PHPWord

 

 

 

العَقِيدَةُ الصَّحِيْحَةُ وَمَا يُضَادُّهَا

 

ITIKADI SAHIHI NA YANAYOPINGANA NAYO

 

 

 

لِسَمَاحَةِ الشَّيْخِ العَلَّامَةِ

عَبْدِ العَزِيزِ بْنِ عَبْدِ اللهِ بْنِ بَازٍ

رَحِمَهُ اللهُ

 

Mtunzi Mheshimiwa, Sheikh,

Abdulaziz bin Abdillah bin Baaz

 

 

 


بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

Makala ya kwanza:

Itikadi sahihi na mambo yanayopingana nayo

Mtunzi Mheshimiwa, Sheikh,

Abdulaziz bin Abdillah bin Baaz

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu peke yake, na rehema na amani ziwe juu ya yule ambaye hakuna nabii atakayekuja baada yake, na ziwe juu ya watu wa familia yake na Maswahaba wake.

Ama baada ya kusema hayo: Kwa maana itikadi sahihi ndiyo asili ya dini ya Uislamu na msingi wa mila, nimeona kwamba ni muhimu nizungumzie maudhui haya, kuandika juu yake na kutunga makala katika kuyaeleza na kuyabainisha.

Na inavyofahamika kwa ushahidi wa kisheria utokanao na Qur'ani na Hadithi ni kuwa matendo na maneno yanakuwa sahihi na kukubaliwa ikiwa yatatokana na itikadi iliyo sahihi. Ama itikadi inapokuwa si sahihi, basi hubatilika kila kinachotokana nayo miongoni mwa matendo na maneno, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿...وَمَن يَكۡفُرۡ بِٱلۡإِيمَٰنِ فَقَدۡ حَبِطَ عَمَلُهُۥ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ﴾

"Na anayekufuru kuamini, basi hakika matendo yake yameharibika, naye Akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara." [Al-Maidah: 5]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَلَقَدۡ أُوحِيَ إِلَيۡكَ وَإِلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكَ لَئِنۡ أَشۡرَكۡتَ لَيَحۡبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ 65﴾

"Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa wale waliokuwa kabla yako: 'Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu, matendo yako yataanguka, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye kupata hasara.'" [Az-Zumar: 65]

Na aya zenye maana hii ni nyingi sana. Na kwa hakika kitabu cha Mwenyezi Mungu kilicho wazi na sunna za Mtume wake muaminifu, ziwe juu yake kutoka kwa Mola wake Mlezi rehema na amani bora zaidi, vimeashiria kwamba itikadi sahihi kwa muhutasari ni mambo sita: Kumuamini Mwenyezi Mungu, Malaika wake, Vitabu vyake, Mitume wake na Siku ya Mwisho, na kuamini mipango ya Mwenyezi Mungu ya heri na ya shari. Hivyo basi, mambo haya sita ndiyo msingi wa itikadi iliyo sahihi ambayo Kitabu kitukufu cha Mwenyezi Mungu kiliteremka nayo, na Mwenyezi Mungu akamtuma nayo Mtume wake Muhammad - rehema na amani ziwe juu yake.

 

Na umekuja ushahidi mwingi wa kuhusu misingi hii sita katika Kitabu (cha Mwenyezi Mungu) na Sunna sahihi, na miongoni mwa ushahidi huo kwa mfano tu ni huu ufuatao:

Kwanza: Ushahidi kutoka katika Kitabu; Ikiwa ni pamoja na kauli ya Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mtukufu:

﴿لَّيۡسَ ٱلۡبِرَّ أَن تُوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ قِبَلَ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَلَٰكِنَّ ٱلۡبِرَّ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ وَٱلۡكِتَٰبِ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ...﴾

"Sio wema tu peke yake kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi katika kusali, bali wema hasa ni wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii." [Al-Baqara: 177]

Na kauli yake aliyetakasika na kutukuka:

﴿ءَامَنَ ٱلرَّسُولُ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مِن رَّبِّهِۦ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَۚ كُلٌّ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَمَلَٰٓئِكَتِهِۦ وَكُتُبِهِۦ وَرُسُلِهِۦ لَا نُفَرِّقُ بَيۡنَ أَحَدٖ مِّن رُّسُلِهِ...﴾

"Mtume ameamini yale yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake Mlezi, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. (Wao husema) Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake." [Al-Baqara: 285]

 

Na kauli yake Mtukufu:

﴿يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ ءَامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلَّذِي نَزَّلَ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ مِن قَبۡلُۚ وَمَن يَكۡفُرۡ بِٱللَّهِ وَمَلَٰٓئِكَتِهِۦ وَكُتُبِهِۦ وَرُسُلِهِۦ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ فَقَدۡ ضَلَّ ضَلَٰلَۢا بَعِيدًا 136﴾

"Enyi mlioamini! Muaminini Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Kitabu alichokiteremsha juu ya Mtume wake, na Kitabu alichokiteremsha kabla yake. Na anayemkataa Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume wake, na Siku ya Mwisho, basi huyo amekwishapotea kupotea kwa mbali." [An-Nisaa: 136].

Na kauli yake Mtukufu:

﴿أَلَمۡ تَعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّ ذَٰلِكَ فِي كِتَٰبٍۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٞ 70﴾

"Je, hujui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi? Hakika hayo yamo Kitabuni. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi." [Al-Hajj: 70]

Pili: Ushahidi kutoka katika Sunna: Miongoni mwake ni hadithi sahihi na maarufu aliyoipokea imamu Muslimu katika sahihi yake kutoka katika hadithi ya kiongozi wa Waumini Omar ibni Khatwab - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kuwa: Jibriil, amani iwe juu yake, alimuuliza Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - kuhusu imani. Akamwambia: "Imani ni kumuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume wake, na Siku ya Mwisho, na kuamini mipango ya Mwenyezi Mungu, kheri yake na shari yake."1 Hadi mwisho wa Hadithi hii, na imepokelewa na masheke wawili (Bukhari na Muslim) - pamoja na kuwepo tofauti ndogo - kutoka kwa Hadithi ya Abu Hurairah, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi.

Na hii misingi sita kinatokana nayo kila kitu kilicho lazima kwa Muislamu kukiamini kuhusiana na Mwenyezi Mungu Mtukufu na katika jambo la kurudishwa kwa Mwenyezi Mungu, na mengineyo katika mambo yasiyoonekana, miongoni mwa yale aliyojulisha juu yake Mwenyezi Mungu na Mtume wake, rehema na amani ziwe juu yake.

Ufafanuzi wa misingi hii sita ni kama ifuatavyo:

Msingi wa kwanza: Kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu. Inajumuisha mambo kadhaa; ikiwa ni pamoja na:

Na inajumuisha mambo kadhaa; miongoni mwayo: Kuamini kwamba Yeye ndiye Mungu wa kweli anayestahiki kuabudiwa mbali na kila kisichokuwa yeye, kwa kuwa yeye ndiye Muumba wa waja, Mwenye kuwatendea wema, Mwenye kusimamia riziki zao, Mwenye kujua mambo yao ya siri na ya wazi, Mwenye uwezo wa kumlipa thawabu mtiifu wao na kumuadhibu mwenye kuasi miongoni mwao.

Mwenyezi Mungu aliumba vizito viwili (majini na wanadamu) kwa ajili ya ibada hii na akawaamrisha kuifanya, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ 56 مَآ أُرِيدُ مِنۡهُم مِّن رِّزۡقٖ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطۡعِمُونِ 57 إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلۡقُوَّةِ ٱلۡمَتِينُ 58﴾

"Nami sikuwaumba majini na watu isipokuwa waniabudu Mimi.

Sitaki kutoka kwao riziki wala sitaki wanilishe.

Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti." [Adh-Dhariyat: 56-58].

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱعۡبُدُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ 21 ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ فِرَٰشٗا وَٱلسَّمَآءَ بِنَآءٗ وَأَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجَ بِهِۦ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ رِزۡقٗا لَّكُمۡۖ فَلَا تَجۡعَلُواْ لِلَّهِ أَندَادٗا وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ 22﴾

"Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Mlezi aliye waumba nyinyi na wale wa kabla yenu, ili mpate kuwa wacha Mungu.

(Mwenyezi Mungu) ambaye amewafanyia hii ardhi kuwa kama tandiko, na mbingu kama paa, na akateremsha maji kutoka mbinguni, na kwayo akatoa matunda yawe riziki zenu. Basi msimfanyie Mwenyezi Mungu washirika, na hali nyinyi mnajua." [Al-Baqara: 21-22].

Na kwa hakika Mwenyezi Mungu aliwatuma Mitume na akateremsha Vitabu kwa ajili ya kubainisha haki na kuilingania, na kutahadharisha yote yanayopingana nayo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu aliyetakasika, Mtukufu:

﴿وَلَقَدۡ بَعَثۡنَا فِي كُلِّ أُمَّةٖ رَّسُولًا أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱجۡتَنِبُواْ ٱلطَّٰغُوتَ...﴾

"Na kwa hakika tulituma katika kila umma mtume, ya kuwa wamuabudu Mwenyezi Mungu na wajiepushe na kila kinachoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu." [An-Nahli: 36].

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِيٓ إِلَيۡهِ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعۡبُدُونِ 25﴾

"Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hakuna mungu isipokuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu." [Al-Anbiya: 25].

Na amesema Mwenye nguvu na utukufu:

 

﴿الر كِتَابٌ أُحْكِمَتْ آيَاتُهُ ثُمَّ فُصِّلَتْ مِنْ لَدُنْ حَكِيمٍ خَبِيرٍ1 أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا اللَّهَ إِنَّنِي لَكُمْ مِنْهُ نَذِيرٌ وَبَشِيرٌ2﴾

"Alif Lam Ra. Hiki ni Kitabu ambacho Aya zake zimewekwa wazi, kisha zikapambanuliwa, kilichotoka kwa Mwenye Hekima na Mwenye habari zote.

Ili msimuabudu isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi kwenu ni muonyaji na mbashiri nitokae kwake." [Huud: 1-2].

Na uhakika wa ibada hii ni katika kumpwekesha Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka kwa mambo yote wanayotumia waja kuabudia miongoni mwa dua, hofu, kutaraji, kuswali, kufunga, kuchinja wanyama, kuweka nadhiri na mengineyo miongoni mwa ibada zinazofanywa kwa kumnyenyekea yeye, kumtaka Yeye tu na kumuogopa pamoja na kumpenda kikamilifu yeye aliyetakasika na kujishusha chini mbele ya ukuu wake.

Na mwenye kutafakari Qur'ani tukufu, atapata kwamba aya zake nyingi ziliteremka kuhusiana na misingi hii mitukufu, kama ilivyo katika maneno yake Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka:

﴿إِنَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ فَٱعۡبُدِ ٱللَّهَ مُخۡلِصٗا لَّهُ ٱلدِّينَ فَاعْبُدِ اللَّهَ مُخْلِصًا لَهُ الدِّينَ 2 أَلَا لِلَّهِ الدِّينُ الْخَالِصُ وَٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءَ مَا نَعۡبُدُهُمۡ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَآ إِلَى ٱللَّهِ زُلۡفَىٰٓ إِنَّ ٱللَّهَ يَحۡكُمُ بَيۡنَهُمۡ فِي مَا هُمۡ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي مَنۡ هُوَ كَٰذِبٞ كَفَّارٞ3﴾

"Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu hiki kwa Haki. Basi muabudu Mwenyezi Mungu ukimsafia Dini Yeye tu.

Sikilizeni. Hakika Dini Safi ni ya Mwenyezi Mungu tu. Na wale wanaowafanya wenginewe kuwa ni walinzi wakisema: 'Sisi hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu', hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika yale wanayo hitilafiana. Hakika Mwenyezi Mungu hamuongoi aliye muongo kafiri." [Az-Zumar: 3-2]

Na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّآ إِيَّاهُ...﴾

"Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote isipokuwa Yeye." [Al Israai: 23].

Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu:

﴿فَٱدۡعُواْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡكَٰفِرُونَ14﴾

"Basi muombeni Mwenyezi Mungu mkimsafia Dini Yeye tu, hata kama watachukia makafiri." [Ghaafir: 14]

Vile vile, mwenye kutafakari Sunna ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, atapata kwamba msingi huu mkubwa pia umepewa kipaumbele. Miongoni mwa hayo ni yale yaliyosimuliwa katika Sahihi mbili kutoka kwa Mua'adh - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwamba Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alisema: "Haki ya Mwenyezi Mungu juu ya waja wake, ni wamuabudu yeye na wala wasimshirikishe na kitu chochote."2

Na huingia vilevile katika kumuamini Mwenyezi Mungu: Kuyaamini mambo yote aliyoyawajibisha Mwenyezi Mungu kwa waja wake, na akawalazimisha kuyafanya, miongoni mwayo ni nguzo tano za Uislamu zilizo maarufu.

Na hizo nguzo tano ni: Kushuhudia kuwa hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kusimamisha swala, na kutowa Zaka, na kufunga Ramadhani, na kuhiji Nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu kwa yule awezaye njia ya kuiendea, na mambo mengine yasiyokuwa hayo miongoni mwa mambo yaliyolazimishwa ambayo yamekuja katika sheria iliyo nzuri.

Na nguzo muhimu zaidi na tukufu katika hizi nguzo ni: Kushuhudia kuwa hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Tamko hili la shahada linahitajia kuifanya ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake na kumkataa asiyekuwa yeye, na hii ndiyo maana ya (Laailaha illallahu). Kwani maana yake -kama walivyosema wanazuoni Mwenyezi Mungu awarehemu- ni: Hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake. Na kwa mujibu wa maana hiyo, basi kila kinachoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu - awe ni mwanadamu au Malaika au jini au au yoyote asiyekuwa hao - ni muabudiwa batili, na mwenye kuabudiwa kwa haki ni Mwenyezi Mungu peke yake hana mshirika wake kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿ذَٰلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡحَقُّ وَأَنَّ مَا يَدۡعُونَ مِن دُونِهِۦ هُوَ ٱلۡبَٰطِلُ...﴾

"Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu ndiye wa haki, na kwamba kila wanachokiabudu kinyume na yeye ni batili." [Al-Hajj: 62].

Na imeshatangulia kuwekwa wazi kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwaumba majini na watu kwa ajili ya msingi huu wa asili, na akawaamrisha kushikamana na msingi huo, na akatuma kwa ajili hiyo Mitume wake, na akateremsha kwa ajili hiyo Vitabu vyake. Hivyo basi ni wajibu kwa mja kulifikiria hilo vizuri na kulizingatia sana; ili ikuwiye wazi namna gani walivyo tumbukia Waislamu wengi katika ujinga mkubwa wa kutojuwa msingi huu; mpaka wakafikia kiwango cha kuabudu wengineo pamoja na Mwenyezi Mungu, na wakawafanyia wengineo haki yake ya kipekee. Basi Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuombwa msaada.

Na miongoni mwa kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kuamini kuwa Yeye ndiye Muumba wa ulimwengu, Mwenye kupanga mambo yao na Mwenye kuwaendesha kwa elimu yake na uwezo wake kama anavyotaka Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwamba Yeye ndiye Mmiliki wa dunia na akhera, na ndiye Mola Mlezi wa walimwengu wote, hakuna muumba asiye kuwa Yeye wala hakuna Mola Mlezi asiyekuwa Yeye. Na kwamba yeye alituma Mitume na akateremsha Vitabu ili kuwafanya waja kuwa wema na kuwalingania kwenye mambo yenye wokovu wao na kutengenea kwao duniani na akhera. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu hana mshirika yeyote katika hayo yote. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿ٱللَّهُ خَٰلِقُ كُلِّ شَيۡءٖۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٞ 62﴾

"Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa kila kitu, na Yeye ndiye Mlinzi juu ya kila kitu." [Az-Zumar: 62].

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿إِنَّ رَبَّكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يُغۡشِي ٱلَّيۡلَ ٱلنَّهَارَ يَطۡلُبُهُۥ حَثِيثٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ وَٱلنُّجُومَ مُسَخَّرَٰتِۭ بِأَمۡرِهِۦٓۗ أَلَا لَهُ ٱلۡخَلۡقُ وَٱلۡأَمۡرُۗ تَبَارَكَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ54﴾

"Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akainuka juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zilizotiishwa kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba ni kwake, na amri (ni yake). Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote." [Al-A'araf: 54]

Na vilevile miongoni mwa kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu: Ni kuyaamini majina yake mazuri na sifa zake tukufu zilizokuja katika Kitabu chake kitukufu, na zilizothibiti kutoka kwa Mtume wake muaminifu, pasina kubadilisha, kupinga, kutafuta kujua namna zilivyo haswa wala kufananisha.

﴿...لَيۡسَ كَمِثۡلِهِۦ شَيۡءٞۖ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ﴾

"Hakuna kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona." [Ash-Shuraa: 11].

Hivyo, ni wajibu kuyapitisha kama yalivyokuja bila kutafuta

kujua namna yalivyo haswa, pamoja na kuamini maana tukufu ambazo yaliashiria, ambazo ni sifa za Mwenyezi Mungu mwenye nguvu na utukufu, na ni wajibu kumuelezea Yeye Mtukufu kwa sifa hizo kwa namna inayomfailia pasina ya kumfananisha na kiumbe chake chochote kama sifa zake zozote. Kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Na amesema Mwenye nguvu na utukufu:

﴿فَلَا تَضۡرِبُواْ لِلَّهِ ٱلۡأَمۡثَالَۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ74﴾

"Basi msimpigie Mwenyezi Mungu mifano. Kwa hakika yeye anajuwa, na nyinyi hamjui kitu chochote." [An-Nahli: 74].

Na hii ndiyo itikadi sahihi ya Ahlussunna waljamaa miongoni mwa Maswahaba wa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - na wale waliofuata baada yao kwa wema, na ndiyo itikadi aliyoinukuu imamu Abul Hasani Al-ash-'ariy katika kitabu chake, Mwenyezi Mungu amrehemu, kitabu kiitwacho "Makala mbalimbali" kutoka kwa watu wa hadithi na sunna" na pia waliinukuu wengineo miongoni mwa watu wenye elimu na imani.

Alisema Al-Awzaaiy Mwenyezi Mungu amrehemu: Aliulizwa imamu Zuhriy na Maq-huul kuhusu aya zinazohusiana na sifa za Mwenyezi Mungu, wakasema: "Zipitisheni kama zilivyokuja."3

 

 

 

 

 

Na akasema Al-Awzaaiy vilevile - Mwenyezi Mungu amrehemu: Tulikuwa tukisema ilhali wale waliokuja baada ya Maswahaba bado wako hai: 'Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu yupo juu ya Kiti chake cha Enzi, na tunaamini sifa zote zilizopokewa katika hadithi (za Mtume)."4

Na alisema Al-Waliid bin Muslim -Mwenyezi mungu amrehemu- "Aliulizwa Imamu Maalik, Auzaaiy, Al-laithiy ibnu Saad na Sufiani Al-thauriy -Mwenyezi Mungu awarehemu- kuhusu habari zilizopokelewa kuhusu sifa za Mwenyezi Mungu wakasema wote kuwa: 'Zipitisheni kama zilivyokuja bila ya kutafuta kujua namna zilivyo haswa.'"5

Na alipoulizwa Rabii'a ibn Abdurahmani, sheikh wa imamu Maalik, Mwenyezi Mungu amrehemu yeye na sheikh wake, kuhusu kuwa juu kwa Mwenyezi Mungu, akasema: 'Kuwa juu kwake kuna fahamika, na namna yake hasa haifahamiki, na lililo kwa Mwenyezi Mungu ni kutuma ujumbe, nao ni wajibu wa Mtume ni kufikisha kwa uwazi, na wajibu wetu sisi ni kusadiki.'6 Na alipoulizwa imamu Maalik -Mwenyezi Mungu amrehemu- kuhusu hilo alisema: "Kuwa juu kwake kunafahamika, na namna yake hasa haifahamiki, na kuamini jambo hilo ni wajibu, na kuuliza namna yake ni uzushi." Kisha akamwambia muulizaji: "Ninakuona kuwa wewe ni mtu muovu!" Kisha akatoa amri na akatolewa mahali pale.7 Na imepokelewa maana hii vilevile kutoka kwa mama wa waumini Ummu Salama - radhi za Mwenyezi Mungu - zimfikie.8

Na amesema imamu Abuu Abdurahman ibnu Mubaaraka -rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa: "Tunamjua Mola wetu Mlezi Mtukufu kuwa Yeye yupo juu ya mbingu zake na yupo juu ya Kiti chake cha Enzi hali yakujitenga na viumbe wake."9

Na maneno ya maulamaa kwenye mlango huu ni mengi sana hatuwezi kuyanukuu yote katika muhadhara huu. Mwenye kutaka kulifuatilia hilo zaidi, basi ayarejelee yaliyoandikwa na maulamaa wa sunna katika mlango huu, mfano kitabu kiitwacho "As-Sunnah" cha mtunzi aitwaye Abdullah ibn imamu Ahmad, na pia kitabu kiitwacho "At-Tauhiid" cha mtunzi aitwaye Al-imamu al-jaliil Muhammad ibn Khuzaimata, na kitabu kiitwacho "As-Sunna" cha mtunzi aitwaye Abulqaasim Al-lalkaaiy At-twabariy, na kitabu kiitwacho "As-Sunna" cha mtunzi aitwaye Abuubakar ibn Aaswim, na majibu ya sheikhul -islaam ibn Taimiya kujibu watu wa Hamaat, nalo ni jibu zuri lenye faida kubwa. Ameweka wazi humo -Mwenyezi Mungu amrehemu- itikadi ya Ahlusunnah, na akanukuu humo mengi ya maneno yao, na ushahidi wa kisheria na wa kiakili juu ya usahihi wa yale waliyoyasema Ahlusunnah, na ubatili wa yale waliyo yasema wagomvi wao.

Na hivi ndivyo ilivyokuwa risala yake iliyoitwa Tadmuuriyya. Kwani kwa hakika alieleza humo kwa undani na akaweka wazi itikadi ya ahlusunnah waljamaa kwa kutumia ushahidi ulionukuliwa kutoka katika Kitabu na Sunna na pia ushahidi wa kiakili na kujibu hoja za wapinzani majibu yenye kuweka wazi haki na kuibomoa batili kwa kila mwenye kulitazama hilo miongoni mwa wenye elimu kwa lengo zuri na kutaka kuijuwa haki. Na kwa ufupi ni kwamba: Itikadi ya Ahlusunnah wal-jamaa katika mlango wa majina ya Mwenyezi Mungu na sifa zake, ni kwamba wame mthibitishia Mwenyezi Mungu Mtukufu kile alicho kithibitisha yeye mwenyewe katika Kitabu chake, au kamthibitishia katika sunna zake Mtume wake Muhammad rehema na amani ziwe juu yake. Walimthibitishia bila ya kumfananisha, na wakamtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu kutokana na kufanana na viumbe wake utakaso ulio mbali na kuzikataa sifa zake. Kwa hivyo, wakafanikiwa kwa kusalimika kutokana na mgongano. Waliufanyia kazi ushahidi wote kwa kuwezeshwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa sababu ni katika sunna na kawaida ya Mwenyezi Mungu kumuwezesha mtu aliyekamatana na haki ambayo amewatuma nayo Mitume wake, na katowa kwa ajili ya hilo bidii zake, na akamkusudia Mwenyezi Mungu tu katika kutafuta kwake, kwamba Mwenyezi Mungu humuwezesha kuipata haki na kudhihiri ushahidi wake kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿بَلۡ نَقۡذِفُ بِٱلۡحَقِّ عَلَى ٱلۡبَٰطِلِ فَيَدۡمَغُهُۥ فَإِذَا هُوَ زَاهِقٞ...﴾

"Bali (tulifanyalo ni hili) tunaitupa kweli juu ya batili; ikaivunjilia mbali, na mara ikatoweka." [Surat Al-Anbiyaa: 18].

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَلَا يَأۡتُونَكَ بِمَثَلٍ إِلَّا جِئۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَأَحۡسَنَ تَفۡسِيرًا33﴾

"Na hawakujii, ewe Mtume, hawa washirikina na hoja yoyote au utata wowote isipokuwa tutakuletea majibu ya ukweli na ufafanuzi wake mzuri zaidi." [Surat Al-Furqan: 33]

 

 

Na ama yule ambaye amekwenda kinyume na itikali ya Ahlusunnah kwa namna wanavyoitakidi katika mlango wa majina na sifa, huyo hapana shaka ni lazima atakuwa amekwenda kinyume na ushahidi wa Qur'ani na Sunna na ushahidi wa kiakili; na atakuwa ni mwenye kukinzana waziwazi na kila anachokithibitisha na kukikataa. Na ametaja Al-haafidh ibnu Kathiir -Mwenyezi Mungu amrehemu- katika tafsiri yake maarufu, kataja maneno mazuri katika maudhui hii, pale aliposema kuhusu maneno ya Mwenyezi Mungu -Mwenye nguvu na utukufu:

﴿إِنَّ رَبَّكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِ...﴾

"Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akainuka juu ya Kiti cha Enzi." [Al-A'araf: 54]

Na inapendeza kuyanukuu maneno hayo hapa kutokana na faida zake kubwa. Amesema ibnu Kathiir -Mwenyezi Mungu amrehemu- maneno ambayo maandishi yake yanasema hivi:

Watu kwenye suala hili wana maneno mengi sana, na hapa siyo mahala sahihi pa kuyakunjua maneno hayo. Sisi katika suala hili tunafuata madhehebu ya wema waliotangulia: Maaliki, Auzaaiy, At-Thauriy, Al-laithiy ibnu Saad, Ash-Shaafiiy, Ahmad ibnu Hanbal na Is-haqa ibnu Rahawaihi na wengineo miongoni mwa maimamu wa Waislamu wazamani na wa sasa. Nao ni msimamo wa kuyapitisha kama yalivyokuja pasina kutafuta kujua namna yalivyo haswa wala kuyafananisha wala kuyakataa. Na maana ya dhahiri inayotokea kwenye akili za wenye kuyafananisha haiingiliani na Mwenyezi Mungu.

Kwa hakika Mwenyezi Mungu hafanani na chochote katika viumbe wake.

﴿...لَيۡسَ كَمِثۡلِهِۦ شَيۡءٞۖ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ﴾

"Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona." [Ash-Shuraa: 11]. Bali uhakika wa jambo hilo ni kama walivyokwisha sema maimamu - miongoni mwao ni Nu'aimu ibnu Hammad Al-khuzaaiy, sheikh wa imamu Bukhariy alisema: "Yeyote atakaye mfananisha Mwenyezi Mungu na viumbe vyake, basi amekufuru. Na mwenye kupinga sifa aliyojisifu kwayo Mwenyezi Mungu, basi hakika amekufuru.10 Na hakuna kufananisha kokote katika sifa ambazo Mwenyezi Mungu alijisifia mwenyewe wala sifa ambazo amesifiwa kwazo na Mtume wake. Kwa hivyo, mwenye kumthibitishia Mwenyezi Mungu Mtukufu sifa zilizopokelewa katika aya zilizo waziwazi na hadithi sahihi kwa njia inayo endana na utukufu wa Mwenyezi Mungu, na aka mkanushia Mwenyezi Mungu mapungufu, basi hakika huyo atakuwa amefuata njia ya uongofu."11 mwisho wa kunukuu maneno ya Ibnu Kathiir Mwenyezi Mungu amrehemu.

Na huingia vilevile katika imani ya kumuamini Mwenyezi Mungu: kuwa na itikadi kwamba imani sahihi inakusanya maneno na vitendo. Imani hiyo inazidi kwa kutii maamrisho, na hupunguwa kwa kufanya madhambi. Na haifai kumkufurisha Muislamu kwa kufanya kitu katika madhambi ambayo siyo ushirikina wala kufuru, kama vile kufanya zinaa, kuiba, kula riba, kunywa pombe, kutowatendea wema wazazi wawili na mengineyo katika madhambi makubwa ikiwa hakuyafanya kuwa ni halali. Hili ni kwa mujibu maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَغۡفِرُ أَن يُشۡرَكَ بِهِۦ وَيَغۡفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَآءُ...﴾

"Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi kushirikishwa, na husamehe madhambi yasiyokuwa shirki kwa amtakaye." [An-Nisaa: 48] Na kwa uthibitisho wa hadithi zilizopokelewa na wengi kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- miongoni mwazo ni maneno yake: "Hakika Mwenyezi Mungu atamtoa Motoni yeyote atakayekuwa katika moyo wake na imani yenye uzito sawa na punje ya haradali."12

 

Msingi wa pili: Kuwaamini Malaika, na imani hii inakusanya mambo mawili:

Na inakusanya mambo mawili: Jambo la kwanza: kuwaamini Malaika kwa ujumla; nako ni kuamini kuwa Mwenyezi Mungu ana Malaika amewaumba ili wamtii na akawasifia kuwa wao:

﴿وَقَالُواْ ٱتَّخَذَ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَلَدٗاۗ سُبۡحَٰنَهُۥۚ بَلۡ عِبَادٞ مُّكۡرَمُونَ 26 لَا يَسۡبِقُونَهُۥ بِٱلۡقَوۡلِ وَهُم بِأَمۡرِهِۦ يَعۡمَلُونَ27 يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡ وَلَا يَشۡفَعُونَ إِلَّا لِمَنِ ٱرۡتَضَىٰ وَهُم مِّنۡ خَشۡيَتِهِۦ مُشۡفِقُونَ28﴾

"Na wanasema: 'Arrahman (Mwingi wa rehema), ana mwana!' Subhanahu (ametakasika mbali na hayo)! Bali hao (wanaowaita wana) ni waja waliotukuzwa.

"Hawamtangulii kwa neno nao wanafanya kwa amri zake.

"Mwenyezi Mungu anayajuwa yaliyo mbele yao (hao Malaika) na yaliyo nyuma yao (hao Malaika) wala hawamuombei yeyote ila yule anayemridhia Mwenyezi Mungu, nao kwa sababu ya kumuogopa wananyeyekea." [Surat Al-Anbiyaa: 26-28]

Na wao wapo aina nyingi. Miongoni mwao kuna wale waliopewa jukumu la kubeba Kiti cha Enzi, na wengine ni walinzi wa Pepo na Moto, na wengine wamepewa jukumu la kuyahifadhi matendo ya waja. Jambo la pili: Kuwaamini Malaika mmoja mmoja kwa kina. Na hilo ni kwa kuamini jina la Malaika aliloitwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kama vile jina la Jibril aliyepewa jukumu la kubeba Ufunuo wa Mwenyezi Mungu (wahyi), na Mikaili aliyepewa jukumu la kunyesheleza mvua, na Malik mlinzi wa Moto, na Israfiil aliyepewa jukumu la kupuliza parapanda. Kama ulivyokuja utajo wao katika Hadithi sahihi, miongoni mwa hizo hadithi ni hadithi iliyothibiti katika sahihi kutoka kwa Aisha -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amesema: "Wameumbwa Malaika kutokana na nuru, na wameumbwa majini kutokana moto halisi, na ameumbwa Adam kutokana na udongo kama mlivyoelezewa."13 Ameipokea Imamu Muslim katika Sahihi yake.

 

 

 

 

Msingi wa tatu: Kuamini Vitabu. Na hili linakusanya vile vile mambo mawili:

Jmabo la kwanza: Kuviamini Vitabu kwa ujumla. Hilo ni kwa kuamini kwamba Mwenyezi Mungu aliteremsha Vitabu kwa Manabii na Mitume wake; ili kuweka wazi haki yake, na kulingania hiyo haki kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَأَنزَلۡنَا مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمِيزَانَ لِيَقُومَ ٱلنَّاسُ بِٱلۡقِسۡطِ...﴾

"Kwa hakika tuliwatuma Mitume wetu kwa hoja za waziwazi, na tukateremsha Kitabu pamoja nao na Mizani, ili watu wasimamie uadilifu." [Al Hadid: 25]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿كَانَ ٱلنَّاسُ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَبَعَثَ ٱللَّهُ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ وَأَنزَلَ مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ فِيمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ...﴾

"Watu wote walikuwa ni umma mmoja. Basi Mwenyezi Mungu akatuma Manabii wabashiri na waonyaji. Na pamoja nao akateremsha Kitabu kwa Haki, ili kihukumu baina ya watu katika yale waliyohitilafiana. Na wala hawakuhitalifiana ndani yake ila wale waliopewa Kitabu hicho..." [Al-Baqara: 213]

 

 

Jambo la pili: Kuviamini Vitabu kimoja kimoja; nako ni kuamini vitabu alivyoviita Mwenyezi Mungu kwa majina yake, kama vile Taurati, Injili, Zaburi, na Qur'ani. Na tunaitakidi kwamba Qur'ani ndiyo kitabu bora zaidi na cha mwisho. Nayo Qur'ani ndiyo yenye kuvihukumu vitabu vyote na yenye kuvisadikisha. Na Qur'ani ndicho kitabu ambacho yaupasa umma wote kukifuata na kuhukumu kwacho; pamoja na kuhukumu kwa habari sahihi zilizopokelewa kutoka kwa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake. Kwa sababu, Mwenyezi Mungu Mtukufu alimtuma Mtume wake Muhammad -rehema na mani ziwe juu yake- kwa majini na watu, na akamteremshia hii Qur'ani ili awahukumu kwayo, na kaifanya hii Qur'ani kuwa ni ponyo ya maradhi ya nyoyo, na ubainisho wa kila kitu, na ni muongozo na rehema kwa Waumini, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَهَٰذَا كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ مُبَارَكٞ فَٱتَّبِعُوهُ وَٱتَّقُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ155﴾

"Na hiki ni Kitabu tulichokiteremsha, kilichobarikiwa. Basi kifuateni, na mcheni Mungu, ili mrehemewe." [Al-An'aam: 155]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿...وَنَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ تِبۡيَٰنٗا لِّكُلِّ شَيۡءٖ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٗ وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُسۡلِمِينَ﴾

 

"Na tumeteremsha kwako Kitabu, kiwe ni upambanuzi wa kila kitu, na muongozo na rehema, na bishara njema kwa Waislamu." [An-Nahli: 89]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿قُلۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنِّي رَسُولُ ٱللَّهِ إِلَيۡكُمۡ جَمِيعًا ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِ ٱلنَّبِيِّ ٱلۡأُمِّيِّ ٱلَّذِي يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَكَلِمَٰتِهِۦ وَٱتَّبِعُوهُ لَعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ158﴾

"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliyetumwa na Mwenyezi Mungu Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Hakuna mungu ila Yeye anayehuisha na anayefisha. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake asiyejua kusoma na kuandika, ambaye anamuamini Mwenyezi Mungu na maneno yake. Na mfuateni yeye ili mpate kuongoka." Na aya zenye maana hii ni nyingi.

Nguzo ya nne: Kuwaamini Mitume

Na inakusanya mambo mawili: Jambo la kwanza: Kuwaamini Mitume kwa ujumla. Nako ni kuamini kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwatumia waja wake Mitume kutoka miongoni mwao, ili watoe habari njema na waonye, na walinganizi wa haki. Kwa hivyo, yeyote atakayewakubali, atafaulu kwa kuwa na furaha. Na atakayewapinga, atastahiki hasara na majuto. Na wa mwisho wao na mbora wao zaidi ni Mtume Muhammad ibnu Abdillah -rehema na amani ziwe juu yake- kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَلَقَدۡ بَعَثۡنَا فِي كُلِّ أُمَّةٖ رَّسُولًا أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱجۡتَنِبُواْ ٱلطَّٰغُوتَ...﴾

"Na kwa hakika tulituma katika kila umma Mtume, ya kuwa muabuduni Mwenyezi Mungu na jiepusheni na kila kinachoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu." [An-Nahli: 36]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿رُّسُلٗا مُّبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ لِئَلَّا يَكُونَ لِلنَّاسِ عَلَى ٱللَّهِ حُجَّةُۢ بَعۡدَ ٱلرُّسُلِ...﴾

"Mitume hao ni wabashiri na waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kuletewa Mitume." [An-Nisaa: 165] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿مَّا كَانَ مُحَمَّدٌ أَبَآ أَحَدٖ مِّن رِّجَالِكُمۡ وَلَٰكِن رَّسُولَ ٱللَّهِ وَخَاتَمَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ...﴾

"Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa Manabii." [Al-Ahzab: 40].

Jambo la pili: Kuwaamini Mitume mmoja mmoja. Nako ni kuwaamini Mitume mmoja mmoja na kuwaita kwa majina yao kama alivyowaita Mwenyezi Mungu au kama yalivyothibiti majina yao kutoka kwa Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake; Kama vile Nuuh, Huud, Swaaleh, Ibrahim, na wengineo rehema na amani za Mwenyezi na Mungu ziwe juu yao na juu watu wa familia zao na wafuasi wao.

Msingi wa tano: Kuamini siku ya Mwisho

Msingi huu unajumuisha:

Kuamini kila kitu ambacho Mwenyezi Mungu na Mtume wake rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake walifahamisha kuwa kitatokea baada ya kufa, kama vile mtihani wa kaburini, adhabu na neema zake, na yale yatakayokuwa siku ya Kiyama miongoni mwa mambo ya kutisha na ya shida, na kutakuwepo na Njia (Swiraat), mizani, kuhesabiwa, kulipwa na kusambazwa vitabu vya matendo kwa watu. Basi kutakuwa na mwenye kukichukuwa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia na mwenye kukichukuwa kwa mkono wake wa kushoto au kwa nyuma ya mgongo wake.

Na inaingia vilevile katika imani, kuamini uwepo hodhi ya kunywa maji ya Mtume wetu Muhammad rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ambayo watu watakwenda kunywa maji humo, na kuamini uwepo wa Pepo na Moto, Waumini kumuona Mola wao Mlezi Mtukufu na kuwasemesha wao, na kuamini mengineyo yaliyokuja katika Qur'ani na hadithi sahihi kutoka kwa Mtume rehema amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Ni wajibu kuamini hayo yote na kuyasadikisha kwa namna alivyoweka wazi Mwenyezi Mungu na Mtume wake rehema na mani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Msingi wa sita: Kuamini mipango ya Mwenyezi Mungu

Na inaingia ndani yake kuyaamini mambo manne:

Jambo la kwanza: Kuamini kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu, hakika alikwishajuwa yaliyokuwepo na yaliyopo sasa. Na alijua hali za waja wake, riziki zao, vifo vyao, matendo yao na mengineyo katika mambo yao. Kwa hivyo, hakifichikani kitu chochote kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿...وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ﴾

"Na jueni ya kuwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua zaidi kila kitu." [Al-Baqara: 231] Na amesema Mwenye Nguvu na utukufu:

﴿...لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ وَأَنَّ ٱللَّهَ قَدۡ أَحَاطَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عِلۡمَۢا﴾

"Ili mjue kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu, na kwamba Mwenyezi Mungu amekizingira kila kitu kukijua vilivyo kwa elimu yake." [At-Talaq: 12].

 

 

Jambo la pili: Kuamini kwamba Mwenyezi Mungu alikwishaandika kila alilolipanga na kulipitisha; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿قَدۡ عَلِمۡنَا مَا تَنقُصُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۡهُمۡۖ وَعِندَنَا كِتَٰبٌ حَفِيظُۢ 4﴾

"Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinachopunguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinachohifadhi yote." [Qaaf: 4]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿...وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ فِيٓ إِمَامٖ مُّبِينٖ﴾

"Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asili lenye kubainisha." [Yasin: 12]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿أَلَمۡ تَعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّ ذَٰلِكَ فِي كِتَٰبٍۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٞ70﴾

"Je, hujui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi? Hakika hayo yamo Kitabuni. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi." [Al-Hajj: 70]

Jambo la tatu: Kuamini matashi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu anayoyapitisha. Alitakalo liwe, linakuwa. Na asilolitaka lisiwe, basi haliwi. Kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿...إِنَّ ٱللَّهَ يَفۡعَلُ مَا يَشَآءُ﴾

"Hakika Mwenyezi Mungu hufanya atakalo." [Al-Hajj: 18]. Na amesema Mwenye Nguvu na utukufu:

﴿إِنَّمَآ أَمۡرُهُۥٓ إِذَآ أَرَادَ شَيۡـًٔا أَن يَقُولَ لَهُۥ كُن فَيَكُونُ82﴾

"Hakika amri yake anapotaka kitu kiwe, ni kukiambia, "Kuwa!" Na kikawa." [Yasin: 82]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ29﴾

"Wala nyinyi hamtataka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote."

[At-Takwir: 29].

Jambo la Nne: Kuamini uumbaji wa Mwenyezi Mungu Mtukufu wa viumbe vyote vilivyopo. Hivyo basi, hakuna muumba zaidi yake Yeye, na wala hakuna mola mlezi asiyekuwa Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿ٱللَّهُ خَٰلِقُ كُلِّ شَيۡءٖۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٞ62﴾

"Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa kila kitu, na Yeye ndiye Mlinzi juu ya kila kitu." [Az-Zumar: 62] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡۚ هَلۡ مِنۡ خَٰلِقٍ غَيۡرُ ٱللَّهِ يَرۡزُقُكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِۚ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ فَأَنَّىٰ تُؤۡفَكُونَ3﴾

"Enyi watu, kumbukeni neema za Mwenyezi Mungu juu yenu. Ati yupo muumba mwengine asiyekuwa Mwenyezi Mungu anayekupeni riziki kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Hapana mungu ila Yeye tu. Basi wapi mnakogeuzwa?" [Faatir: 3]

Basi kuamini mipango ya Mwenyezi Mungu kuna jumuisha kuamini haya mambo manne yote kama ilivyo katika itikadi ya Ahlussunnah waljamaa; tofauti na wenye kupinga baadhi ya hayo mambo katika watu wa uzushi (Bidaa).

Na miongoni mwa mambo muhimu katika itikadi sahihi ambayo wanayaitakidi Ahlussunnah waljamaa ni kupenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuchukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kuwafanya vipenzi na kusaidiana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuwafanya uadui kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Hii ndiyo itikadi inayoitwa kupenda na kuchukia, na itikadi hii ni katika kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Hivyo basi, Muumini huwapenda Waumini wenzake na huwafanya ni vipenzi, na huwachukia makafiri na kuwafanyia uadui. Na Waumini wakuu sana katika umma huu ni Maswahaba wa Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kama ilivyopitishwa kwa Ahlussunna waljamaa. Wao wanawapenda na wanawafanya kuwa ni vipenzi vyao, na wanaitakidi kuwa hao Maswahaba ndio watu bora zaidi baada ya Mitume, kwa maneno ya Mtume rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Karne iliyo bora zaidi ni karne yangu, kisha karne ya waliofuata, kisha waliofuata."14 Wanachuoni wamekubaliana kwamba hadithi hii ni sahihi.

Na wanaitakidi kuwa mbora wao zaidi ni Abubakari As-Swiddiq, kisha Umar Al-Faaruuq, kisha Uthman Dhunnurain, kisha Ali Al-murtadhwa radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote. Kisha wanafuatia baada yao waliosalia miongoni mwa wale kumi waliobashiriwa Pepo, kisha Maswahaba wote radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao. Wananyamazia ugomvi uliokuwa kati ya Maswahaba, na wanaitakidi kuwa wao katika ugomvi huo walikuwa ni wenye kujitahidi. Yeyote aliyefikia usahihi, ana malipo mara mbili. Na aliyekosea, basi atapata malipo mara moja.

Na wanawapenda watu wa nyumba ya bwana Mtume -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- wenye kumuamini Mtume na ni vipenzi vyao, na wanawapenda wake za Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake- na wake hao ni mama wa Waumini na wanawaombea radhi wote. Na wanajiweka mbali na njia za Mashia ambao wanawachukia Maswahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na wanawatukana, na kuwasifia watu wa nyumba ya Mtume (Ahlul baiti) zaidi kupita kiasi, na kuwainua juu zaidi ya nafasi yao aliyowaweka Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu na utukufu. Vile vile, wanajiweka mbali na kundi la Nawaaswib, kundi ambalo linawaudhi watu wa nyumba ya Mtume (Ahlul baiti) kwa maneno na vitendo.

Na haya yote tuliyoyataja yanaingia kwenye itikadi sahihi ambayo Mwenyezi Mungu amemtuma Mtume wake Muhammad -rehema na mani ziwe juu yake- kwayo. Nayo ni itikadi ambayo ni wajibu kuiamini, kushikamana nayo, kunyooka juu yake na kujihadhari na itikadi zenye kupingana nayo. nayo pia ndiyo itikadi ya kundi lililofaulu la Ahlussunna waljamaa, kundi ambalo ameliongelea Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- kwa kusema: "Halitowacha kundi moja katika umma wangu kuwa washindi kwenye haki. Hawadhuriki na mwenye kuwaachilia mbali (bila usaidizi) mpaka ije amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu wakiwa vivyo hivyo."15 Na katika riwaya, ilikuja hadithi hii hivi: "Halitowacha kundi katika umma kunusuriwa kwenye haki."16 Na amesema Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Wamegawanyika Mayahudi katika makundi sabini na moja, nao Wakristo wamegawanyika katika makundi sabini na mbili. Na utagawanyika umma huu katika makundi sabini na tatu. Makundi hayo yote yataingia Motoni isipokuwa kundi moja." Tukasema: 'Ni la akina nani ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?' Akasema: "Yeyote atakayekuwa katika mfano wa yale niliyo nayo mimi na Maswahaba zangu."17

 

Itikadi zinazopingana na itikadi sahihi

Wenye kuipinga hii itikadi, na wenye kwenda kinyume nayo; ni makundi mengi. Miongoni mwao kuna wenye kuabudu Masanamu, Malaika, Mawalii, majini, miti, mawe na vinginevyo. Haya makundi yote hayakukubali wito wa Mitume, bali waliwapinga na hawakuwajali, kama ambavyo Makuraishi na makundi ya Waarabu walivyomfanyia Mtume wetu Muhammad - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Walikuwa wakiiomba miungu yao kuwakidhia haja zao, kuwaponya wagonjwa wao na kuwakinga kutokana na maadui zao. Pia walikuwa wakichinja kwa ajili yao na wakiweka nadhiri kwa ajili yao. Alipowakataza hayo Mtume -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na akawaamrisha kumfanyia ibada Mwenyezi Mungu peke yake, walishangaa jambo hilo na wakampinga na wakasema:

﴿أَجَعَلَ ٱلۡأٓلِهَةَ إِلَٰهٗا وَٰحِدًاۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيۡءٌ عُجَابٞ5﴾

"Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu sana." [Swad: 5]

Basi Mtume -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- hakuwacha kuwalingania kuelekea kwa Mwenyezi Mungu, kuwatahadharisha na ushirikina na kuwawekea wazi uhakika wa yale wanayoyalingania, mpaka Mwenyezi Mungu akawaongoza wale walioongoka miongoni mwao, kisha wakaingia baada ya hapo katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi na ikadhihiri dini ya Mwenyezi Mungu na kuzishinda dini zingine zote baada ya wito endelevu na Jihadi ndefu ya Mtume -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na Maswahaba zake, Mwenyezi Mungu awaridhie, na wale waliofuata baada yao kwa wema. Kisha hali ikabadilika, na viumbe wengi wakagubikwa na ujinga; na wengi wakarudi kwenye dini za zama za ujinga, kwa kuvuka mipaka kuhusiana na Manabii na mawalii, na kuwaomba na kuwataka msaada, na aina zingine za ushirikina. Na hawakujuwa maana ya neno "Laailaha ilallahu (hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu)" kama walivyojua maana yake makafiri wa Kiarabu. Basi Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuombwa msaada.

Ushirikina huu haujaacha kuendelea kuenea miongoni mwa watu hadi wakati wetu. Kwa sababu ya kuenea kwa ujinga na kuwepo kwa kipindi kirefu kutokea zama za unabii.

Na tuhuma zenye utata za hawa washirikina wa zamani ndizo tuhuma za utata za washirikina wa sasa, nazo ni kauli zao:

﴿...هَٰٓؤُلَآءِ شُفَعَٰٓؤُنَا عِندَ ٱللَّهِ...﴾

"Hawa ni waombezi wetu kwa Mwenyezi Mungu." [Yunus: 18], Na maneno yao waliposema:

﴿...مَا نَعۡبُدُهُمۡ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَآ إِلَى ٱللَّهِ زُلۡفَىٰٓ...﴾

"Sisi hatuwaabudu wao isipokuwa ili wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu." [Az-Zumar: 3]. Na hakika Mwenyezi Mungu alibatilisha utata huu, na akaweka wazi kuwa atakayemuabudu asiyekuwa Yeye awe atakavyokuwa, atakuwa ame mshirikisha Mwenyezi Mungu na amemkufuru, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَيَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَضُرُّهُمۡ وَلَا يَنفَعُهُمۡ وَيَقُولُونَ هَٰٓؤُلَآءِ شُفَعَٰٓؤُنَا عِندَ ٱللَّهِ...﴾

"Nao, badala ya Mwenyezi Mungu, wanaabudu wasiowadhuru wala kuwanufaisha, na wanasema: 'Hawa ndio waombezi wetu kwa Mwenyezi Mungu!" [Yunus: 18] Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu akawajibu kwa maneno yake:

﴿قُلۡ أَتُنَبِّـُٔونَ ٱللَّهَ بِمَا لَا يَعۡلَمُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَلَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ سُبۡحَٰنَهُۥ وَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ18﴾

"Sema: 'Je, mnamwambia Mwenyezi Mungu asiyoyajua yaliyoko katika mbingu wala katika ardhi? Sub-hanahu wa Taa'la (ametakasika na ametukuka) mbali na hao wanaomshirikisha naye.'" [Yunus: 18]

Basi Mwenyezi Mungu Mtukufu akaweka wazi katika aya hii kuwa kumuabudu asiyekuwa Yeye miongoni mwa Manabii na Mawalii au wengineo ni ushirikina ulio mkubwa hata wakiuita wenye kufanya hivyo kwa jina lingine. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿...وَٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءَ مَا نَعۡبُدُهُمۡ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَآ إِلَى ٱللَّهِ زُلۡفَىٰٓ...﴾

"Na wale waliowafanya walinzi wengine badala yake Yeye, Mwenyezi Mungu ni Mwangalizi bora juu yao. Wala wewe si wakili juu yao." [Az-Zumar: 3]. Kisha Mwenyezi Mungu akawajibu kwa kauli yake:

﴿...إِنَّ ٱللَّهَ يَحۡكُمُ بَيۡنَهُمۡ فِي مَا هُمۡ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي مَنۡ هُوَ كَٰذِبٞ كَفَّارٞ﴾

"Hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika yale wanayohitilafiana. Hakika Mwenyezi Mungu hamuongoi aliye muongo kafiri mno." [Az-Zumar: 3].

Basi Mwenyezi Mungu Mtukufu akaweka wazi kwa hayo kuwa kumuabudu kwao asiyekuwa Yeye kwa kuomba, kuhofu, kutaraji na mfano wa hayo ni kumkufuru Mwenyezi Mungu Mtukufu, na akaweka wazi kuwa kauli yao ni ya uongo waliposema kwamba miungu yao inawaweka karibu zaidi na Mwenyezi Mungu.

Na miongoni mwa itikadi za kikafiri ambazo zinapingana na itikadi iliyo sahihi, na zenye kwenda kinyume na waliyokuja nayo Mitume -rehema na amani ziwe juu yao- ni kile wanachoitakidi wenye kupinga uwepo wa Muumba wanaoishi katika zama hizi miongoni mwa wafuasi wa Marx, Lenin na wasiokuwa hao miongoni mwa walinganizi wa kutokuwepo kwa Muumba na walinganiao ukafiri. Ni sawa waliite hilo kwa jina la Ujamaa au Ukomunisti au Uamsho au yasiyokuwa hayo miongoni mwa majina mengine, hakuna tofauti. Kwani, msingi mkuu wa hawa wanao pinga uwepo wa Mwenyezi Mungu ni kuwa hakuna mungu na kuwa maisha yalipatikana kwa nyenzo tu.

Na miongoni mwa misingi yao ni kupinga kufufuliwa baada ya kufa, na kupinga uwepo wa Pepo na Moto na kupinga dini zote. Na atakayetazama kwenye vitabu vyao na kayasoma waliyokuwa nayo, atayafahamu hayo kwa yakini, na hapana shaka kuwa hizi itikadi zinapingana na dini zote za mbinguni, huwafikisha watu wake kwenye mwisho mbaya hapa duniani na akhera.

Na amiongoni mwa hizo itikadi zenye kupingana na haki, ni kile wanachoitakidi baadhi ya Masufi kwamba baadhi ya wanaowaita Mawalii wanashirikiana na Mwenyezi Mungu kupanga na kuendesha mambo ya ulimwengu, na wanawaita kwa majina ya Aq-twaab (viongozi wakubwa) na Autaad (vigogo) na Al-aghwaath (wasidizi na watoa huduma) na majina mengine ambayo wameyazusha kwa ajili ya miungu wao. Huu ni ushirikina katika umola, nao ndio aina mbaya sana ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na yeyote atakayefuatilia ushirikina wa washirikina wa zama za ujinga, na akaufananisha na wa washirikina wa zama hizi, atakuta kuwa ushirikina wa zama hizi ni mkubwa zaidi na wa hali ya juu, na kuliweka wazi hilo ni kama hivi: Ni kuwa makafiri wa Kiarabu katika zama za ujinga walijulikana kwa mambo mawili: Jambo la kwanza: Washirikina wa zamani hawakuwa wakishirikisha kwenye umola. Bali ushirikina wao ulikuwa kwenye ibada tu. Kwa maana walikuwa wakiukubali umola wa Mwenyezi Mungu peke yake -Mwenye nguvu na utukufu- kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّنۡ خَلَقَهُمۡ لَيَقُولُنَّ ٱللَّهُ...﴾

"Na ukiwauliza ni nani aliyewaumba? Bila ya shaka watasema: "Mwenyezi Mungu!'" [Az-Zukhruf: 87] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿قُلۡ مَن يَرۡزُقُكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ أَمَّن يَمۡلِكُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَٰرَ وَمَن يُخۡرِجُ ٱلۡحَيَّ مِنَ ٱلۡمَيِّتِ وَيُخۡرِجُ ٱلۡمَيِّتَ مِنَ ٱلۡحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ ٱلۡأَمۡرَۚ فَسَيَقُولُونَ ٱللَّهُۚ فَقُلۡ أَفَلَا تَتَّقُونَ31﴾

"Sema: Ni nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Au ni nani anayemiliki kusikia na kuona? Na ni nani amtoaye hai kutoka kwenye maiti, na akamtoa maiti kutoka kwa aliye hai? Na ni nani anayeyaendesha mambo yote? Watasema: Allah (Mwenyezi Mungu). Basi sema: Je, hamumchi?" [Yunus: 31]. Na Aya zenye maana hii ni nyingi sana.

Jambo la pili: Ushirikina wao katika ibada haukuwa ni wa muda wote, bali ulikuwa ukitokea wakati wa raha. Ama wakati wa shida, walikuwa wakimtakasia ibada Mwenyezi Mungu, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿فَإِذَا رَكِبُواْ فِي ٱلۡفُلۡكِ دَعَوُاْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ فَلَمَّا نَجَّىٰهُمۡ إِلَى ٱلۡبَرِّ إِذَا هُمۡ يُشۡرِكُونَ65﴾

"Na wanapopanda makafiri kwenye majahazi baharini, na wakaogopa kuzama, wanampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtakasia dua wakati wa shida yao. Na Anapowaokoa akawafikisha kwenye nchi kavu, na shida ikawaondokea, wanarudi kwenye ushirikina wao." [Al-Ankabut: 65].

Ama washirikina wa sasa, ushurikina wao umezidi zaidi ule wa wale wa mwanzo kwa sehemu mbili: Sehemu ya kwanza: Ushirikina wa baadhi yao kwenye umola Sehemu ya pili: Ushirikina wao wakati wa raha na shida, kama linavyofahamika hilo kwa aliyeishi nao na akawafutalia hali zao, na akayaona wanayoyafanya kwenye kaburi la Hussein na Badawiy na wengineo katika nchi ya Misri, na kwenye kaburi la Al'aidaruus huko Aden, na Al-Haadiy katika nchi ya Yemen, na Ibnu 'Arabiy huko Sham, na sheikh Abdulqadir Al-Jailaaniy katika nchi ya Iraq, na makaburi mengine yaliyo mashuhuri ambayo watu wengi wanayatukuza, na wakayaelekezea haki nyingi za Mwenyezi Mungu - Mwenye nguvu na utukufu. Hata hivyo, ni mara chache sana kupata wenye kuwakataza hayo na kuwabainishia ukweli wa Tauhiid ambayo Mwenyezi Mungu alimtuma nayo Mtume wake, rehema na amani ziwe juu yake, na Mitume waliokuwa kabla yake amani iwe juu yao. Basi sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu na kwake Yeye tutarejea.

Na miongoni mwa itikadi potofu zinazopingana na itikadi sahihi katika mlango wa majina na sifa za Mwenyezi Mungu, ni itikadi ya wazushi miongoni mwa kundi liitwalo Jahmiayyah na Muutazila na wenye kufuata njia zao katika kupinga sifa za Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu, na kuzikataa sifa zake Mwenyezi Mungu Mtukufu zenye ukamilifu, na badala yake wakamsifia kwa sifa za vitu visivyokuwepo, na visivyokuwa na uhai na visivyowezekana. Ametakasika Mwenyezi Mungu kuwa na sifa wanazomsifia utakasifu mkubwa wa hali ya juu.

Na anaingia katika itikadi potofu kila mwenye kupinga baadhi ya sifa na kukubali baadhi yake, kama vile kundi la Ashaaira. Kwa hakika, inawalazimu katika baadhi ya sifa walizozikubali waende sambamba na zile sifa ambazo walizikimbia na kuzikataa na wakabadilisha maana zake na wakawa ni wenye kwenda kinyume na ushahidi wa Kitabu na sunnah na ushahidi wa kiakili, na wakajitia katika mgongano ulio wazi kabisa kwenye suala hilo.

Ama Ahlussunna waljamaa, wao kwa hakika walimthibitishia Mwenyezi Mungu kile alichojithibitishia mwenyewe au kile alichomthibitishia Mtume wake Muhammad -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- miongoni mwa majina na sifa kwa ukamilifu, na wakamuweka mbali na kumtakasa kwa kutomfananisha na viumbe wake, utakaso ambao uko mbali na uchafu wa kukataa kwamba Mwenyezi Mungu ana majina na sifa, na wakaufanyia kazi ushahidi wote na hawakuubadilisha wala kuukataa, na wakasalimika kutokana na mgongano ambao ulitokea kwa wengine kama ilivyotangulia kuwekwa wazi jambo hilo.

 

Na hii ndiyo njia ya mafanikio, na maisha mazuri duniani na akhera, na ndiyo njia iliyonyooka waliyoifuata watu wema waliotangulia katika umma huu na viongizi wake. Hawawezi kuwa wema watu wa mwisho wa umma huu, isipokuwa kwa kufuata kile kilichowafanya wa mwanzo wao kuwa wema, nacho ni kufuata Kitabu na Sunna, na kuacha kila kinachokwenda tofauti na viwili hivyo. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aurudishe umma huu kwenye uongofu wake, na wawe wengi walingazi wa uongofu, na awawezeshe viongozi wake na wanawazuoni wake kuupiga vita ushirikina, na kuumaliza kabisa na kutahadharisha dhidi ya njia zake... hakika Yeye ni Mwenye kusikia, aliye karibu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuwezesha, naye ndiye Mwenye kututosheleza na Msimamizi mzuri zaidi, hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu. Na rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Nabii wetu Muhammad, na familia yake na Maswahaba wake.

***

 


Ameipokea Bukhari (2056) na Muslim (30).

Ameipokea Al-lalkaiy katika Ufafanuzi wa misingi ya itikadi (73 5), na Ibnu abdul barri katka Jaamiy al-ilmi wa fadh-luhu (1801), lakini kwa matamshi "hadithi mbalimbali" badaya ya "aya zenye sifa (za Mwenyezi Mungu)", na tamko lenyewe linasema hivi: "Zipokeeni hadithi hizi kama zilivyokuja wala msijadiliane kuhusiana nao."

Ameipokea Al-baihaqiy katika Al-asmaau wasswifaat (865), na Ibnu Taimiyat akasema kwamba hadithi hii ni sahihi katika kitabi kiitwacho Al-hamawiyyat (uk 269), na Adh-dhahabiy akasema katika kitabu kiitwacho Al-ir-dhwi (2/223): "Wapokezi wake ni maimamu waaminifu."

Ameipokea Al-Laalakaaiy katika Sharhi Usuulul Itikad (930), na Al-Baihaqiy katika Al-Asmaau wa swifaat (955).

Ameipokea Al-Laalakaaiy katika Sharhi Usuulul Itikad (665), na Al-Baihaqiy katika Al-Asmau was-Swifaat (868).

Ameipokea Al-Lalkaaiy katika Sharhi usuulul itikad (664), na Abuu Nu'aimu katika Hil-yatul auliyaa (6/325), na Baihaqiy katika Al-asmau wa swifaat (867)

Ameipokea Al-muzakkiy katika kitabu kiitwacho Al-muzakkiyat (29), na Ibnu Battwah katika Ibaanat (120), na Al-laalakaiy katika Sharh Usuululitiqad (663).

Ameipokea Al- daaramiy katika kuwajibu kundi la Jahamia (67) na Baihaqiy katika kitabu kiitwacho Al-asmaau wa swifaat (903).

Ameipokea Adh-Dhahabiy katika kitabu Al-Uluwwiy (464), na akasema Al-Albaniy katika Mukhtaswar Al-Uluwwiy (uk. 184): "Hii ni cheni sahihi, na wapokezi wake ni waaminifu na wanafahamika."

Tafsiri ya Ibnu Kathiir (3/426 427).

Ameipokea Al-Bukhariy (22) kutoka katika hadithi ya Abii Said Al-Khuduriy - radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie.

Ameipokea hadithi hii Imamu Muslim (2996), kutoka katika hadithi ya Aisha, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Ameipokea Bukhariy (3651) na Muslimu (2533), kutoka katika hadithi ya Abdullahi ibnu Masud - Mwenyezi Mungu amridhie.

Ameipokea Imamu Muslimu (1920) kutoka katika hadithi ya Thauban, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Ameipokea Ibnu Maajah (3953) kutoka katika hadithi ya Thauban, Mwenyezi Mungu amridhie, na kaisahihisha ibnu Hibban (6753), na Al-Haakim (8653).

Ameipokea At-Tirmidhiy (2641) kutoka katika hadithi ya Abdullahi ibnu Umar, radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie, na akasema Al-munaawiy katika kitabu cha Faidhul Qadiir (5/347): "Ndani yake kuna Abdurahman ibnu Ziyaad Al-ifriikiy. Amesema Adh-dhahabiy: 'Walisema kwamba ni dhaifu', naye Albaniy amesema kwamba ni sahihi katika Swahihul jaamiy (5343).

Ameipokea hadithi hii imamu Muslim (8)