhi au jioni mara nne, Mwenyezi Mungu atamuacha huru kutokana na Moto". Ameipokea Hadithi hii Abu Dawud 4/317 kwa nambari 5071, na Al-Bukhari katika kitabu "Al-Adab Al-Mufrad" kwa nambari 1201, na An-Nasaai katika kitabu "'Amal Al-Yawm Wal-Laylah" kwa nambari 9, na Ibn As-Sunni kwa nambari 70, na Mheshimiwa Sheikh Ibn Baaz -Mwenyezi Mungu amrehemu- akasema kwamba Isnaad ya An-Nasaai na Abu Dawud ni Hasan katika kitabu "Tuhfat Al-Akhyaar" uk. 23.
Rejea iliyotangulia.
"Atakayeisema wakati ameamka, kwa hakika ametekeleza shukrani ya siku yake. Na atakayeisema wakati amefika jioni, kwa hakika ametekeleza shukrani ya usiku wake." Kaipokea Abuu Dawud 4/318 nambari 5075, na Nasai katika Amal Al-Yaum Wal-Lailah nambari 7, na Ibn Sunni nambari 41, na Ibn Hibban (Mawarid) nambari 2361, na Ibn Baaz Mwenyezi Mungu amrehemu ameifanya nzuri (Hasan) isnaadi yake katika Tuhfat Al-Akhyar ukurasa 24.
Marejeo yaliyotangulia.
Abu Daud 4/324 kwa nambari 5092, na Ahmad 5/42 kwa nambari 20430, na Nasaai katika "Amalul-Yawmi wal-Laylah" kwa nambari 22, na Ibn As-Sunniy kwa nambari 69, na Al-Bukhariy katika "Al-Adabul-Mufrad" kwa nambari 701, na mwanazuoni mkubwa Ibn Baaz, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema kwamba mlolongo wa wasimulizi wake ni mzuri katika kitabu kiitwacho "Tuhfatul-Akhyaar" ukurasa wa 26.
"Atakayeisema asubuhi na jioni mara saba, Mwenyezi Mungu atamtosheleza kwa yale yanayomshughulisha katika mambo ya dunia na Akhera." Ameipokea Hadithi hii Ibn As-Sunniy kwa nambari 71 ikiwa imefika kwa Mtume rehema na amani zimshukie (Marfuu), na Abuu Daud ikiwa haijafika kwa Mtume rehema na amani zimshukie (Mauquuf) 4/321 kwa nambari 5081, na wameisahihisha isnaad yake Shuaib na Abdulqadir Al-Arnaaut. Tazama: Zaadul-Ma'aad 2/376.
Abu Daud kwa nambari 5074, na Ibn Majah kwa nambari 3871, na tazama: sahihi Ibn Majah 2/332.
At-Tirmidhi, nambari 3392, na Abu Daud, nambari 5067, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi", 3/142.
"Atakayeisema mara tatu asubuhi, na mara tatu jioni hakuna chochote kitakachomdhuru." Ameipokea Abu Daud 4/323 kwa nambari 5088, na At-Tirmidhiy 5/465 kwa nambari 3388, na Ibn Majah kwa nambari 3869, na Ahmad kwa nambari 446. Na tazama: Sahiih Ibn Majah 2/332, na mwanachuoni Ibn Baaz Mwenyezi Mungu amrehemu alisema kwamba isnadi yake ni nzuri katika Tuhfat Al-Akhyaar uk. 39.
"Atakayeisema mara tatu wakati wa asubuhi, na mara tatu wakati wa jioni, inakuwa ni haki kwa Mwenyezi Mungu kumridhisha siku ya Kiyama." Ahmad 4/337 kwa nambari 18967, na An-Nasa'i katika Amal Al-Yawm wal-Laylah kwa nambari 4, na Ibn As-Sunni kwa nambari 68, na Abu Daud 4/318 kwa nambari 1531, na At-Tirmidhi 5/465 kwa nambari 3389, na Ibn Baz, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema kwamba ni hadithi nzuri katika Tuhfat Al-Akhyaar uk. 39.
Ameipokea Al-Haakim na akasema kwamba ni hadithi sahihi, na Adh-Dhahabi akakubaliana naye 1/545, na tazama: "Sahih At-Targhiib wa At-Tarhiib" 1/273.
Abu Daud 4/322 namba 5084, na wamefanya upokezi wake kuwa mzuri Shu'aib na Abdul-Qaadir Al-Arna’ut katika uhakiki wa "Zaad Al-Ma'aad" 2/373.
Marejeo yaliyotangulia.
Ahmad 3/406 na 407 namba 15360 na 15563, na Ibn as-Sunni katika "Amal Al-Yawm Wal-Laylah", namba 34. Tazama pia: "Sahih Al-Jami’" 4/209.
Marejeo yaliyotangulia.
"Atakayeisema mara mia moja asubuhi na jioni, hatoleta yeyote siku ya Kiyama kitu bora kuliko alichokuja nacho, isipokuwa mtu aliyesema mfano wa alichokisema au akazidisha zaidi ya hapo." Muslim 4/2071 kwa namba 2692.
An-Nasaai katika Amali Al-Yaumi wa Al-Lailah kwa nambari 24, na tazama: Sahih At-Targhib wa At-Tarhib 1/272, na Tuhfat Al-Akhyar ya Ibn Baaz (Mwenyezi Mungu amrehemu) ukurasa 44, na tazama fadhila zake katika ukurasa 146 hadithi nambari 255.
Abu Daud kwa nambari 5077, na Ibn Majah kwa nambari 3798, na Ahmad kwa nambari 8719, na tazama: sahihi At-Targhiib Wat-Tarhiib 1/270, na sahihi Abi Daud 3/957, na sahihi Ibn Majah 2/331, na Zaad Al-Ma'aad 2/377.
"Atakayeisema kwa siku mara mia moja, inakuwa kwake ni sawa na kuacha huru watu kumi, na anaandikiwa mema mia moja, na anafutiwa makosa mia moja, na inakuwa kwake ni kinga kutokana na shetani katika siku yake hiyo mpaka afike jioni, na hatokuja yeyote na jambo bora zaidi kuliko atakalokuja nalo, isipokuwa yule atakayefanya zaidi ya alivyofanya yeye." Al-Bukhari 4/95 kwa namba 3293, na Muslim 4/2071 kwa namba 2691.
Muslim 4/2090 namba 2726.
Imepokelewa na Ibn As-Sunni katika "Amali al-yaumi wal-lailah" kwa nambari 54, na Ibn Majah kwa nambari 925, na Abdul Qadir na Shuaib Al-Arnaout walisema kwamba msururu wa wapokezi wake (isnaad) ni hasan katika uhakiki wa "Zaad al-Ma'aad" 2/375 na imetangulia kwa nambari 73.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/101, namba 6307, na Muslim, 4/2075, namba 2702.
(Atakayeisema wakati wa jioni mara tatu, haitamdhuru sumu ya mdudu usiku huo). Ameipokea Hadithi hii Ahmad 2/290 kwa nambari 7898, na An-Nnasaai katika Amali Al-Yaumi wa Al-Lailah kwa nambari 590, na Ibn Al-Sunniy kwa nambari 68, na angalia: kitabu Sahihi At-Tirmidhiy 3/187, na kitabu sahihi Ibn Maajah 2/266, na Tuhfat Al-Akhyaar cha Ibn Baaz ukurasa wa 45.
"Mwenye kunitakia rehema asubuhi mara kumi, na jioni mara kumi, uombezi wangu utamfikia Siku ya Kiyama." Ameipokea At-Tabarani kwa sanadi mbili: mojawapo ni nzuri, tazama: Majma'u az-Zawaid 10/120, na Swahih at-Targhib wat-Tarhib 1/273.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 9/62 namba 5017, na Muslim namba 2192.
"Mwenye kuisoma anapoenda kwenye malazi yake, hakika yeye hataacha kuwa na mlinzi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, wala hakuna shetani atakayemkaribia mpaka afike asubuhi." Bukhari pamoja na Al-Fath 4/487 kwa nambari 2311.
"Mwenye kuzisoma nyakati za usiku, zitamtosheleza." Bukhari pamoja na Al-Fath 9/94 nambari 4008, na Muslim 1/554 nambari 807.
"Atakaposimama mmoja wenu kutoka katika malazi yake kisha akayarejea, basi na ayakung'ute kwa ukingo wa shuka lake mara tatu, na ataje jina la Mwenyezi Mungu. Kwa maana hajui ni nini kilichokuja hapo nyuma yake baada yake, na atakapolala basi aseme:.." Hadiithi, [Na maana ya ukingo wa shuka lake: ni ncha yake inayofuatia pindo lake]. An-Nihayah fiy Ghariib Al-Hadiyth wal-Athar (Sanif).
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/126, namba 6320, na Muslim, 4/2084, namba 2714.
Ameipokea hadithi hii Muslim 4/2083 nambari 2712, na Ahmad kwa tamko lake 2/79 nambari 5502.
"Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapotaka kulala, anaweka mkono wake wa kulia chini ya shavu lake, kisha anasema: ..." Hadithi.
Abu Daud kwa tamko lake 4/311 kwa nambari 5045, na At-Tirmidhiy kwa nambari 3398, na tazama: "Sahih At-Tirmidhiy" 3/143, na "Sahih Abu Daud" 3/240.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/113, namba 6324, na Muslim, 4/2083, namba 2711.
"Atakayesema hayo anapokuwa katika malazi yake, itakuwa kheri kwake kuliko mtumishi." Bukhari pamoja na Al-Fath, 7/71 kwa nambari 3705, na Muslim 4/2091 kwa nambari 2726.
Muslim 4/2084 namba 2713.
Muslim 4/2085, namba 2715.
Abu Daud 4/317 namba 5067, na At-Tirmidhi namba 3629, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 3/142.
At-Tirmidhiy kwa nambari 3404, na An-Nasaai katika "Amali al-yaumi wal-lailah" kwa nambari 707, na tazama: Sahih Al-Jaami' 4/255.
"Utakapochukua malazi yako, shika udhu kama udhu unapotaka kusali, kisha lalia ubavu wa kulia, kisha sema: ..." Hadithi.
Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- kwa aliyesema hivyo: 'Basi ukifa utakufa juu ya Fitra.' Ameipokea Bukhari pamoja na Fath 11/113 kwa nambari 6313, na Muslim 4/2081 kwa nambari 2710."
Anasema hayo anapogeuka kutoka upande mmoja kwenda mwingine usiku. Ameitoa Haakim, na amesema kwamba ni sahihi na amekubaliana naye Adhahaby 1/540, na Al-Nnasaai katika Amali Al-Yaumi wa Al-Lailah kwa nambari 202, na Ibn Al-Sunniy kwa nambari 757, na tazama: kitabu sahihi Al-Jaami 4/213.
Abu Daud 4/12 namba 3893, na At-Tirmidhi namba 3528, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 3/171.
Muslim 4/1772 namba 2261.
Muslim 4/1772, 1773 namba 2261 na 2262.
Muslim 4/1772 namba 2261 na 2263.
Muslim 4/1773 namba 2261.
Muslim 4/1773 namba 2263.
Wameipokea Hadithi hii Ashaabu wa Sunan nne, na Ahmad, na Ad-Daarimiy, na Al-Bayhaqiy: Abuu Daud kwa nambari 1425, na At-Tirmidhiy kwa nambari 464, na Al-Nnasaai kwa nambari 1744, na Ibn Maajah kwa nambari 1178, na Ahmad kwa nambari 1718, na Ad-Daarimiy kwa nambari 1592, na Al-Haakim 3/172, na Al-Bayhaqiy 2/209, na yaliyo kwenye mabano ni ya Al-Bayhaqiy, na tazama: sahihi At-Tirmidhiy 1/144, na sahihi Ibn Maajah 1/194, na Irwaau Al-Ghaliyl ya Albaniy 2/172.
Wameitoa watunzi wa Sunan nne, na Ahmad: Abu Daud kwa nambari 1427, na Tirmidhiy kwa nambari 3566, na Nasaai kwa nambari 1746, na Ibn Maajah kwa nambari 1179, na Ahmad kwa nambari 751. Tazama: sahihi At-Tirmidhiy 3/180, na Sahihi Ibn Maajah 1/194, na Al-Irwaa 2/175.
Ameipokea Al-Baihaqiy katika As-Sunan Al-Kubraa, na ameisahihisha sanad yake 2/211, na amesema Sheikh Al-Albaniy katika Irwaa Al-Ghaliyl: "Na hii ni sanad sahihi" 2/170. Nayo imekomea (Mawquuf) kwa Umar.
Kaipokea An-Nasaai 3/244 kwa nambari 1734, na Al-Daaraqutniy 2/31, na wengineo, na yaliyo kwenye mabano ni ziada ya Al-Daaraqutniy 2/31 kwa nambari 2, na Isnadi yake ni Sahihi. Tazama: Zaad Al-Ma'aad kwa uhakiki wa Shu'ayb Al-Arnaauutw na Abdul-Qaadir Al-Arnaauutw 1/337.
Ahmad 1/391 namba 3712, na Al-Albaani alisema kwamba ni Hadithi sahihi katika "Silsilat Al-Ahadith Al-Sahihah" 1/337.
Bukhari 7/158 kwa nambari 2893. Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa akisema dua hii kwa wingi. Tazama: Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/173, na itakuja uk. 89 kwa nambari 137.
Bukhari 7/154 nambari 6345, na Muslim 4/2092 nambari 2730.
Abu Daud, 4/324, namba 5090, na Ahmad, 5/42, namba 20430, na Al-Albani alisema kwamba ni Hadithi nzuri (Hasan) katika "Sahih Abi Daud", 3/959.
At-Tirmidhi 5/529 namba 3505, na Al-Hakim, na akasema kwamba ni hadithi sahihi, na Adh-Dhahabi akakubaliana naye 1/505, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi" 3/168.
Ameipokea Abuu Daudi 2/87 kwa nambari 1525, na Ibn Majah kwa nambari 3882, na tazama: Sahih Ibn Majah 2/335.
Abu Daud 2/89 kwa nambari 1537, na Al-Haakim alisema kwamba ni Hadithi sahihi na akakubaliana naye Adh-Dhahabiy 2/142.
" Abu Daud 3/42 namba 2632, na At-Tirmidhi 5/572 namba 3584, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 3/183."
Bukhari 5/172 kwa nambari 4563.
Bukhari katika Adabu Al-Mufrad kwa nambari 707, na amesema Albaniy kwamba ni hadithi sahihi katika Sahihi Adabu Al-Mufrad kwa nambari 545.
Bukhari katika Adabu Al-Mufrad kwa nambari 708, na amesema Albaniy kwamba ni hadithi sahihi katika Sahihi Adabu Al-Mufrad kwa nambari 546.
Muslim 3/1362, namba 1742.
Muslim 4/2300 namba 3005.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/336, namba 3276, na Muslim 1/120, namba 134.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/336 namba 3276, na Muslim 1/ 120 namba 134.
Muslim 1/119-120 namba 134.
Abu Daud 4/329 kwa nambari 5110, na Al-Albani alisema kwamba ni Hadithi nzuri (Hasan) katika "Sahih Abi Daud" 3/962.
At-Tirmidhi 5/560 namba 3563, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi" 3/180.
Bukhari 7/158 kwa nambari 2893, na imetangulia uk. 83 kwa nambari 121.
Muslim 4/1729 nambari 2203, kutoka katika Hadithi ya Uthman bin Abi Al-Aas, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, na ndani yake: Basi nikafanya hivyo, Mwenyezi Mungu akaniondolea hilo.
Ameipokea Ibn Hibaan katika Sahihi yake kwa nambari 2427 (Mawaarid), na Ibn Al-Sunniy kwa nambari 351, na amesema Al-Haafidhw: "Hii ni Hadithi sahihi", na ameisahihisha Abdul Qaadir Al-Arnaauutw katika Takhriij Al-Adhkaar ya Al-Nawawiy uk. 106.
Abu Daud, 2/86, namba 1521, na At-Tirmidhi, 2/257, namba 406, na Al-Albaani alisema kwamba ni hadithi sahihi katika "Sahih Abi Daud", 1/283.
Abu Daud 1/203 kwa nambari, na Ibn Majah 1/265 kwa nambari 807 na imetangulia kuelezea upokezi wake kwa nambari 31, na tazama: Surat Al-Mu'minun: [97-98].
Muslim 1/291 kwa nambari 389, na Bukhari 1/151 kwa nambari 608.
Kaipokea Muslim 1/539 kwa nambari 780.
Kaipokea Bukhari 4/126 kwa nambari 3293.
"Muumini mwenye nguvu ni bora na anapendeka kwa Mwenyezi Mungu kuliko muumini dhaifu, na katika kila mmoja wao kuna kheri. Pupia yenye manufaa na wewe, na utake msaada kwa Mwenyezi Mungu na wala usishindwe. Na likikusibu jambo, usiseme: 'Lau ningefanya kadha, basi ingelikuwa kadha na kadha', lakini sema: 'Hili ni kwa mipango ya Mwenyezi Mungu naye hufanya alitakalo', maana neno "Lau" hufungua matendo ya shetani" Muslim 4/2052 namba 2664.
Imetajwa kutokana na maneno ya Al-Hasan Al-Basri. Tazama: Kitabu Tuhfatul Mawduud cha Bin Qayyim uk. 20, na akainasibisha kwa Bin Mundhir katika Al-Awsat.
Amesema haya Annawawiy katika kitabu Al-Adhkaar ukurasa 349, angalia kitabu: Swahiih Al-Adhkaar cha Annawawiy, cha Saliim Al-Hilaaliy 2/713, na Tamaam At-Takhriij katika Adh-Dhikr na Dua na tiba na kisomo cha ruqya cha mtunzi 1/416 huyu.
Bukhari 4/119 nambari 3371, kutoka kwa Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awawiye radhi.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 10/118, namba 3616.
“Hakuna mja Muislamu anayemtembelea mgonjwa ambaye muda wake wa kifo haujafika na kusema mara saba:...isipokuwa ataponywa.” Ameipokea Tirmidhi kwa namba 2083, na Abu Dawud kwa namba 3106, na tazama: Swahih Tirmidhi 2/210, na Swahihul Jami'i 5/180.
Ameipokea At-Tirmidhiy kwa nambari 969, na Ibn Majah kwa nambari 1442, na Ahmad kwa nambari 975, na Tazama: sahihi Ibn Majah 1/244 na Sahihi At-Tirmidhiy 1/286, na Ahmad Shakir pia amesema kwamba ni sahihi.
Bukhari 7/10 namba 4435, na Muslim 4/1893 namba 2444.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 8/144, namba 4449, na katika Hadithi kumetajwa mswaki.
Ameipokea Hadithi hii At-Tirmidhiy kwa nambari 3430, na Ibn Maajah kwa nambari 3794, na amesema Albaniy kwamba ni hadithi sahihi, tazama: Sahihi At-Tirmidhiy 3/152, na Sahihi Ibn Maajah 2/317.
Abu Daud 3/190 namba 3116, na angalia: "Sahih Al-Jami’i" 5/432.
Muslim, 2/632, namba 918.
Muslim 2/634 namba 920.
Muslim 2/663 namba 963.
Abu Daud kwa nambari 3201, na Tirmidhiy kwa nambari 1024, na Nasaai kwa nambari 1985, na Ibn Majah 1/480 kwa nambari 1498, na Ahmad 2/368 kwa nambari 8809, na tazama: Sahih Ibn Majah 1/251.
Ameipokea Hadithi hii Ibn Maajah kwa nambari 1499, tazama: sahihi Ibn Maajah 1/251, na ameipokea Abu Daud 3/211 kwa nambari 3202.
Ameipokea Al-Haakim na akasema kwamba ni sahihi, na Adh-Dhahabiy akakubaliana naye 1/359. Pia angalia kitabu "Ahkaam Al-Janaaiz" cha Albaani ukurasa wa 125.
(Amesema Saidi bin Musayyab: Niliswali nyuma ya Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kumswalia mtoto ambaye hakutenda dhambi kamwe, nikamsikia akisema..) Hadithi. Ameipokea Maalik katika Al-Muwattwa 1/288, na Ibnu Abiy Shaiba katika Al-Muswannaf 3/217, na Al-Baihaqiy 4/9, na akasahihisha isnadi yake Shuaib Al-Arnaout katika uhakiki wake wa Sharh as-Sunnah ya Al-Baghawiy 5/357.
Tazama: Al-Mughni, cha bin Qudama 3/416, na Ad-Duruusul-Muhimmah Li'aamatil-Ummah, cha Sheikh Abdul-Aziz bin Abdillah bin Baaz, Mwenyezi Mungu amrehemu, uk. 15.
Alikuwa Hasan akimsomea mtoto Suratul Fatiha, na akisema... Hadithi. Imepokelewa na Baghawi katika Sharhus Sunnah 5/357, na Abdur-Razzaq kwa namba 6588, na ameipokea Bukhari kwa njia ya Taaliq katika Kitabu cha Janaiz 65 mlango wa kusoma Suratul Fatiha kwenye jeneza 2/113, kabla ya Hadithi nambari 1335.
Bukhari 2/80 nambari 1284, na Muslim 2/636 nambari 923.
Al-Adhkaar ya An-Nawawiy ukurasa wa 126.
Abu Daud 3/314 kwa nambari 3215 kwa sanadi sahihi, na Ahmad kwa nambari 5234 na nambari 4812 kwa tamko: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na kulingana na mila ya Mtume wa Mwenyezi Mungu', na sanadi yake ni sahihi.
Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa anapomaliza kumzika maiti, anasimama karibu yake na anasema: "Mwombeeni msamaha ndugu yenu, na mwombeeni uthabiti; kwani sasa anaulizwa." Abu Dawud 3/315 kwa namba 3223 na Al-Hakim na akaisahihisha, na Adh-Dhahabi akakubaliana naye 1/370.
Muslim 2/671 kwa nambari 975, na Ibn Majah 1/494, na tamko ni lake kwa nambari 1547 kutoka kwa Buraida, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, na yaliyo baina ya mabano ni kutoka katika hadithi ya Aisha, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, kwa Muslim 2/671 kwa nambari 975.
Imepokelewa na Abu Daawuud 4/326, nambari 5099, na Ibn Maajah 2/1228, nambari 3727, na tazama: Swahihi Ibn Maajah 2/305.
Muslim, na tamko hili ni lake 2/666 kwa nambari 899, na Bukhari 4/76 kwa nambari 3206 na 4829.
Alikuwa Abdillahi bin Zubeyri- radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- anaposikia radi, anaacha kuzungumza na kusema:... Hadithi, Al-Muwatta 2/992, na Al-Albani amesema katika "Sahih Al-Kalim at-Tayyib" 157: "Sanadi yake ni sahihi na ni Mawquf".
Abu Daud 1/303 kwa nambari 1171, na Al-Albaani alisema kwamba ni hadithi sahihi katika "Sahih Abi Daud" 1/216.
Bukhari 1/224 kwa nambari 1014, na Muslim 2/613 kwa nambari 897.
Abu Daud 1/305 kwa nambari 1178, na Al-Albani alisema kwamba ni Hadithi nzuri (Hasan) katika "Sahih Abi Daud" 1/218.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 2/518 namba 1032.
Bukhari 1/205 nambari 846, na Muslim 1/83 nambari 71.
Bukhari 1/224 kwa nambari 933, na Muslim 2/614 kwa nambari 897.
At-Tirmidhi, 5/504, namba 3451, na Ad-Darimi kwa tamko lake, 1/336, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi", 3/157.
Imepokelewa na Abuu Daud 2/306 nambari 2359, na wengineo. Na tazama: Swahihi Jaamiiy 4/209.
Ameipokea Hadithi hii Ibn Maajah 1/557 kwa nambari 1753 kutokana na dua ya Abdullah bin Amr, Mwenyezi Mungu awaridhie, na ameihasanisha Al-Haafidh katika kitabu cha "Takhriij Al-Adhkaar". Tazama: "Sharhu Al-Adhkaar" 4/342.
Imepokelewa na Abu Daawuud 3/347 nambari 3767, na At-Tirmidhiy 4/288 nambari 1858, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 2/167.
At-Tirmidhi 5/506 namba 3455, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 3/158.
Imepokelewa na waandishi wa vitabu vya Sunan isipokuwa An-Nasaai: Abu Daawuud kwa nambari 4025, na At-Tirmidhiy kwa nambari 3458, na Ibn Maajah kwa nambari 3285, na tazama sahihi At-Tirmidhiy 3/159.
Bukhari 6/214 nambari 5458, na Tirmidhi kwa tamko lake 5/507 nambari 3456.
Muslim 3/1615 namba 2042.
Muslim 3/1626 namba 2055.
Sunan Abu Daud 3/367 kwa nambari 3856, na Ibn Majah 1/556 kwa nambari 1747, na Nasaai katika Amalul-Yaumi Wal-Lailah, kwa nambari 296-298, na akabainisha kwamba yeye Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alikuwa akiisema anapofuturu kwa watu wa nyumba, na amesema Albaniy kwamba ni hadithi sahihi katika Sahihi Abu Daud 2/730.
Muslim, 2/1054, namba 1150.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 4/103 namba 1894, na Muslim 2/806 namba 1151.
Muslim 2/1000 namba 1373.
Bukhari 7/125 nambari 5870.
At-Tirmidhi 5/82 namba 2741, na Ahmad 4/400 namba 19586, na Abu Daud 4/308 namba 5040, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 2/354.
Imepokelewa na As-haabus-Sunan isipokuwa An-Nasaai: Abu Daawuud kwa nambari 2130, na At-Tirmidhiy kwa nambari 1091, na Ibn Maajah kwa nambari 1905, na An-Nasaai katika "Amali al-yaumi wal-lailah" kwa nambari 259, na tazama: Sahih At-Tirmidhiy 1/316.
Abu Daud 2/248 kwa nambari 2160, na Ibn Majah 1/617 kwa nambari 1918, na tazama: Sahih Ibn Majah 1/324.
Bukhari 6/141 nambari 141, na Muslim 2/1028 nambari 1434.
Bukhari 7/99 nambari 3282, na Muslim 4/2015 nambari 2610.
At-Tirmidhi, 5/494 na 5/493, namba 3432, na tazama: "Sahih At-Tirmidhi", 3/153.
At-Tirmidhiy kwa nambari 3434, na Ibn Majah kwa nambari 3814, na tazama: sahihi Al-Tirmidhiy 3/153, na sahihi Ibn Majah 2/321, na tamko ni la At-Tirmidhiy.
Wenye Sunan: Abu Daud kwa nambari 4858, na At-Tirmidhiy kwa nambari 3433, na An-Nasaai kwa nambari 1344, na tazama "Sahih At-Tirmidhiy" 3/153, na imethibiti ya kwamba Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alisema: "Hakukaa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake kikao chochote, na wala hakusoma Qur'ani, na wala hakuswali swala isipokuwa alihitimisha hilo kwa maneno..." Hadithi, ameipokea An-Nasaai katika "Amal Al-Yaum Wal-Lailah" kwa nambari 308, na Ahmad 6/77 kwa nambari 24486, na amesema Daktari Faruq Hamadah kwamba ni sahihi katika uhakiki wake wa "Amal Al-Yaum Wal-Lailah" ya An-Nasaai uk. 273.
Ahmad 5/82 yenye namba 20778, na An-Nasaai katika "Amal Al-Yawm wal-Laylah" uk. 218 kwa namba 421, uhakiki wa Daktari Farouq Hamadah.
Imepokelewa na At-Tirmidhiy, nambari 2035, na tazama: Swahihi Al-jaamiy 6244 na Swahihi At-Tirmidhiy 2/200.
Tazama: hadithi namba 55, na hadithi 56 ukurasa 41 katika kitabu hiki.
Muslim 1/555 nambari 809, na katika riwaya: "Kutoka mwisho wa Al-Kahf" 1/556 nambari 809.
Imepokelewa na Abuu Daud 4/333, nambari 5125, na Al-Albaani alisema kwamba ni hadithi nzuri (Hasan) katika Sahihi Sunan Abi Daud 3/965.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 4/288, namba 2049.
Ameipokea Hadithi hii An-Nasaai katika "Amali al-yaumi wal-lailah" uk. 300, na Ibn Maajah 2/809 kwa nambari 2424, na tazama: "Sahih Ibn Maajah" 2/55.
Ahmad 4/403 kwa nambari 19606, na Al-Adab Al-Mufrad cha Bukhari kwa nambari 716, na tazama: Sahih Al-Jaami'i 3/233, na Sahih At-Targhiib wa At-Tarhiib cha Albaani 1/19.
Imepokelewa na Ibn As-Sunni uk. 138, nambari 278, na tazama: Al-Wabil As-Sayyib cha Ibn Al-Qayyim uk. 304, uhakiki wa Bashir Muhammad Uyun.
Ahmad 2/220 kwa nambari 7045, na Ibn As-Sunni kwa nambari 292, na ameisahihisha Al-Albani katika "Silsilat Al-Ahadith As-Sahiha" 3/54 kwa nambari 1065. Ama kujipa matumaini kulikuwa kunamfurahisha Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-; na kwa ajili hiyo alisikia maneno mazuri kutoka kwa mtu yakamfurahisha akasema: "Tumeyachukua matumaini yako kutoka kinywani mwako", Abu Dawud kwa nambari 3719, na Ahmad kwa nambari 9040, na amesema Al-Albani kwamba ni sahihi katika "Silsilat Al-Ahadith As-Sahiha" 2/363, kwa Abu Ash-Shaykh katika "Akhlaq An-Nabiyy" -rehema na amani ziwe juu yake- ukurasa 270.
Abu Daud 3/34 kwa nambari 2602, na At-Tirmidhiy 5/501 kwa nambari 3446, na tazama: Sahih At-Tirmidhiy 3/156, Surat Az-Zukhruf [13- 14].
Muslim 2/978 namba 1342.
" Ameipokea Al-Haakim na akasema ni hadithi sahihi, na Adh-dhahabi akakubaliana naye 2/100, na Ibn As-Sunni kwa nambari 524, na Al-Hafidh alisema kwamba ni hadithi nzuri (hasan) katika kitabu "Takhriij Al-Adhkaar" 5/154, alisema mwanazuoni mkuu Ibn Baaz Mwenyezi Mungu amrehemu: "Na ameipokea An-Nasai kwa isnad nzuri (hasan)". Tazama: "Tuhfatu Al-Akhyaar" uk. 37."
At-Tirmidhi, namba 3428, na Ibn Majah 5/291 namba 3860, na Al-Haakim 1/538, na Al-Albaani alisema kwamba ni hadithi nzuri (Hasan) katika Sahih Ibn Majah 2/21, na katika Sahih At-Tirmidhi 3/152.
Abu Daud 4/296 kwa nambari 4982, na Al-Albaani alisema kwamba ni Hadithi sahihi katika "Sahih Abi Daud" 3/941.
Ahmad 2/403 kwa namba 9230, na Ibn Majah 2/943 kwa namba 2825, na tazama: Sahih Ibn Majah 2/133.
Ahmad 2/7 kwa namba 4524, na At-Tirmidhi 5/499 kwa namba 3443, na amesema Al-Albani kwamba ni sahihi katika Sahihi Sunani Attrimidhi 3/419.
Ameipokea Tirmidhiy kwa namba 3444, na tazama: Sahih At-Tirmidhi 3/155.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/135, namba 2993.
Muslim 4/2086 namba 2718, na maana ya Samma'a saami'un: yaani ameshuhudia shahidi juu ya kumhimidi kwetu Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa neema zake, na majaribio yake mema. Na maana ya Samma'a saami'un: Afikishe msikilizaji kauli yangu hii kwa mwingine, na aseme mfano wake kama ukumbusho juu ya dhikri katika wakati wa mwisho wa usiku na dua. Sharh an-Nawawi juu ya Sahih Muslim 17/39.
Muslim 4/2080 namba 2709.
Alikuwa mtume -rehema na amani ziwe juu yake- akiyasema anaporudi kutoka vitani au Hija, Bukhari 7/163 kwa nambari 1797, na Muslim 2/980 kwa nambari 1344.
Ameipokea Ibn As-Sunniy katika Amali Al-Yaumi wa Al-Lailah kwa nambari 377, na Haakim na akasema kwamba ni sahihi 1/499, naye Al-albaaniy alisema kwamba ni sahihi katika Swahihiul jaamiy 4/201.
Imepokelewa na Muslim 1/288, nambari 384.
Abu Daud 2/218 kwa nambari 2044, na Ahmad 2/367 kwa nambari 8804, na Al-Albaani alisema kwamba ni Hadithi sahihi katika "Sahih Abi Daud" 2/383.
At-Tirmidhiy, 5/551, kwa nambari 3546, na wengineo. Tazama: "Sahih Al-Jaami'i", 3/25, na "Sahih At-Tirmidhiy", 3/177.
Ameipokea An-Nnasai 3/43 kwa nambari 1282, na Al-Hakim 2/421, na amesema Albaniy kwamba ni hadithi sahihi katika Sahihi An-Nnasai 1/274.
Abu Daud kwa nambari 2041, na ameipa daraja la kuwa Hadithi nzuri (Hasan) Albaniy katika sahihi Abi Daud 1/383.
Muslim 1/74 nambari 54, na Ahmadi nambari 1430, na tamko hili ni la kwake, na tamko la Muslim ni: "Laa tadkhuluuna (Hamtaingia)...".
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 1/82, namba 28, kutoka kwa Ammar, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, ikiwa ni Mawquuf Mu'allaq.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 1/55 namba 12, na Muslim 1/65 namba 39.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/42 namba 6258, na Muslim 4/1705 namba 2163.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/350 namba3303, na Muslim 4/2092 namba 2729.
Abu Daud 4/327 kwa nambari 5105, na Ahmad 3/306 kwa nambari 14283, na Al-Albaani alisema kwamba ni Hadithi sahihi katika "Sahih Abi Daud" 3/961.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/171 namba 6361, na Muslim 4/2007 namba 396, na lafdhi yake: "Basi ijaalie kwake iwe ni utakaso na rehema."
Ameipokea Muslim 4/2296 kwa nambari 3000.
Bukhari katika Adabu Al-Mufrad kwa nambari 761, na amesema Albaani kwamba msururu wa wasimulizi wake ni sahihi katika Sahih Adabu Al-Mufrad kwa nambari 585, na yaliyo baina ya mabano ni ziada ya Al-Baihaqiy katika Shu'ab Al-Iymaan 4/228 kutoka njia nyingine.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 3/408, namba 1549, na Muslim 2/841, namba 1184.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 3/476, namba 1613, na kinachokusudiwa kwa neno 'kitu' ni: Al-Mihjan. Tazama: Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 3/472.
Abu Daud 2/179 kwa nambari 1894, na Ahmad 3/411 kwa nambari 15398, na Al-Baghawiy katika "Sharh As-Sunnah" 7/128, na Al-Albaaniy akasema kwamba ni nzuri (hasan) katika "Swahih Abi Daud", 1/354, Surat Al-Baqarah.
Muslim 2/888 namba 1218, Surat Al-Baqarah: namba 158.
At-Tirmidhi kwa namba 3585, na Al-Albaani alisema kwamba ni hadithi nzuri (Hasan) katika Sahih At-Tirmidhi 3/184, na katika Silsilat Al-Ahadith As-Sahiha 4/6.
Muslim 2/891 namba 1218.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 3/583 namba 1751, na tazama tamko lake huko. Na Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 3/583, na 3/584, na 3/581 namba 1753, na ameipokea Muslim pia namba 1218.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 1/210 na 390 na 414 namba 115 na 3599 na 6218, na Muslim 4/1857 namba 1674.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 8/441 namba 4741 na 3062, na At-Tirmidhiy kwa nambari 2180, na An-Nasaai katika kitabu cha "Al-Kubraa" kwa nambari 11185, na tazama: Sahih At-Tirmidhiy 2/103 na 2/235, na Musnad Ahmad 5/218 namba 21900.
Wameipokea Ahlus-Sunan isipokuwa An-Nasaai: Abu Daud kwa nambari 2774, na At-Tirmidhiy kwa nambari 1578, na Ibn Majah kwa nambari 1394, tazama "Sahih Ibn Majah" 1/233, na "Irwaa Al-Ghaliyl" 2/226.
Muslim 4/1728 namba 2202.
Musnad Ahmad 4/447 namba 15700, na Ibn Maajah nambari 3508, na Maalik 3/118-119, na Al-Albani alisema kwamba ni hadithi sahihi katika "Sahih Al-Jaami'" 1/212, tazama pia uhakiki wa "Zaad Al-Ma'ad" wa Al-Arnauut 4/170.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 6/381, namba 3346, na Muslim, 4/2208, namba 2880.
Muslim 3/1557 kwa nambari 1967, na Al-Baihaqi 9/287 na kilicho baina ya mabano kiko kwa Al-Baihaqi 9/287 na wengineo, na sentensi ya mwisho nimeileta kwa maana kutoka katika riwaya ya Muslim.
Ahmad 3/419 nambari 15461 yenye mnyororo sahihi wa wapokezi, na Ibn as-Sunni nambari 637, na akasema Al-Arnautu kwamba mnyororo wake wa wapokezi ni sahihi katika kuelezea upokezaji wake katika At-Twahawiyyah uk. 133. Tazama pia: "Majma’ az-Zawa’id" 10/127.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/101, namba 6307.
Muslim 4/2076 namba 2702.
Abu Daud 2/85 kwa nambari 1517, na Tirmidhiy 5/569 kwa nambari 3577, na Al-Haakim na akasema kwamba ni sahihi na akakubaliana naye Adh-Dhahabiy 1/511, na amesema Albaniy kwamba ni sahihi, tazama: "Sahih At-Tirmidhiy" 3/182 na "Jaami' Al-Usul li Ahadith Ar-Rasuul (rehema na amani zimshukie)" 4/389-340 kwa uhakiki wa Al-Arnaawut.
At-Tirmidhi kwa nambari 3579, na An-Nasaai 1/279 kwa nambari 572, na Al-Haakim 1/309, na tazama: Sahihi Al-Tirmidhiy 3/183, na kitabu Jaamii Al-Usuul kwa uhakiki wa Al-Arnautu 4/144.
Muslim 1/350 nambari 482.
Ameipokea Muslim 4/2075 kwa nambari 2702, amesema Ibn Al-Athiir: "Hakika moyo wangu hufunikwa", yaani kufunikwa na kugubikwa, na makusudio yake ni: Kughafilika; kwa sababu yeye -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - alikuwa daima akiendelea kuzidisha utajo (dhikri), kujikurubisha na kudumu katika uangalizi, basi anapoghafilika na chochote katika hayo baadhi ya nyakati, au kusahau, hulihesabu kuwa ni kosa juu ya nafsi yake, hivyo hukimbilia kuomba msamaha. Angalia: Jaami'u Al-Usuul 4/386.
Bukhari 7/168 kwa nambari 6405, na Muslim 4/2071 kwa nambari 2691, na tazama: Fadhila za mwenye kuisema mara mia asubuhi na jioni uk. 65 katika kitabu hiki.
Bukhari 7/67 kwa nambari 6404, na Muslim kwa tamko lake 4/2071 kwa nambari 2693, na tazama: Fadhila za mwenye kuisema kwa siku mara mia moja. Dua nambari 93 uk. 66 katika kitabu hiki.
Bukhari 7/168 nambari 6404, na Muslim 4/2072 nambari 2694.
Muslim 4/2072 namba 2695.
Muslim 4/2073 namba 2698.
Ameipokea At-Tirmidhiy 5/511 kwa nambari 3464, na Al-Hakim 1/501, na akasema kwamba ni hadithi sahihi na Adh-Dhahabi akakubaliana naye, na tazama: Sahih Al-Jaami'i 5/531, na Sahih At-Tirmidhiy 3/160.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 11/213, namba 4206, na Muslim, 4/2076, namba 2704.
Muslim 3/1685 namba 2137.
Ameipokea Muslim 4/ 2072 kwa nambari 2696 na amezidisha Abu Daud 1/ 220 kwa nambari 832: Pindi alipoondoka bedui huyo, akasema Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Hakika ameujaza heri mkono wake."
Muslim 4/2073 kwa nambari 3697 na katika upokezi wake pia: "Hakika maneno hayo yanakukusanyia dunia yako na Akhera yako."
At-Tirmidhiy 5/462 nambari 3383, na Ibn Majah 2/1249 nambari 3800, na Al-Haakim 1/503 na akasema kwamba ni sahihi na akakubaliana naye Adhahabiy, na tazama: Sahihi Al-Jaamii 1/362.
Ameipokea Ahmad kwa nambari 513 kwa mpangilio wa Ahmad Shaakir, na tazama: Majmau Az-Zawaaid 1/297 na ameinasibisha Ibnu Hajar katika Buluugh Al-Maraam kutokana na riwaya ya Abuu Said kwa An-Nnasaai [katika kitabu Al-Kubraa] kwa nambari 10617 na akasema: Amesema Ibnu Hibbaan kwamba ni sahihi kwa nambari 840, na Al-Haakim 1/541.
Ameipokea Abuu Daud kwa tamko lake 2/81 kwa nambari 1502, na At-Tirmidhiy 5/521 kwa nambari 3486, na tazama: Swahihi Jaamiiy 4/271 kwa nambari 4865, na amesema Al-Albaani kwamba ni sahihi katika Sahihi sunani Abi Daud 1/411.
Bukhari na vile vile "Al-Fat-h" 10/88, namba 5623, na Muslim, 3/1595, namba 2012.
Kitabu cha asili kilichotajwa hapo juu kilichapishwa - na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu - pamoja na kueleza kwa kina upokezaji wa Hadithi zake, katika juzuu nne. Kitabu kiitwacho "Hisn Al-Muslim (Kinga Ya Muislamu)" kinapatikana katika juzuu yake ya kwanza na ya pili.